You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
12- PADRI MKUU VIACHESLAV POLOSIN (URUSI).<br />
90<br />
Viacheslay Sergeevich Polosin alizaliwa mwaka 1956. Mwaka 1979 alihitimu<br />
kitengo cha falsafa cha MGU na mnamo 1984 alihitimu Seminari ya makasisi<br />
Moscow. Alikuwa ni padri msimikwa na alihudumia parokia katika dayosisi<br />
ya Asia ya kati na Kaluga ya RPTS. Mwaka 1990 alinyanyuliwa daraja ya<br />
upadri mkuu. Mwaka huo huo alichaguliwa kaimu wa watu wa RSFSR<br />
kutoka jimbo la Kaluga na aliongoza tume ya mamlaka kuu kabisa ya Soviet,<br />
alihitimu katika shule ya kidiplomasia ya wizara ya mambo ya nje na kutetea<br />
makala zake juu ya madai ya: “Kanisa la Kiothodoksi la Kirusi na hali ya<br />
USSR, 1971-1991.” Kuanzia 1993 amekuwa ni mwajiriwa wa kazi za serikali<br />
ya Duma katika Baraza la harakati za kidemokrasia ya Kikristo ya Kirusi na<br />
ni mwanachama wa baraza la umoja wa Kikristo. Mwaka 1991, alienda likizo<br />
kutokea dayosisi ya Kaluga na tangu mwaka 1995 hajasalisha katika Liturujia<br />
(kawaida ya ibada ya usharika mtakatifu). Katika mahojiano yake na jarida la<br />
Musulmane yeye, kirasmi alijiita Mwislamu: “Ninazingatia kuwa Quran ni<br />
ufunuo wa mwisho duniani, ulioteremshwa kwa Mtume Muhammad. Hakuna<br />
Mola ispokuwa ni Mungu Mmoja, Allah, na Muhammad ni Mtume wake.”<br />
Viacheslav Polosin ni mtunzi wa kazi nyingi za kisomi juu ya mambo ya<br />
kihistoria, kisiasa, kidini, na mada za kifalsafa. Mwezi Februari wa mwaka<br />
huo alitetea makala nyingine juu ya mada: “Lahaja ya visa vya kubuniwa na<br />
waundaji wa visa vya kubuni vya kisiasa.” Mawazo yake ya msingi ya<br />
kifalsafa ni kukiwasilisha kitabu chake “visa vya kubuni, Dini, na hali.”<br />
(Moscow, 1999).<br />
Katika mahojiano na jarida “Musulmane;” VIACHESLAV POLOSIN<br />
alisema kuwa <strong>Uislamu</strong> haujaanza kutokana na Ukristo lakini ni mapinduzi ya<br />
pili na makuu ya imani ya Mungu Mmoja imani ya Ibrahimu. Ibrahimu<br />
alikuwa anaamini Mungu Mmoja na alikuwa ni mtu wa kwanza kueleza<br />
jambo hili wazi wazi. Alitangaza jambo hilo na alilithibitisha kwa mafanikio,<br />
akawa “baba” wa waumini wote. Baadaye utamaduni huo ukakatizwa na<br />
mkengeuko. Hilo linajulikana kwa kuwa Mitume yote na wengi wao vilevile<br />
wanaitwa “waokozi”… wakiwakosoa watu kwa mkengeuko wao na<br />
kutumbukia katika upagani na ukafiri. Na Mtume mkuu ambaye ni Yesu,<br />
vilevile alikosoa watu kwa kukengeuka na kuingia ukafiri. Zaidi ya hayo,<br />
Yesu yeye mwenyewe alijizungumzia nafsi yake kwa mafumbo kuwa<br />
ametumwa na Mungu kufanya kazi maalumu. Kabla watu hawa kusema:<br />
“Mitume ni watu kama sisi.” Lakini Mungu amempeleka Malaika wa Mungu