08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

12- PADRI MKUU VIACHESLAV POLOSIN (URUSI).<br />

90<br />

Viacheslay Sergeevich Polosin alizaliwa mwaka 1956. Mwaka 1979 alihitimu<br />

kitengo cha falsafa cha MGU na mnamo 1984 alihitimu Seminari ya makasisi<br />

Moscow. Alikuwa ni padri msimikwa na alihudumia parokia katika dayosisi<br />

ya Asia ya kati na Kaluga ya RPTS. Mwaka 1990 alinyanyuliwa daraja ya<br />

upadri mkuu. Mwaka huo huo alichaguliwa kaimu wa watu wa RSFSR<br />

kutoka jimbo la Kaluga na aliongoza tume ya mamlaka kuu kabisa ya Soviet,<br />

alihitimu katika shule ya kidiplomasia ya wizara ya mambo ya nje na kutetea<br />

makala zake juu ya madai ya: “Kanisa la Kiothodoksi la Kirusi na hali ya<br />

USSR, 1971-1991.” Kuanzia 1993 amekuwa ni mwajiriwa wa kazi za serikali<br />

ya Duma katika Baraza la harakati za kidemokrasia ya Kikristo ya Kirusi na<br />

ni mwanachama wa baraza la umoja wa Kikristo. Mwaka 1991, alienda likizo<br />

kutokea dayosisi ya Kaluga na tangu mwaka 1995 hajasalisha katika Liturujia<br />

(kawaida ya ibada ya usharika mtakatifu). Katika mahojiano yake na jarida la<br />

Musulmane yeye, kirasmi alijiita Mwislamu: “Ninazingatia kuwa Quran ni<br />

ufunuo wa mwisho duniani, ulioteremshwa kwa Mtume Muhammad. Hakuna<br />

Mola ispokuwa ni Mungu Mmoja, Allah, na Muhammad ni Mtume wake.”<br />

Viacheslav Polosin ni mtunzi wa kazi nyingi za kisomi juu ya mambo ya<br />

kihistoria, kisiasa, kidini, na mada za kifalsafa. Mwezi Februari wa mwaka<br />

huo alitetea makala nyingine juu ya mada: “Lahaja ya visa vya kubuniwa na<br />

waundaji wa visa vya kubuni vya kisiasa.” Mawazo yake ya msingi ya<br />

kifalsafa ni kukiwasilisha kitabu chake “visa vya kubuni, Dini, na hali.”<br />

(Moscow, 1999).<br />

Katika mahojiano na jarida “Musulmane;” VIACHESLAV POLOSIN<br />

alisema kuwa <strong>Uislamu</strong> haujaanza kutokana na Ukristo lakini ni mapinduzi ya<br />

pili na makuu ya imani ya Mungu Mmoja imani ya Ibrahimu. Ibrahimu<br />

alikuwa anaamini Mungu Mmoja na alikuwa ni mtu wa kwanza kueleza<br />

jambo hili wazi wazi. Alitangaza jambo hilo na alilithibitisha kwa mafanikio,<br />

akawa “baba” wa waumini wote. Baadaye utamaduni huo ukakatizwa na<br />

mkengeuko. Hilo linajulikana kwa kuwa Mitume yote na wengi wao vilevile<br />

wanaitwa “waokozi”… wakiwakosoa watu kwa mkengeuko wao na<br />

kutumbukia katika upagani na ukafiri. Na Mtume mkuu ambaye ni Yesu,<br />

vilevile alikosoa watu kwa kukengeuka na kuingia ukafiri. Zaidi ya hayo,<br />

Yesu yeye mwenyewe alijizungumzia nafsi yake kwa mafumbo kuwa<br />

ametumwa na Mungu kufanya kazi maalumu. Kabla watu hawa kusema:<br />

“Mitume ni watu kama sisi.” Lakini Mungu amempeleka Malaika wa Mungu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!