08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

76<br />

8- GEORGE ANTHONY – ALIYEKUWA PADRI WA<br />

KIKATOLIKI (SRI LANKA)<br />

Fr. Anthony alikuwa ni padri wa Kikatoliki nchini Sri-lanka. Masimulizi yake<br />

ya kuwa muumini wa kweli na kuchagua jina la Abdulrahmani ni jambo la<br />

kuvutia sana. Kwani kwa kuwa padri wa Kikatoliki kwa hakika alikuwa na<br />

ujuzi sana wa mafundisho ya Biblia. Alikuwa ananukuu Biblia mara kwa<br />

mara pale alipokaa na kutusimulia safari yake ya kuingia <strong>Uislamu</strong>. Alipokuwa<br />

anasoma Biblia aligundua migongano mingi ndani yake. Anaendelea kunukuu<br />

Aya za Biblia kwa lugha ya Kisri-lanka na kuonyesha utata.<br />

Ananukuu Esaih 29:12 isemayo: “Kisha chuo hiki apewa mtu asiye na<br />

maarifa, akaambiwa, Kisome hicho tafadhali, akasema, Sina maarifa mimi.”<br />

Aya hii ni utabiri wa Mtume Muhammad (S.A.W), kwa sababu Muhammad<br />

(S.A.W), ndiye aliyekuwa Mtume asiyejua kusoma na kwa kuwa yeye ndiye<br />

Mtume asiyejua kusoma na alipotakiwa na malaika Jibrilu asome ufunuo<br />

mtakatifu wa kwanza mbele yake alisema; “Mimi si msomi” na hii ni<br />

kinyume na imani ya Kikristo kuwa Yesu ni Mungu, huku Matendo ya<br />

Mitume 2:22 ya Biblia Takatifu inayomchukulia Yesu kuwa ni mtu. Inasema;<br />

“Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu<br />

aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo<br />

Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe<br />

mnavyojua;”<br />

Ukristo na dini nyinginezo, haziuelezei utume kwa uwazi kwa mujibu wa<br />

kauli yake. Wala Ubudha na ukimya wake juu ya Mitume wengine. Kinyume<br />

na hayo, kwani katika <strong>Uislamu</strong> ni lazima kuamini Mitume yote iliyotangulia<br />

na kuwaheshimu. Kwa mujibu wa Abdulrahmani imani hii ni ya kukinaisha<br />

kabisa na ni ya kupendeza kwa kila mtu. Abdulrahmani anasema kuwa<br />

hakuna sababu ya kuwazuia mapadri wa Kikatoliki wasioe, wakati mapadri<br />

wa madhehebu mengine ya Kikristo wnaoa. Abdulrahmani alikuwa<br />

anatafakari juu ya mkorogeko wa imani ya Kikristo wakati huo huo alipata<br />

mkanda wa kaseti wa padri wa Kikristo wa Kisir-lanka aliyesilimu Shareef D.<br />

Alwis. Mkanda wa Ahmad Deedat pia ulimvutia. Juhudi zake za kuendelea<br />

kuupata ukweli mwishowe zilitoa matokeo ya kumbadili dini na kuwa<br />

Mwislamu. Fr. Goerge Anthony.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!