Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
37<br />
zaidi; 3)- mabadiliko ya itikadi hizo kama ya nafsi tatu kwa moja ya Mungu<br />
na uwana wa Yesu, amani iwe juu yake; 4)- mambo ya wasiokuwa na dini<br />
yapo katika kanuni za imani na mafundisho ya Wakristo wengi; 5)- kuwepo<br />
kwa makanisa yote hayo ya mwanzo na harakati za Kikristo ambazo<br />
hazikubali itikadi ya utatu wa Mungu, na ambazo kamwe hazikubali itikadi ya<br />
uungu wa Yesu, amani iwe juu yake; 6)- mengineyo (baadhi ya matunda haya<br />
ya elimu yangu ya seminari yanasimulia habari nyingi zaidi katika kitabu<br />
changu kipya, Msalaba na Mwezi; mazungumzo ya imani mchanganyiko<br />
kati ya Ukristo na <strong>Uislamu</strong>, yaliyochapishwa na Amana Publications<br />
2001.)<br />
Kwa hiyo, si ajabu kabisa kuwa wanaomaliza masomo ya seminari wengi wao<br />
wanatoka kutoka katika seminari si kwenda “kujaza majukwaa,” sehemu<br />
ambayo wataombwa wahubiri kile wanachokijua kuwa si cha kweli, lakini<br />
kinyume chake wanajiingiza katika kazi mbali mbali za ushauri. Hali hiyo<br />
ndiyo iliyonikumba, kwani nilijiendeleza ili nipate stashahada ya uzamili na<br />
udaktari ya matibabu ya kisaikolojia. Niliendelea kujiita Mkristo, kwa sababu<br />
hilo lilikuwa linahitajika kwa ajili ya kujitambulisha, na kwa kuwa nilikuwa<br />
Mkristo, baada ya yote, ni mchungaji msimikwa, hata hivyo, kazi yangu ni<br />
kazi ya kutibu magonjwa ya kiakili. Hata hivyo, elimu yangu ya seminari<br />
ilikuwa ni kinga dhidi ya imani ya kuamini utatu wa Mungu, au uungu wa<br />
Yesu, amani iwe juu yake. (Kura za maoni mara kwa mara zinabainisha kuwa<br />
wachungaji wanaimani ndogo katika kuamini mambo hayo na imani<br />
nyinginezo za kanisa kuliko walei (waumini wa kawaida) wanaowahudumia,<br />
kwa sitiari, huku wakazi wa parokia wakifahamu jambo hilo kimaneno tu.)<br />
Mimi nilikuwa Mkristo wa Krismasi na Pasaka.” Naenda kanisani mara moja<br />
moja sana, kisha nikakerekeza meno yangu na kuuma ulimi wangu<br />
nilipokuwa nasikiliza mahubiri yaliotetea kile nilichokijua kuwa hakikuwa<br />
kadhia husika.<br />
Hakuna hata moja katika hayo yaliyopita liwezalo kuchukuliwa ili lionyeshe<br />
kuwa mimi nilikuwa nina upeo wa dini mdogo au uelewa wa kiroho mdogo<br />
kuliko vile nilivyokuwa zamani. Nilikuwa ninasali kila siku, imani yangu kwa<br />
Mungu Mkuu ilibaki imara na salama, na niliendesha maisha yangu binafsi<br />
katika mstari pamoja na maadili niliyofundishwa kanisani na katika shule ya<br />
Jumapili. Kiwepesi, nilikuwa ninajua lilobora zaidi kuliko kununua imani<br />
zilizotengenezwa na mtu na mamlaka za kiimani za usharika wa kanisa,<br />
ambazo zilikuwa zimeshehenezwa mambo mazito mazito ya kipagani, fikra