08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

5<br />

vile?” “Kwa nini tunaamini dhambi ya asili?” na “Kwa nini wanadamu<br />

wamelazimishwa wakubali ‘dhambi’ za Adamu na kisha matokeo yake<br />

waadhibiwe milele?” Lakini kama utamuuliza mtu yeyote maswali hayo,<br />

watakujibu kuwa unalazimika uamini bila ya kuhoji, au kuwa hiyo ni “siri<br />

isiyoelezwa” na hutakiwi kuuliza “Kaka wewe amini tu.”<br />

Maana ya Utatu<br />

Jambo la kushangaza sana, neno ‘utatu’ halimo katika Biblia. Na limekuwa<br />

likihusishwa na wanazuoni wa kidini mapema mnamo miaka mia mbili baada<br />

ya kunyanyuliwa kwa Yesu kwenda kwa Mungu wake Muweza.<br />

Ningewaomba wahubiri na wachungaji wanipe japo fikra, vipi ‘moja’<br />

itapigwa hesabu ili iwe ‘tatu’ au vipi Mungu mwenyewe awezaye kufanya<br />

kila kitu atakacho, hawezi kuwasamehe watu na dhambi zao, isipokuwa hadi<br />

ajifanye mwanadamu, aje chini duniani, awe mtu, na kisha achukuwe<br />

madhambi ya watu wote; huku tukiweka akilini kuwa pamoja na hayo yote<br />

yeye ni Mungu wa Ulimwengu wote na anafanya atakalo kulifanya, popote<br />

pale, ndani na nje ya ulimwengu kama tunavyojua. Hao wahubiri na<br />

wachungaji kamwe hawaonyeshi kuwa wataweza kuleta kitu kingine zaidi ya<br />

maoni yao au mlinganisho wa kiajabu ajabu.<br />

Baba - Mchungaji Msimikwa Asiye Na Madhehebu<br />

Baba yangu alikuwa mchangamfu sana katika kuunga mkono kazi za kanisa,<br />

na hasa hasa vipindi vya shule ya kanisa. Akasimikwa ukasisi katika miaka ya<br />

sabini. Yeye na mkewe (mama yangu wa kambo) walikuwa wanawajua<br />

wainjilisti na wahubiri wa kwenye tv wengi, vilevile wameshamtembelea Oral<br />

Roberts na wamesaidia kujenga ‘mnara wa sala’ katika Tulsa, pia walikuwa ni<br />

waungaji mkono imara wa Jimmy Swaggart, Jim na Tommy Fae Bakker,<br />

Jerry Fallwell, John Haggi na Pat Robertson.<br />

Kukutana na Mtu Kutokea Misri<br />

Ilikuwa ni mwanzoni mwa 1991 pale baba yangu alipoanza kufanyabiashara<br />

na mtu kutoka Misri na kuniambia kuwa anataka nikutane na mtu huyo. Wazo<br />

hilo lilinivutia kwani niliwaza juu ya wazo la kuwa na ladha ya kimataifa.<br />

Unajua tena, mapiramidi, Sphinx, mto Naili na mengineyo.<br />

Alikuwa ni ‘Mwislamu’: Watekajinyara, Walipuaji mabomu, Magaidi,<br />

na ni nani ajuaye kingine ni nini?

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!