08.06.2013 Views

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

Makasisi Waingia Uislamu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

17<br />

Kwa mujibu wa mabaki ya tafsiri ya Biblia juu ya Yesu, Mungu amrehemu,<br />

hajahubiri habari za uwokovu kwa kumwabudu yeye. Jambo hili<br />

limeongezwa baada yake na Saul (ambaye baadaye akawa Paulo). Tunapata<br />

maelezo ya wazi kabisa yanayoashiria uwokovu utakaokuja kupitia kumkiri<br />

Mungu Muweza kuwa ni Mungu mmoja na kumwabudu kwa moyo wote,<br />

akili na nguvu zote tu! Yesu, Amani iwe juu yake, amefundisha wafuasi wake<br />

waabudu hivi “Mungu wangu Ndiye Mungu Wenu, Mola wangu Ndiye Mola<br />

wenu.”<br />

Kwa mara nyingine, kwa mujibu wa tafsiri ya Biblia ya Kingereza iliyobaki,<br />

tunamuona mtu aangukwaye msalabani akilia kwa kusihi sana, “Eloi, Eloi,<br />

lama sabakhthani? (Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?)”<br />

Sentensi hii juu ya msalaba kwa uwazi kabisa inaonyesha kuwa yule mtu<br />

aliye msalabani hajafurahishwa na hali hiyo na wala haichukulii hali hiyo<br />

kuwa ni haki au uadilifu. Kwa hiyo, mtu lazima ahitimishe jambo hilo kuwa<br />

lilikuwa ni kitu ambacho hakikutakiwa na Yesu wala kukubaliwa au<br />

vinginevyo ni mtu mwingine aliyekuwa msalabani katika nafasi yake. Kwa<br />

njia yeyote ile utakavyolitazama jambo hilo, mtu aliyekuwa msalabani<br />

hakukubali jambo hilo kuwa ni mpango wa uwokovu.<br />

Quran kwa ukamilifu inapingana na mafundisho hayo, na Waislamu<br />

wanamwabudu Mungu na Bwana yule yule wa Yesu, Musa, Ibrahimu na<br />

Adamu, amani iwe juu yao. Quran katika sehemu nyingi inaeleza, hakuna mtu<br />

atakayebebeshwa kazi za dhambi za Mwingine, wala hakuna mtu atakaye<br />

beba mzigo wa mwingine. Sote tutakuwa na mambo yetu wenyewe siku hiyo.<br />

Na ninamuomba Allah awerehemu na awasamehe wote waliomwamini,<br />

aamiin.<br />

Ninajiona kuwa sijaacha mafundisho ya Yesu Kristo, (amani iwe juu yake).<br />

Kinyume chake, nahisi kuwa nipo karibu na Yesu, amani iwe juu yake, na<br />

ninatarajia kurejea kwake hapa duniani kuliko nilivyokuwa zamani. Kwa sasa<br />

ninamwabudu Mungu yule yule anayemwabudu na ninamtumikia Bwana yule<br />

yule anayemtumikia, katika njia ile ile aifanyao. Yesu alimuomba Mungu<br />

Muweza, na alifundisha wafuasi wake wafanye hayo hayo. Mimi kwa wepesi<br />

kabisa ninafanya kile alichokiamrisha kwa uwezo wangu na ninamuomba<br />

Mungu Muweza anikubalie matendo yangu.<br />

2. “Je, unadhani kuwa ni kweli “umeokolewa” na kwa hakika<br />

umezaliwa upya?”

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!