You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
64<br />
nimeshawasamehe, kwa hakika alipata muda wa kusuluhishwa na baba yake<br />
kabla hajaiaga dunia.<br />
“Hao wazazi walikuwa ni wazee wasiojiweza. Walikuwa hawajui hata<br />
kuisoma Biblia… Chote walichokijuwa ilikuwa ni kile walichokisikia<br />
kikisomwa na mapadri” anaelezea. Baada ya kuomba akae kwa usiku mmoja<br />
tu, mchana uliofuatia, alianza safari yake ya kuelekea kule kwenye asili ya<br />
wazazi wake, Kyela, karibu na mpaka kati ya Tanzania na Malawi. Wazazi<br />
wake walifanya makazi mjini Kilosa, Morogoro. Katika safari yake hiyo,<br />
alikwamia Basale, kwa familia moja ambayo ilikuwa inauza pombe<br />
zilizosindikwa nyumbani. Na ilikuwa ni hapo ndipo alipokutana na mkewe<br />
wa baadaye, ambaye ni mtawa wa Kikatoliki, jina lake ni Sista Gertrude<br />
Kibweya, kwa sasa anajulikana kwa jina la Sister Zainabu. Na ilikuwa ni<br />
pamoja naye ndipo Mwaipopo aliposafiri hadi Kyela, ambako yule mzee,<br />
aliyempa hifadhi kwa usiku uliopita alipomwambia kuwa hiyo ndiyo namna<br />
Mwaipopo atavyowapata Waislamu wengine. Lakini kabla ya hivyo, wakati<br />
wa asubuhi ya siku hiyo alipopiga adhana, kitu kilichowafanya wanakijiji<br />
watoke, huku wakimuuliza mwenyeji wake kwa nini alikuwa anamuhifadhi<br />
“mwendawazimu.” Alikuwa ni yule mtawa ndiye aliyeeleza kuwa mimi<br />
sikuwa mwendawazimu, ispokuwa ni Mwislamu” anasema Mwaipopo. Na<br />
alikuwa ni mtawa huyo huyo aliyemsaidia Mwaipopo hapo baadaye kulipia<br />
ada ya matibabu katika hospitali ya Misheni ya Kianglikana, alipokuwa<br />
mgonjwa sana, shukrani kwa mazungumzo aliyoyafanya na mtawa huyo.<br />
Kisa chenyewe kinaenda hivi, Mwaipopo alipomuuliza mtawa huyo kwa nini<br />
alikuwa anavaa shanga ya Rozali, naye akajibu kuwa ni kwa sababu Yesu<br />
Kristo alisulubiwa msalabani. “Lakini, hebu sema, kama mtu amemuua baba<br />
yako na bunduki, Je, utatembea huku umebeba bunduki kifuani kwako?”<br />
Mmmhhh. Hilo lililmfanya yule mtawa afikirie, akili zake zikapata<br />
“changamoto”, na Askofu wa zamani alimuomba amuoe hapo baadaye,<br />
jawabu lilikuwa “sawa”. Walioana kwa siri, na wiki nne baadaye, huyo<br />
mtawa aliandika barua kwa viongozi wake, akiwajulisha kuwa anaondoka.<br />
Wakati yule mzee aliyempa hifadhi Mwaipopo, (mjomba wa mtawa)<br />
aliposikia juu ya ndoa hiyo, na Mwaipopo na mkewe walipofika nyumbani<br />
kwa mzee huyo, walishauriwa wahame nyumba hiyo, kwa sababu “yule mzee<br />
alikuwa anashindilia bunduki yake”, na Baba wa yule mtawa alikasirika sana,<br />
“alikuwa mkali kama simba”.