You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
56<br />
“Nasi tulipousikia uwongofu tuliuamini; basi anayemwamini Mola wake<br />
hataogopa kupunjwa wala kutwikwa (kubebeshwa) dhambi (za mtu<br />
mwengine).” (Qurani 72:13)<br />
Nilihisi faraja ya kina usiku huo na niliporudi nyumbani niliupitisha usiku<br />
wote nikiwa peke yangu katika maktaba yangu nikisoma Qurani. Mke wangu<br />
alitaka nimjulishe lengo la kukesha kwangu usiku kucha na nilimweleza<br />
aniache peke yangu. Nilisimama kusoma kwa muda mrefu nikifikiria na<br />
kutafakari juu ya aya; “Lau kama Tungaliiteremsha hii Quran juu ya mlima,<br />
ungaliuona ukinyenyekea (na) kupasuka kwa sababu ya hofu ya Mwenyezi<br />
Mungu. Na hii ni mifano Tunawapigia (Tunawaeleza) watu ili wafikiri.”<br />
(Qurani 59:21) na “Hakika utawakuta walio maadui zaidi kuliko watu<br />
(wengine) kwa Waislamu ni Mayahudi na wale mushirikina (wasiokuwa na<br />
Kitabu), na utawaona walio karibu kwa urafiki na Waislamu ni wale<br />
wanaosema: “Sisi ni Wakristo.” (Hayo) ni kwa sababu wako miongoni mwao<br />
wanavyuoni na wamchao Mungu, na kwa sababu wao (Wakristo)<br />
hawatakabari; (wakijua haki huifuata). Na wanaposikia yaliyoteremshwa<br />
kwa Mtume (na yakawatulilikia kuwa ni kweli), utaona macho yao<br />
yanamiminika machozi kwa sababu ya haki waliyoitambua; wanasema:<br />
“Mola wetu! Tumeamini, basi tuandike pamoja na wanaoshuhudia (ukweli<br />
huu).” (Na wakilaumiwa kwa kusilimu kwao husema): “Na kwa nini<br />
tusimwamini Mwenyezi Mungu na haki iliyotufikia, na hali tunatumai Mola<br />
wetu atuingize (Peponi) pamoja na watu wema?” (Qurani 5:82-84).<br />
Bwana Khalil kisha alinukuu nukuu ya tatu kutoka katika Quran Tukufu<br />
isemayo; “Ambao wanamfuata Mtume, Nabii aliye Ummy (asiyejua kusoma<br />
wala kuandika, na juu ya hivi atafundisha mafundisho hayo ya ajabu ya<br />
<strong>Uislamu</strong>), ambaye wanamuona ameandikwa kwao katika Taurati na Injili<br />
ambaye anawaamrisha mema na anawakataza yaliyo mabaya, na<br />
kuwahalalishia vizuri na kuwaharamishia vibaya, na kuwaondolea mizigo<br />
yao na minyororo iliyokuwa juu yao (yaani sharia ngumu za zamani na mila<br />
za kikafiri). Basi wale waliomwamini yeye na kumuhishimu na kumsaidia na<br />
kuifuata Nuru iliyoteremshwa pamoja naye (yaani Qurani) hao ndiyo wenye<br />
kufaulu. Sema (Ewe Nabii Muhammad): “Enyi watu; Hakika mimi ni Mtume<br />
wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote; (Mungu) ambaye anao ufalme wa<br />
mbingu na ardhi, hapana aabudiwaye (kwa haki) ila Yeye; Yeye ndiye<br />
Ahuishaye na ndiye Afishaye. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume<br />
Wake, aliye Nabii Ummy (asiyejua kusoma na wala kuandika) ambaye