You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
27<br />
kuwa jambo hilo limekuwa ni uzoefu unaoweza kubadili maisha yangu kwa<br />
mtindo wa kisanaa. Kamwe maishani mwangu sijapatapo kumsikia mtu<br />
mweusi akiongea kwa njia aliyoongea. Nami kwa haraka haraka nilitaka<br />
kuandaa nikutane naye ili nijaribu kumbadili na aingie dini yangu. Nilifurahia<br />
kuhubiri Injili, nikitaraji kuzipata nyoyo zilizopotea ili niziokoe ziepukane na<br />
Moto wa Jehannamu- bila kujali watu hao ni akina nani.<br />
Baada ya kumaliza chuo kikuu nilianza kufanya kazi kamili. Nilifikia kilele<br />
cha uchungaji wangu, huku wafuasi wa Elijah Muhammad wakiwa<br />
wanaonekana sana, na niliziheshimu juhudi zao za kujaribu kuiondoa jamii ya<br />
watu weusi waepukane na maovu ambayo yalikuwa yakiwaharibu. Nilianza<br />
kuwaunga mkono, akilini, kwa kununua maandiko yao na hata kukutana nao<br />
kwa mazungumzo. Nilihudhuria mazungumzo na masomo yao ili nijue nini<br />
hasa walichokuwa wanakiamini. Kwa namna niliyokuwa nawajua, wengi wao<br />
walikuwa waaminifu, lakini sikuweza kununua (kukubali) wazo la kuwa<br />
Mungu, ni mtu mweusi. Nilipinga utuimiaji wao wa Biblia kuunga mkono<br />
upande wao katika mambo maalumu. Hiki kilikuwa ndicho kitabu<br />
nilichokijua vizuri sana, na nilisumbuka sana kwa kile nilichokifikiria kuwa<br />
ni kufahamu vibaya kwao, na upotoshaji wao wa kitabu hicho. Nilienda shule<br />
ya Biblia ya mtaani na nikawa na elimu kubwa katika nyanja mbali mbali za<br />
masomo ya Biblia.<br />
Baada ya takriban miaka sita nilienda Texas na nikawa nashiriki katika<br />
makanisa mawili. La kwanza lilikuwa linaongozwa na mchungaji kijana<br />
ambaye alikuwa hana uzoefu wala elimu ya kutosha. Elimu yangu ya<br />
maandiko ya Kikristo kwa muda huo ilikuwa imeendelea kwa kitu kisicho cha<br />
kawaida. Nilijawa na mafundisho ya Kibiblia. Nikaanza kutazama kwa kina<br />
ndani ya maandiko na nikatambua kuwa nilikuwa ninajua zaidi kuliko<br />
kiongozi aliyekuwepo. Kwa kuonyesha heshima, nililiacha na kujiunga na<br />
kanisa lingine katika mji mwingine ambako nilihisi kuwa nitajifunza zaidi.<br />
Mchungaji wa kanisa hili la kipekee alikuwa ni mwanazuoni sana. Alikuwa ni<br />
mwalimu wa daraja la juu lakini alikuwa na baadhi ya ya fikra ambazo<br />
hazikuwa za kawaida kwa umoja wa kanisani kwetu. Yeye alikuwa na<br />
mitazamo ya kiliberali lakini bado nilikuwa nafurahia mafundisho yake.<br />
Punde tu nikajifunza somo la thamani sana juu ya maisha yangu ya Ukristo,<br />
ambalo lilikuwa ni “Kila king’acho si dhahabu” kinyume na umbile lake la<br />
nje, kulikuwa na uovu uliochukua nafasi ambao kamwe sijaufikiria kuwa<br />
unawezekana kuwepo kanisani. Uovu huo ulinisababishia nitafakari kwa kina,<br />
na kuanza kusaili mafundisho ambayo nilijizatiti nayo kwa sana.