You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
alicho nacho atanyang’anywa.” (Mat. 25:24-29)<br />
Katika maandiko haya tunasoma maneno haya “… Wewe<br />
mtumwa mbaya na mlegevu.” Unaona? Anatajwa moja kwa<br />
moja ya kuwa kilichomfanya akashindwa kutumia kipaji chake ni<br />
ulegevu wake mwenyewe na madhara yake ni kunyang’anywa<br />
hata hicho alichokuwa nacho.<br />
Tabia Sugu Ya Ulevi Na Madawa Ya Kulevya<br />
Miaka 3,000 iliyopita kabla ya elimu ya sayansi kuwepo,<br />
manabii walitoa maonyo kuhusu matumizi ya pombe wakisema<br />
athari zake ni pamoja na kuharibu fahamu za wanadamu:<br />
“Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”<br />
(Hos. 4:11)<br />
Maandiko haya yanathibitisha kwamba pombe ina athari<br />
kubwa kwa kipaji cha binadamu kwa kuwa inadhoofisha uwezo<br />
wa kufikiri. Kwa mantiki hii divai mpya inajumuisha kila kitu<br />
kinacholewesha ikiwemo uvutaji wa bangi; matumizi ya dawa za<br />
kulevya unaojumuisha unga wa kubugia, kunusa, au uchomaji<br />
sindano.<br />
Maandiko matakatifu, kama jina lake lilivyo, yameandika<br />
waziwazi ya kwamba ndani ya pombe mna sumu inayoharibu<br />
tabia ya mtu na kumwondolea ubinadamu wake na kufanya awe<br />
kama hayawani:<br />
“Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali<br />
mjazwe Roho.” (Efe.5:18)<br />
Neno “ufisadi” katika maandiko haya linamaanisha “uchafu<br />
uliokithiri”. Huu si uchafu wa mwili bali vitendo haramu visivyo vya<br />
kimaadili. Ndiyo maana nimeorodhesha ulevi kuwa ni “tabia sugu”<br />
inayoharibu utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya binadamu.<br />
66