14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Udhalilishaji<br />

Mdhalilishaji ni mtu anayezua mambo ya uongo kwa nia ya<br />

kuharibu heshima na hadhi za wengine hadharani. Mdhalilishaji<br />

huzalisha kashfa ili kuharibu maisha ya wengine.<br />

“Basi wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na<br />

husuda na masingizio yote.” (1 Pet. 2:1)<br />

Madhara Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />

Hudhoofisha Ubunifu Wa Kipaji<br />

Mwathirika wa mtazamo hasi wa kulalamika na kuhukumu<br />

hukiathiri kipaji chake cha asili kwa kudhoofisha uwezo wake wa<br />

asili wa kubuni mambo mapya. Kumbuka ya kwamba utendaji wa<br />

kipaji unategemea nguvu za ubunifu wa mambo mapya. Na nguvu<br />

za ubunifu hutokana na mawazo chanya.<br />

Kimaumbile “mawazo hasi” hayawezi kutenda kazi kwa<br />

wakati mmoja na “mawazo chanya”. Kila kimoja kinafanya kazi<br />

kwa wakati wake kinapokuwa kimepewa nafasi ya kwanza. Kwa<br />

hiyo, “mawazo hasi” huamsha “hisia hasi” ambazo huwa kikwazo<br />

cha utendaji wa mawazo chanya. Wakati mwathirika wa mtazamo<br />

hasi hutumia mawazo hasi na kughubikwa na hisia hasi; hali hiyo<br />

huzuia upande wa pili wa mawazo chanya na hisia chanya kufanya<br />

kazi kwa wakati mmoja.<br />

Changamoto iliyopo hapa ni kwamba, muda wote ambapo<br />

mawazo hasi, na hisia hasi vinatenda kazi ndani ya mwathirika,<br />

kipaji chake kinakuwa kimefungiwa ule uwezo wake wa kutenda<br />

kazi yenye tija kwa muhusika. Kwa hiyo, muda mwingi unaopotea<br />

kwenye kulalamika na kuhukumu wengine, mambo yake<br />

mwenyewe husimama au kukwama.<br />

61

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!