Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
5<br />
vile?” “Kwa nini tunaamini dhambi ya asili?” na “Kwa nini wanadamu<br />
wamelazimishwa wakubali ‘dhambi’ za Adamu na kisha matokeo yake<br />
waadhibiwe milele?” Lakini kama utamuuliza mtu yeyote maswali hayo,<br />
watakujibu kuwa unalazimika uamini bila ya kuhoji, au kuwa hiyo ni “siri<br />
isiyoelezwa” na hutakiwi kuuliza “Kaka wewe amini tu.”<br />
Maana ya Utatu<br />
Jambo la kushangaza sana, neno ‘utatu’ halimo katika Biblia. Na limekuwa<br />
likihusishwa na wanazuoni wa kidini mapema mnamo miaka mia mbili baada<br />
ya kunyanyuliwa kwa Yesu kwenda kwa Mungu wake Muweza.<br />
Ningewaomba wahubiri na wachungaji wanipe japo fikra, vipi ‘moja’<br />
itapigwa hesabu ili iwe ‘tatu’ au vipi Mungu mwenyewe awezaye kufanya<br />
kila kitu atakacho, hawezi kuwasamehe watu na dhambi zao, isipokuwa hadi<br />
ajifanye mwanadamu, aje chini duniani, awe mtu, na kisha achukuwe<br />
madhambi ya watu wote; huku tukiweka akilini kuwa pamoja na hayo yote<br />
yeye ni Mungu wa Ulimwengu wote na anafanya atakalo kulifanya, popote<br />
pale, ndani na nje ya ulimwengu kama tunavyojua. Hao wahubiri na<br />
wachungaji kamwe hawaonyeshi kuwa wataweza kuleta kitu kingine zaidi ya<br />
maoni yao au mlinganisho wa kiajabu ajabu.<br />
Baba - Mchungaji Msimikwa Asiye Na Madhehebu<br />
Baba yangu alikuwa mchangamfu sana katika kuunga mkono kazi za kanisa,<br />
na hasa hasa vipindi vya shule ya kanisa. Akasimikwa ukasisi katika miaka ya<br />
sabini. Yeye na mkewe (mama yangu wa kambo) walikuwa wanawajua<br />
wainjilisti na wahubiri wa kwenye tv wengi, vilevile wameshamtembelea Oral<br />
Roberts na wamesaidia kujenga ‘mnara wa sala’ katika Tulsa, pia walikuwa ni<br />
waungaji mkono imara wa Jimmy Swaggart, Jim na Tommy Fae Bakker,<br />
Jerry Fallwell, John Haggi na Pat Robertson.<br />
Kukutana na Mtu Kutokea Misri<br />
Ilikuwa ni mwanzoni mwa 1991 pale baba yangu alipoanza kufanyabiashara<br />
na mtu kutoka Misri na kuniambia kuwa anataka nikutane na mtu huyo. Wazo<br />
hilo lilinivutia kwani niliwaza juu ya wazo la kuwa na ladha ya kimataifa.<br />
Unajua tena, mapiramidi, Sphinx, mto Naili na mengineyo.<br />
Alikuwa ni ‘Mwislamu’: Watekajinyara, Walipuaji mabomu, Magaidi,<br />
na ni nani ajuaye kingine ni nini?