08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

42<br />

ya kujitambulisha, ilikuwa ni muhimu sana katika kurekebisha matibabu ya<br />

kisaikolojia. Na hii ndiyo iliyokuwa sehemu ngumu sana kimatibabu.<br />

Kubadilisha msingi wa fikra za mtu za kujitambulisha ni kazi ngumu sana.<br />

Akili ya mtu inang`ang`ania mambo ya zamani na yaliyozoeleka, ambayo<br />

yanaonekana ni yenye kutia raha sana kisaikolojia na ni yenye usalama sana<br />

kuliko mambo mapya na yasiyozoeleka.<br />

Kwa msingi wa kazi, nilikuwa na elimu hiyo, na niliitumia kila siku. Hata<br />

hivyo, kwa dhihaka ya kutosha, sikuwa tayari kuutumia msingi huo kwa nafsi<br />

yangu mwenyewe, na katika kadhia yangu ya kusitasita iliyozunguka<br />

utambulisho wangu wa kidini. Kwa miaka 43, utambulisho wangu wa kidini<br />

kimaridadi ulikuwa ni jina la “Ukristo” hata hivyo, sifa nyingi niliweza<br />

kuziongeza katika jambo hilo kwa miaka mingi. Kuacha jina hilo la<br />

kujitambulishia dhati binafsi, lilikuwa si rahisi. Lilikuwa ni sehemu na fuko la<br />

namna nilivyofahamu kuwepo kwangu. Kupewa faida ya kung’amua, ni wazi<br />

kuwa kusita kwangu kulihudumia lengo la kuhakikisha kuwa nitunze<br />

utambulisho wangu wa kidini niliouzoea wa kuwa mimi ni Mkristo, ingawa ni<br />

Mkristo ambaye anaamini kama wanavyoamini Waislamu.<br />

Na ilikuwa mwishoni kabisa mwa Desemba, mimi na mke wangu tulipokuwa<br />

tukijaza fomu za maombi ya pasipoti za US, kwa hiyo, safari<br />

iliyopendekezwa ya kwenda mashariki ya kati imekuwa ni ya uhakika. Moja<br />

ya swali lilikuwa ni kuhusu ushiriki wa kidini. Hata sikufikiria jambo hilo, na<br />

bila kufikiri nikaangukia kule kule kwa zamani na mazoea, nilifungwa katika<br />

“Ukristo.” Ulikuwa ni mwepesi na ulikuwa uliozoeleka, na wenye kutia raha.<br />

Hata hivyo, raha hivyo ilikuwa ni ya muda tu na ilivurugika pale mke wangu<br />

aliponiuliza vipi nilijibu swali la utambulisho wa dini katika fomu ya<br />

maombi. Nami haraka haraka nilijibu “Mkristo”, na kuchekelea chini chini<br />

kunakosikika. Sasa, moja ya nadharia ya udadisi ya Kifreudi inayosaidia<br />

kufahamu nafasi ya mwanadamu ilikuwa ni kutambua kuwa kicheko mara<br />

nyingine ni tiba ya mfadhahiko wa kisaikolojia. Hata hivyo, nadharia ya<br />

udadisi ya Kifreudi inaweza ikawa katika mitazamo mingi ya nadharia yake<br />

ya mwendelezo wa saikolojia ya ngono, utambuzi wake katika kicheko<br />

ulikuwa katika lengo kabisa. Nilicheka! Nini kilikuwa mfadhaiko wa<br />

kisaikolojia ambao nililazimika kuutuliza kupitia kicheko cha wastani?<br />

Kisha haraka haraka niliendelea kumpa mke wangu maelezo mafupi<br />

yanayothibitisha kuwa nilikuwa Mkristo na sio Mwislamu. Katika kujibu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!