Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Udhalilishaji<br />
Mdhalilishaji ni mtu anayezua mambo ya uongo kwa nia ya<br />
kuharibu heshima na hadhi za wengine hadharani. Mdhalilishaji<br />
huzalisha kashfa ili kuharibu maisha ya wengine.<br />
“Basi wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na<br />
husuda na masingizio yote.” (1 Pet. 2:1)<br />
Madhara Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />
Hudhoofisha Ubunifu Wa Kipaji<br />
Mwathirika wa mtazamo hasi wa kulalamika na kuhukumu<br />
hukiathiri kipaji chake cha asili kwa kudhoofisha uwezo wake wa<br />
asili wa kubuni mambo mapya. Kumbuka ya kwamba utendaji wa<br />
kipaji unategemea nguvu za ubunifu wa mambo mapya. Na nguvu<br />
za ubunifu hutokana na mawazo chanya.<br />
Kimaumbile “mawazo hasi” hayawezi kutenda kazi kwa<br />
wakati mmoja na “mawazo chanya”. Kila kimoja kinafanya kazi<br />
kwa wakati wake kinapokuwa kimepewa nafasi ya kwanza. Kwa<br />
hiyo, “mawazo hasi” huamsha “hisia hasi” ambazo huwa kikwazo<br />
cha utendaji wa mawazo chanya. Wakati mwathirika wa mtazamo<br />
hasi hutumia mawazo hasi na kughubikwa na hisia hasi; hali hiyo<br />
huzuia upande wa pili wa mawazo chanya na hisia chanya kufanya<br />
kazi kwa wakati mmoja.<br />
Changamoto iliyopo hapa ni kwamba, muda wote ambapo<br />
mawazo hasi, na hisia hasi vinatenda kazi ndani ya mwathirika,<br />
kipaji chake kinakuwa kimefungiwa ule uwezo wake wa kutenda<br />
kazi yenye tija kwa muhusika. Kwa hiyo, muda mwingi unaopotea<br />
kwenye kulalamika na kuhukumu wengine, mambo yake<br />
mwenyewe husimama au kukwama.<br />
61