Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
17<br />
Kwa mujibu wa mabaki ya tafsiri ya Biblia juu ya Yesu, Mungu amrehemu,<br />
hajahubiri habari za uwokovu kwa kumwabudu yeye. Jambo hili<br />
limeongezwa baada yake na Saul (ambaye baadaye akawa Paulo). Tunapata<br />
maelezo ya wazi kabisa yanayoashiria uwokovu utakaokuja kupitia kumkiri<br />
Mungu Muweza kuwa ni Mungu mmoja na kumwabudu kwa moyo wote,<br />
akili na nguvu zote tu! Yesu, Amani iwe juu yake, amefundisha wafuasi wake<br />
waabudu hivi “Mungu wangu Ndiye Mungu Wenu, Mola wangu Ndiye Mola<br />
wenu.”<br />
Kwa mara nyingine, kwa mujibu wa tafsiri ya Biblia ya Kingereza iliyobaki,<br />
tunamuona mtu aangukwaye msalabani akilia kwa kusihi sana, “Eloi, Eloi,<br />
lama sabakhthani? (Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?)”<br />
Sentensi hii juu ya msalaba kwa uwazi kabisa inaonyesha kuwa yule mtu<br />
aliye msalabani hajafurahishwa na hali hiyo na wala haichukulii hali hiyo<br />
kuwa ni haki au uadilifu. Kwa hiyo, mtu lazima ahitimishe jambo hilo kuwa<br />
lilikuwa ni kitu ambacho hakikutakiwa na Yesu wala kukubaliwa au<br />
vinginevyo ni mtu mwingine aliyekuwa msalabani katika nafasi yake. Kwa<br />
njia yeyote ile utakavyolitazama jambo hilo, mtu aliyekuwa msalabani<br />
hakukubali jambo hilo kuwa ni mpango wa uwokovu.<br />
Quran kwa ukamilifu inapingana na mafundisho hayo, na Waislamu<br />
wanamwabudu Mungu na Bwana yule yule wa Yesu, Musa, Ibrahimu na<br />
Adamu, amani iwe juu yao. Quran katika sehemu nyingi inaeleza, hakuna mtu<br />
atakayebebeshwa kazi za dhambi za Mwingine, wala hakuna mtu atakaye<br />
beba mzigo wa mwingine. Sote tutakuwa na mambo yetu wenyewe siku hiyo.<br />
Na ninamuomba Allah awerehemu na awasamehe wote waliomwamini,<br />
aamiin.<br />
Ninajiona kuwa sijaacha mafundisho ya Yesu Kristo, (amani iwe juu yake).<br />
Kinyume chake, nahisi kuwa nipo karibu na Yesu, amani iwe juu yake, na<br />
ninatarajia kurejea kwake hapa duniani kuliko nilivyokuwa zamani. Kwa sasa<br />
ninamwabudu Mungu yule yule anayemwabudu na ninamtumikia Bwana yule<br />
yule anayemtumikia, katika njia ile ile aifanyao. Yesu alimuomba Mungu<br />
Muweza, na alifundisha wafuasi wake wafanye hayo hayo. Mimi kwa wepesi<br />
kabisa ninafanya kile alichokiamrisha kwa uwezo wangu na ninamuomba<br />
Mungu Muweza anikubalie matendo yangu.<br />
2. “Je, unadhani kuwa ni kweli “umeokolewa” na kwa hakika<br />
umezaliwa upya?”