You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
vitatu ambavyo ni dhamiri, ushirika na utambuzi. Kwa kuwa asili<br />
ya karama za kiroho ni “hali ya kiungu” (supernatural source) na<br />
hutenda kazi kutokea ndani ya roho yake.<br />
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, tunajifunza ya kuwa<br />
Roho Mtakatifu ndiye mdhibiti mkuu wa karama na vipawa vya<br />
huduma za kiroho. Hatua ya kwanza kazi ya Roho Mtakatifu ni<br />
kumzaa mtu mara ya pili (Yoh. 3:3), na tunafundishwa hali hii ya<br />
kuzaliwa mara ya pili hufanyika ndani ya roho ya mtu (Yoh. 3:6).<br />
Baada ya Roho Mtakatifu kumzaa upya mtu katika roho<br />
yake, hatua ya pili ni kujaa ndani ya mtu na kufanya makao ya<br />
kudumu ndani roho ya binadamu. Na humo ndimo utendaji wa<br />
karama za Roho pamoja na vipawa vya huduma za kiroho hutokea<br />
na kudhihirika katika nafsi ya mtu.<br />
11