Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Angalizo<br />
Si kila kukosoa ni mtazamo hasi. Wala kuona makosa<br />
na kuyasema kwa nia ya kusahihisha sio vibaya. Muktadha<br />
wa kipengele hiki ni kwa wale walioathiriwa na “tabia sugu ya<br />
kulalamika na kuhukumu wengine”.<br />
Mtu ambaye hajaathiriwa na tabia sugu ya kulalamika<br />
na kuhukumu wengine anapoona makosa huchukua hatua za<br />
kumwendea mkosaji na kumwelimisha kwa nia njema na lugha<br />
ya upole, tena baada ya kumsikiliza kwanza na kupata uhakika<br />
kutoka kwa muhusika.<br />
Lakini mwathirika wa tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu<br />
wengine, hata kama analalamikia mambo ya kweli, huwa hatumii<br />
njia ya kuelimisha bali lugha ya kudhalilisha hadharani kwa kuanika<br />
makosa ya wengine. Tatizo huwa sio “kuona makosa” bali “njia ya<br />
kushughukilia makosa yenyewe”<br />
Mtu ambaye ni mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika<br />
na kuhukumu wengine” anaweza hata kujitetea ya kwamba ana<br />
mzigo wa kuwasaidia wale anaowakosoa wajirekebishe; lakini<br />
lugha inayotumika katika kukosoa ni ya kuudhi, kuumiza hisia,<br />
kudhalilisha, na kuwavunjia heshima wengine hadharani, wale<br />
anaodai kuwakosoa.<br />
Dalili Kuu Za Tabia Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />
Ulalamishi<br />
Mlalamishi ni mtu mwenye hulka ya kutokuridhika<br />
na mambo ya wengine. Hata pale mambo yakifanyika vizuri<br />
walalamishi hawana shukrani wala pongezi kwa wengine. Lakini<br />
likitokea dosari au udhaifu wao wataukomalia huo utafikiri hakuna<br />
jambo jema kwa wale wanaolalamikiwa.<br />
59