08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

64<br />

nimeshawasamehe, kwa hakika alipata muda wa kusuluhishwa na baba yake<br />

kabla hajaiaga dunia.<br />

“Hao wazazi walikuwa ni wazee wasiojiweza. Walikuwa hawajui hata<br />

kuisoma Biblia… Chote walichokijuwa ilikuwa ni kile walichokisikia<br />

kikisomwa na mapadri” anaelezea. Baada ya kuomba akae kwa usiku mmoja<br />

tu, mchana uliofuatia, alianza safari yake ya kuelekea kule kwenye asili ya<br />

wazazi wake, Kyela, karibu na mpaka kati ya Tanzania na Malawi. Wazazi<br />

wake walifanya makazi mjini Kilosa, Morogoro. Katika safari yake hiyo,<br />

alikwamia Basale, kwa familia moja ambayo ilikuwa inauza pombe<br />

zilizosindikwa nyumbani. Na ilikuwa ni hapo ndipo alipokutana na mkewe<br />

wa baadaye, ambaye ni mtawa wa Kikatoliki, jina lake ni Sista Gertrude<br />

Kibweya, kwa sasa anajulikana kwa jina la Sister Zainabu. Na ilikuwa ni<br />

pamoja naye ndipo Mwaipopo aliposafiri hadi Kyela, ambako yule mzee,<br />

aliyempa hifadhi kwa usiku uliopita alipomwambia kuwa hiyo ndiyo namna<br />

Mwaipopo atavyowapata Waislamu wengine. Lakini kabla ya hivyo, wakati<br />

wa asubuhi ya siku hiyo alipopiga adhana, kitu kilichowafanya wanakijiji<br />

watoke, huku wakimuuliza mwenyeji wake kwa nini alikuwa anamuhifadhi<br />

“mwendawazimu.” Alikuwa ni yule mtawa ndiye aliyeeleza kuwa mimi<br />

sikuwa mwendawazimu, ispokuwa ni Mwislamu” anasema Mwaipopo. Na<br />

alikuwa ni mtawa huyo huyo aliyemsaidia Mwaipopo hapo baadaye kulipia<br />

ada ya matibabu katika hospitali ya Misheni ya Kianglikana, alipokuwa<br />

mgonjwa sana, shukrani kwa mazungumzo aliyoyafanya na mtawa huyo.<br />

Kisa chenyewe kinaenda hivi, Mwaipopo alipomuuliza mtawa huyo kwa nini<br />

alikuwa anavaa shanga ya Rozali, naye akajibu kuwa ni kwa sababu Yesu<br />

Kristo alisulubiwa msalabani. “Lakini, hebu sema, kama mtu amemuua baba<br />

yako na bunduki, Je, utatembea huku umebeba bunduki kifuani kwako?”<br />

Mmmhhh. Hilo lililmfanya yule mtawa afikirie, akili zake zikapata<br />

“changamoto”, na Askofu wa zamani alimuomba amuoe hapo baadaye,<br />

jawabu lilikuwa “sawa”. Walioana kwa siri, na wiki nne baadaye, huyo<br />

mtawa aliandika barua kwa viongozi wake, akiwajulisha kuwa anaondoka.<br />

Wakati yule mzee aliyempa hifadhi Mwaipopo, (mjomba wa mtawa)<br />

aliposikia juu ya ndoa hiyo, na Mwaipopo na mkewe walipofika nyumbani<br />

kwa mzee huyo, walishauriwa wahame nyumba hiyo, kwa sababu “yule mzee<br />

alikuwa anashindilia bunduki yake”, na Baba wa yule mtawa alikasirika sana,<br />

“alikuwa mkali kama simba”.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!