You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
50<br />
4 - SISTA KHADIJA “SUE” WATSON ALIYEKUWA<br />
MCHUNGAJI, MMISHIONARI, NA PROFESA ANA<br />
STASHAHADA YA UZAMILI YA MASWALA YA THEOLOJIA<br />
(NI MMAREKANI MWENYE ASILI YA KIFILIPINO)<br />
“Nini kimekutokea?” Kila siku hicho ndicho kitendo rejeshi cha kwanza,<br />
ambacho nilikabiliana nacho. Wakati wanafunzi wenzangu wa zamani,<br />
marafiki na wachungaji wenzangu waliponiona baada ya kuingia <strong>Uislamu</strong>.<br />
Nadhani sikuweza kuwalaumu kwa kuwa mimi mwenyewe nilikuwa sipendi<br />
kabisa mtu abadili dini. Zamani, nilikuwa Profesa, mchungaji, mwasisi wa<br />
kanisa na mmishionari. Kama kuna mtu yeyote aliyekuwa na msimamo mkali<br />
kabisa, basi nilikuwa ni mimi.<br />
Baada ya kuhitimu stashahada ya uzamili ya theolojia kutoka katika seminari<br />
ya watu wenye vipaji na uwezo maalumu miezi mitano hapo kabla. Ilikuwa ni<br />
baada ya wakati huo nilipokutana na bibi mmoja ambaye aliwahi kufanya<br />
kazi nchini Saudi Arabia na ameshasilimu. Bila ya shaka nilimuuliza juu ya<br />
namna wanavyotendewa wanawake katika <strong>Uislamu</strong>. Nilishutushwa na jibu<br />
lake, kwani halikuwa ni lile niliolitarajia kwa hiyo, niliendelea kuuliza<br />
maswali mengine yanayohusiana na Allah na Muhammad amani iwe juu yake<br />
(S.A.W) 5 . Naye akanifahamisha kuwa atanipeleka katika kituo cha Kiislamu<br />
sehemu ambayo wataweza kujibu maswali yangu.<br />
Baada ya kusali- yaani kumuomba Yesu anikinge dhidi ya Shetani na pepo<br />
wabaya, ikionyesha kuwa kile tulichofundishwa kuhusu <strong>Uislamu</strong> kuwa ni dini<br />
ya mapepo na mashetani. Kwa kuwa nimeshafundishwa uinjilisti nilikuwa<br />
nimeshtushwa kabisa kabisa na ujaji wa Waislamu, kwani ulikuwa ni wa moja<br />
kwa moja na usio na mizengwe. Hakuna vitisho, hakuna bughudha, hakuna<br />
kutawaliwa kisaikolojia, hakuna kuvutwa bila ya kujihisi! Hakuna lolote<br />
katika hayo, “Acha tukupatie mafunzo ya Quran nyumbani mwako”, iwe ni<br />
kama mwenzi wa mafunzo ya Biblia. Sikuweza kuamini jambo hilo! Walinipa<br />
baadhi ya vitabu na wakaniambia kama nitakuwa na maswali wao wapo<br />
ofisini, tayari kuyajibu maswali hayo. Usiku huo nilisoma vitabu vyote<br />
walivyonipatia. Na hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kusoma kitabu juu<br />
ya <strong>Uislamu</strong> kilichoandikwa na Mwislamu, tumeshajifunza na kusoma vitabu<br />
juu ya <strong>Uislamu</strong> vilivyoandikwa na Wakristo tu! Siku iliyofuata nilitumia<br />
masaa matatu pale ofisini kwao nikiuliza maswali. Tukio hilo liliendelea kila<br />
5 Ni kifupi cha maneno ya Kiarabu na maana yake ni rehema na amani ziwe juu yake.