You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
39<br />
Baada ya miezi kumi na sita, kukutana na Jamal kuliongezeka kidogo kidogo<br />
na kuwa mara kwa mara, hadi ikawa mara moja kila wiki mbili na kufikia kila<br />
wiki. Katika safari hizo, Jamal kamwe hajanihubiria kuhusu <strong>Uislamu</strong>, kamwe<br />
hajaniuliza kuhusu imani ya dini yangu au ninachokikinai, na kamwe<br />
hajapendekeza kwa mdomo kuwa niwe Mwislamu. Hata hivyo, nilianza<br />
kujifunza mengi. Kwanza kabisa, kulikuwa na mfano wa matendo ya daima<br />
kutoka kwa Jamal wa kunionyesha vipindi vya sala zake za kila siku. Pili<br />
kulikuwa na mfano wa kimwenendo wa namna Jamal alivyokuwa<br />
akiyaendesha maisha yake ya kila siku kwa unyofu wa hali ya juu na tabia ya<br />
maadili, anafanya yote mawili hayo katika ulimwengu wake wa kibiashara na<br />
katika ulimwengu wake wa kijamii. Tatu, kulikuwa na mfano wa<br />
kimwenendo juu ya namna Jmal anavyohusiana na watoto wake wawili. Kwa<br />
mke wangu, mke wa Jamal alitoa mifano hiyo hiyo. Nne, daima kulikuwa na<br />
wigo wa kunisaidia nifahamu historia ya farasi wa Uarabuni wa Mashariki ya<br />
Kati, Jamal alianza kushirikiana nami: 1) visa vya Warabu na historia ya<br />
<strong>Uislamu</strong>; 2) hadithi za Mtume Muhammad, rehema ziwe juu yake; na 3) aya<br />
za Quran na mijadala yake inayozingatia muktadha na ifanyayo kituo juu ya<br />
baadhi ya mitazamo ya Kiislamu, lakini daima alikuwa anaiwasilisha kwa<br />
istilahi za kunisaidia kifikra ili nifahamu muktadha wa <strong>Uislamu</strong> katika<br />
historia ya farasi wa Uarabuni. Kamwe sijaambiwa kuwa “hivi ndivyo vitu<br />
vilivyo”, nilikuwa naambiwa “hivi ndivyo Waislamu wanavyoamini” tu. Kwa<br />
kuwa sikuwa “nahubiriwa,” na kwa kuwa Jamal kamwe hajataka imani<br />
yangu, sikuhitaji kujisumbua na kujaribu kutetea upande wangu. Mambo yote<br />
yalifanyika kiakili, na si kama mbadilishaji dini.<br />
Kidogo kidogo, Jamal alianza, kututambulisha kwa familia za Waarabu<br />
wengine katika jamii ya Waislamu wa mtaani. Kulikuwa na Wa’eli na familia<br />
yake, Khalidi na familia yake, na wengine wachache kwa unyofu, niliona mtu<br />
mmoja na familia ambazo zilikuwa zinaishi maisha yao kwa maadili ya hali<br />
ya juu, yaliyo sawa sawa kuliko jamii ya Kimarekani ambayo kwayo sisi sote<br />
tulikuwa ndani yake. Huenda kulikuwa na jambo katika matendo ya <strong>Uislamu</strong><br />
niliyokuwa nayakosa wakati nilipokuwa mwanachuo na katika siku za<br />
seminari.<br />
Hadi Desemba, 1992, nilianza kujiuliza baadhi ya maswali makali juu ya<br />
wapi nilipokuwepo na nilikuwa ninafanya nini. Maswali hayo yalichochewa<br />
na nadhari zifuatazo. 1) Baada ya kozi ya awali ya miezi kumi na sita, maisha<br />
yetu ya kijamii yalianza kukua katika kutilia maanani wigo wa Waarabu wa