You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
6<br />
Kisha baba yangu alieleza kuwa mtu huyo ni ‘Mwislamu.’ Awali, nilichukia<br />
wazo la kukutana na mtu asiye na imani, mtekajinyara, mlipuaji mabomu,<br />
gaidi, kafiri.’ Mtu yeyote wa kawaida angelikataa wazo hilo. Sikuamini<br />
masikio yangu. Mwislamu?’ Haiwezekani! Nilimkumbusha baba yangu<br />
mambo mbali mbali tuliyoyasikia juu ya watu hao ‘Waislamu.’<br />
Uongo dhidi ya Waislamu na <strong>Uislamu</strong> – walitwambia, kuwa Waislamu:<br />
• Hata hawaamini Mungu.<br />
• Wanaabudu boksi jeusi liliopo jangwani.<br />
• Na wanabusu ardhi mara tano kwa siku.<br />
Haiwezekani! Sikutaka Kukutana Naye!<br />
Sikutaka kukutana na Mwislamu huyo. Haiwezekani! Baba yangu alisisitiza<br />
nikutane naye na akanihakikishia kuwa mtu huyo ni mwema sana. Hilo<br />
lilikuwa ni kubwa mno kwangu. Na hasa hasa walokole tuliokuwa tunasafiri<br />
nao wote waliwachukia sana Waislamu na <strong>Uislamu</strong>. Hata walikuwa wakisema<br />
vitu visivyo vya kweli ili kuwatisha watu waougope <strong>Uislamu</strong>. Kwa hiyo, kwa<br />
nini mimi nihitaji kitu cha kufanya na watu hao?<br />
Wazo: ‘Kumbadilisha Awe Mkristo.’<br />
Kisha wazo fulani lilinijia, ‘Tunaweza kumbadili mtu huyo awe Mkristo.’<br />
Kwa hiyo, nilikubali na kuafiki kukutana naye. Lakini kwa masharti yangu.<br />
Nikutane naye nikiwa na Biblia, Msalaba na kofia ya chopeo (kepu)<br />
iliyoandikwa ‘Yesu ni Bwana.’ Nilikubali nikutane naye siku ya Jumapili<br />
baada ya kutoka kanisani. Kwa hiyo, sote tungesali na kusimama vizuri na<br />
Bwana. Ningechukua Biblia yangu chini ya kwapa kama desturi. Ningekuwa<br />
na msalaba wangu mkubwa ung`aao na kuning`inia pia ningevaa kofia yangu<br />
isemayo: ‘Yesu ni Bwana.’ Maandishi yaliyo kwa mkato upande wa mbele.<br />
Mke wangu na mabinti zangu wawili wadogo wangekuja na sote tungekuwa<br />
tayari kwa kukabiliana kwa mara ya kwanza na ‘Waislamu.’<br />
Yupo wapi? Nilipoingia dukani na kumuuliza baba; “Huyo Mwislamu yupo<br />
wapi”, aliashiria na kusema: “Yule pale.” Nilichanganyikiwa. Huyo hawezi<br />
kuwa Mwislamu. Haiwezekani.<br />
Kiremba na midevu? Nalitafuta jitu kubwa lenye majoho yanayoburura,<br />
mremba mkubwa kichwani mwake, midevu inayofikia nusu ya shati lake na