08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

51<br />

siku kwa wiki moja, kwa muda huo tayari nilikuwa nimeshasoma vitabu 12<br />

na kujua kwa nini Waislamu ni watu wagumu zaidi duniani kubadili dini na<br />

kuwa Wakristo. Kwa nini? Kwa sababu hakuna kitu cha kuwapa!! (Katika<br />

<strong>Uislamu</strong>) kuna kufungamana na Allah, kusamehewa dhambi, uwokovu na<br />

kuahidiwa maisha ya milele.<br />

Kikawaida, swali langu la kwanza lilitilia umuhimu suala la Uungu wa Allah.<br />

Ni nani huyu Allah ambaye Waislamu wanamwabudu? Sisi kama Wakristo<br />

tumeshafundishwa kuwa huyo ni Mungu mwingine, Mungu wa uongo.<br />

Wakati, kwa hakika yeye ndiye Mjuzi, Mwenye nguvu, na Aliye hai. Mmoja<br />

asiye na mshirika wala aliye sawa naye. Ni jambo la kuvutia kujua kuwa<br />

kulikuwa na maaskofu katika kipindi cha miaka mia tatu ya mwanzoni ya<br />

kanisa ambao walikuwa wanafundisha kama wanavyofundisha Waislamu<br />

kuwa Yesu (A.S) 6 alikuwa ni Mtume na si Mwana wa Mungu!! Na ilikuwa ni<br />

baada ya mageuzi ya utawala ya mfalme Constantine kuwa yeye ndiye<br />

aliyekuwa wa kwanza kutangaza na kujulisha imani ya utatu. Yeye alikuwa ni<br />

mtu aliyebadili dini na kuwa Mkristo ambaye hajui lolote la kidini na<br />

aliitambulisha itikadi ya kipagani ambayo historia yake inarejea zama za<br />

Mababyloni. Kwa sababu nafasi hainiruhusu kuingia katika maelezo kwa<br />

upana juu ya somo hilo insha-Allah, nitazungumza hayo mara nyingine. Kitu<br />

pekee ambacho ni lazima nikizungumze ni neno utatu kuwa halimo katika<br />

Biblia, katika tafsiri nyingi za Biblia wala halipatikani katika Biblia ya<br />

Kigiriki au ya Kiyahudi!<br />

Swali langu muhimu jengine lilitilia umuhimu juu ya Muhammad (S.A.W).<br />

Ni nani huyu Muhammad? Nimegundua kuwa Waislamu hawamwabudu<br />

kama vile Wakristo wanavyomwabudu Yesu. Yeye si mpatanishi na kwa<br />

hakika ni haramu kumwabudu. Tunamuombea abarikiwe mwishoni mwa sala<br />

zetu lakini vilevile Tunamuombea Abrahamu naye abarikiwe. Yeye ni Mtume<br />

na ni mjumbe, Mtume wa mwisho. Kwa hakika, hadi sasa, ni miaka elfu moja<br />

mia nne na kumi na nane imeshapita hakuna Mtume yeyote baada yake.<br />

Ujumbe wake ni kwa watu wote ikiwa ni kinyume na ujumbe wa Yesu au<br />

Musa (rehema ziwe juu yao) ambao walitumwa kwa Wayahudi. “Sikia ee<br />

Israeli” lakini ujumbe wenyewe ni ule ule ujumbe wa Allah. “Yesu akamjibu,<br />

Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;”<br />

(Marko 12:29)<br />

6 Ni kifupi cha maneno ya Kiarabu yenye maana Iwe juu yake amani.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!