14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Angalizo<br />

Si kila kukosoa ni mtazamo hasi. Wala kuona makosa<br />

na kuyasema kwa nia ya kusahihisha sio vibaya. Muktadha<br />

wa kipengele hiki ni kwa wale walioathiriwa na “tabia sugu ya<br />

kulalamika na kuhukumu wengine”.<br />

Mtu ambaye hajaathiriwa na tabia sugu ya kulalamika<br />

na kuhukumu wengine anapoona makosa huchukua hatua za<br />

kumwendea mkosaji na kumwelimisha kwa nia njema na lugha<br />

ya upole, tena baada ya kumsikiliza kwanza na kupata uhakika<br />

kutoka kwa muhusika.<br />

Lakini mwathirika wa tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu<br />

wengine, hata kama analalamikia mambo ya kweli, huwa hatumii<br />

njia ya kuelimisha bali lugha ya kudhalilisha hadharani kwa kuanika<br />

makosa ya wengine. Tatizo huwa sio “kuona makosa” bali “njia ya<br />

kushughukilia makosa yenyewe”<br />

Mtu ambaye ni mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika<br />

na kuhukumu wengine” anaweza hata kujitetea ya kwamba ana<br />

mzigo wa kuwasaidia wale anaowakosoa wajirekebishe; lakini<br />

lugha inayotumika katika kukosoa ni ya kuudhi, kuumiza hisia,<br />

kudhalilisha, na kuwavunjia heshima wengine hadharani, wale<br />

anaodai kuwakosoa.<br />

Dalili Kuu Za Tabia Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />

Ulalamishi<br />

Mlalamishi ni mtu mwenye hulka ya kutokuridhika<br />

na mambo ya wengine. Hata pale mambo yakifanyika vizuri<br />

walalamishi hawana shukrani wala pongezi kwa wengine. Lakini<br />

likitokea dosari au udhaifu wao wataukomalia huo utafikiri hakuna<br />

jambo jema kwa wale wanaolalamikiwa.<br />

59

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!