You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
24<br />
2 – ABDULLAH M. AL-FARUQUE ALIYEKUWA AKIIITWA<br />
KENETH L. JENKINS, MCHUNGAJI NA MZEE WA KANISA<br />
LA PENTECOSTAL. (USA)<br />
Nikiwa ni mchungaji na ni mzee wa kanisa la Kristo, hapo zamani, ilikuwa ni<br />
wajibu wangu kuwaelimisha wale wote wanaoendelea kutembea kizani.<br />
Baada ya kuingia <strong>Uislamu</strong> nilihisi haja kubwa mno ya kuwasaidia wale wote<br />
wasiobarikiwa na kupata nuru ya Kiislamu.<br />
Namshukuru Mungu Muweza, Allah, anihurumie, anijaalie niujue uzuri wa<br />
<strong>Uislamu</strong> kama ulivyofundishwa na Mtume Muhammad na maswahaba 4 zake<br />
waongofu. Ni kwa rehema za Allah tu, ya kwamba sisi tunapokea uongofu wa<br />
kweli kweli na uwezo wa kufuata njia iliyonyooka, inayoongoza katika<br />
mafanikio katika maisha haya na ya kesho ahera.<br />
Mungu asifiwe kwa wema niliofanyiwa na sheikhi “Abdallah bin Abdul-<br />
Azeez bin Baz” wa Falme ya Saudi Arabia juu ya kuingia kwangu <strong>Uislamu</strong>.<br />
Naishi kwa matumaini na nitapitia juu ya elimu yote iliyopatikana kutokana<br />
na kila kikao nlichokaa naye. Kuna wengine wengi walionisaidia kwa kunipa<br />
nguvu na kunielimisha. Ni jambo la kutosha kusema kuwa namshukuru<br />
Mungu Muweza, Allah, kwa madada na makaka wote walioruhusiwa na<br />
Mungu kushiriki katika ukuaji na maendeleo yangu nikiwa Mwislamu.<br />
Naiombea kazi hii fupi, iwe ni kwa faida ya wote. Natarajia Wakristo<br />
watagundua kuwa bado kuna matarajio licha ya masharti ya ukaidi<br />
yanayoshawishi makundi mengi ya Wakristo. Ufumbuzi wa matatizo ya<br />
Wakristo haupatikani kwa Wakristo wenyewe, kwani wao, kwa namna<br />
4 Swahaba ni mfuasi wa Mtume Muhammad (S.A.W) aliyekuwepo zama za Mtume.