You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
76<br />
8- GEORGE ANTHONY – ALIYEKUWA PADRI WA<br />
KIKATOLIKI (SRI LANKA)<br />
Fr. Anthony alikuwa ni padri wa Kikatoliki nchini Sri-lanka. Masimulizi yake<br />
ya kuwa muumini wa kweli na kuchagua jina la Abdulrahmani ni jambo la<br />
kuvutia sana. Kwani kwa kuwa padri wa Kikatoliki kwa hakika alikuwa na<br />
ujuzi sana wa mafundisho ya Biblia. Alikuwa ananukuu Biblia mara kwa<br />
mara pale alipokaa na kutusimulia safari yake ya kuingia <strong>Uislamu</strong>. Alipokuwa<br />
anasoma Biblia aligundua migongano mingi ndani yake. Anaendelea kunukuu<br />
Aya za Biblia kwa lugha ya Kisri-lanka na kuonyesha utata.<br />
Ananukuu Esaih 29:12 isemayo: “Kisha chuo hiki apewa mtu asiye na<br />
maarifa, akaambiwa, Kisome hicho tafadhali, akasema, Sina maarifa mimi.”<br />
Aya hii ni utabiri wa Mtume Muhammad (S.A.W), kwa sababu Muhammad<br />
(S.A.W), ndiye aliyekuwa Mtume asiyejua kusoma na kwa kuwa yeye ndiye<br />
Mtume asiyejua kusoma na alipotakiwa na malaika Jibrilu asome ufunuo<br />
mtakatifu wa kwanza mbele yake alisema; “Mimi si msomi” na hii ni<br />
kinyume na imani ya Kikristo kuwa Yesu ni Mungu, huku Matendo ya<br />
Mitume 2:22 ya Biblia Takatifu inayomchukulia Yesu kuwa ni mtu. Inasema;<br />
“Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu<br />
aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo<br />
Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe<br />
mnavyojua;”<br />
Ukristo na dini nyinginezo, haziuelezei utume kwa uwazi kwa mujibu wa<br />
kauli yake. Wala Ubudha na ukimya wake juu ya Mitume wengine. Kinyume<br />
na hayo, kwani katika <strong>Uislamu</strong> ni lazima kuamini Mitume yote iliyotangulia<br />
na kuwaheshimu. Kwa mujibu wa Abdulrahmani imani hii ni ya kukinaisha<br />
kabisa na ni ya kupendeza kwa kila mtu. Abdulrahmani anasema kuwa<br />
hakuna sababu ya kuwazuia mapadri wa Kikatoliki wasioe, wakati mapadri<br />
wa madhehebu mengine ya Kikristo wnaoa. Abdulrahmani alikuwa<br />
anatafakari juu ya mkorogeko wa imani ya Kikristo wakati huo huo alipata<br />
mkanda wa kaseti wa padri wa Kikristo wa Kisir-lanka aliyesilimu Shareef D.<br />
Alwis. Mkanda wa Ahmad Deedat pia ulimvutia. Juhudi zake za kuendelea<br />
kuupata ukweli mwishowe zilitoa matokeo ya kumbadili dini na kuwa<br />
Mwislamu. Fr. Goerge Anthony.