08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

27<br />

kuwa jambo hilo limekuwa ni uzoefu unaoweza kubadili maisha yangu kwa<br />

mtindo wa kisanaa. Kamwe maishani mwangu sijapatapo kumsikia mtu<br />

mweusi akiongea kwa njia aliyoongea. Nami kwa haraka haraka nilitaka<br />

kuandaa nikutane naye ili nijaribu kumbadili na aingie dini yangu. Nilifurahia<br />

kuhubiri Injili, nikitaraji kuzipata nyoyo zilizopotea ili niziokoe ziepukane na<br />

Moto wa Jehannamu- bila kujali watu hao ni akina nani.<br />

Baada ya kumaliza chuo kikuu nilianza kufanya kazi kamili. Nilifikia kilele<br />

cha uchungaji wangu, huku wafuasi wa Elijah Muhammad wakiwa<br />

wanaonekana sana, na niliziheshimu juhudi zao za kujaribu kuiondoa jamii ya<br />

watu weusi waepukane na maovu ambayo yalikuwa yakiwaharibu. Nilianza<br />

kuwaunga mkono, akilini, kwa kununua maandiko yao na hata kukutana nao<br />

kwa mazungumzo. Nilihudhuria mazungumzo na masomo yao ili nijue nini<br />

hasa walichokuwa wanakiamini. Kwa namna niliyokuwa nawajua, wengi wao<br />

walikuwa waaminifu, lakini sikuweza kununua (kukubali) wazo la kuwa<br />

Mungu, ni mtu mweusi. Nilipinga utuimiaji wao wa Biblia kuunga mkono<br />

upande wao katika mambo maalumu. Hiki kilikuwa ndicho kitabu<br />

nilichokijua vizuri sana, na nilisumbuka sana kwa kile nilichokifikiria kuwa<br />

ni kufahamu vibaya kwao, na upotoshaji wao wa kitabu hicho. Nilienda shule<br />

ya Biblia ya mtaani na nikawa na elimu kubwa katika nyanja mbali mbali za<br />

masomo ya Biblia.<br />

Baada ya takriban miaka sita nilienda Texas na nikawa nashiriki katika<br />

makanisa mawili. La kwanza lilikuwa linaongozwa na mchungaji kijana<br />

ambaye alikuwa hana uzoefu wala elimu ya kutosha. Elimu yangu ya<br />

maandiko ya Kikristo kwa muda huo ilikuwa imeendelea kwa kitu kisicho cha<br />

kawaida. Nilijawa na mafundisho ya Kibiblia. Nikaanza kutazama kwa kina<br />

ndani ya maandiko na nikatambua kuwa nilikuwa ninajua zaidi kuliko<br />

kiongozi aliyekuwepo. Kwa kuonyesha heshima, nililiacha na kujiunga na<br />

kanisa lingine katika mji mwingine ambako nilihisi kuwa nitajifunza zaidi.<br />

Mchungaji wa kanisa hili la kipekee alikuwa ni mwanazuoni sana. Alikuwa ni<br />

mwalimu wa daraja la juu lakini alikuwa na baadhi ya ya fikra ambazo<br />

hazikuwa za kawaida kwa umoja wa kanisani kwetu. Yeye alikuwa na<br />

mitazamo ya kiliberali lakini bado nilikuwa nafurahia mafundisho yake.<br />

Punde tu nikajifunza somo la thamani sana juu ya maisha yangu ya Ukristo,<br />

ambalo lilikuwa ni “Kila king’acho si dhahabu” kinyume na umbile lake la<br />

nje, kulikuwa na uovu uliochukua nafasi ambao kamwe sijaufikiria kuwa<br />

unawezekana kuwepo kanisani. Uovu huo ulinisababishia nitafakari kwa kina,<br />

na kuanza kusaili mafundisho ambayo nilijizatiti nayo kwa sana.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!