14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

sasa kinaweza kuona kwamba kuwekeza katika “elimu na ujuzi”<br />

ni gharama kubwa, na kutafuta unafuu na urahisi ili kukwepa<br />

kugharimia viwango bora vya elimu na ujuzi. Kumbe katika<br />

kushusha “viwango vya ubora” tayari tumechagua kurithisha<br />

“viwango duni vya elimu” kwa kizazi kinachoinukia ambacho<br />

hakitaweza kumudu ushindani wa kimataifa katika uzalishaji.<br />

Sio siri hivi sasa kuona kwamba watoto na vijana wetu<br />

wamesongwa katika mazingira magumu ya kimfumo wa huduma<br />

za elimu kwa sababu mbali mbali. Baadhi ya sababu za watoto na<br />

vijana wetu kukosa kupata elimu bora ni pamoja na: i) uhaba wa<br />

nafasi za kuendelea na elimu ya juu katika mfumo wa elimu yetu.<br />

ii) udhaifu wa mitaala isiyokidhi viwango vya ubora wa elimu ya<br />

kimataifa. iii) Vitendo vya uchakachuaji wa mitihani kunakotokana<br />

na kukithiri kwa rushwa katika taasisi zinazosimamia mitihani. iv)<br />

Walimu kukosa motisha katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi.<br />

Kwa kadiri ambavyo idadi kubwa ya watoto na vijana<br />

wengine wanavyoishia katika viwango vya chini vya elimu;<br />

hiyo ndiyo dalili iliyo waziwazi kwamba kizazi chetu tuliopo hivi<br />

sasa tumeamua kurithisha ujinga kwa kizazi kijacho. Kimsingi,<br />

tumekuwa tukifanya zoezi la kurithisha ujinga na kizazi kinachokuja<br />

kitatukumbuka kwa urithi wa ujinga tuliokiachia.<br />

Mabadiliko yoyote ya kimfumo hayaji kwa miujiza. Yanakuja<br />

kwa utashi na uamuzi wa nguvu. Lazima tuutumie utashi wetu<br />

na kufanya uamuzi wa kukataa kuendelea kurithisha ujinga kwa<br />

watoto na vijana wetu. Uwezo na nguvu tunazo, kinachokosekana<br />

ni nia ya dhati. Lazima tukatae kurithisha ujinga kwa watoto na<br />

vijana wetu.<br />

Umaskini<br />

Kuna mtu mmoja maarufu sana anayeongoza kwa utajiri<br />

hapa duniani anaitwa Bill Gates. Miaka ya hivi karibuni alitoa kauli<br />

ambayo imezua mjadala mpaka hivi sasa, lakini ina ushawishi<br />

92

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!