14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

ajitambue na kujiandaa kwa ajili ya kutumikia kipaji chake wakati<br />

atakapohitimu masomo yake.<br />

Hapa ndipo mifumo yetu ya elimu katika nchi za kiafrika<br />

ilipodhoofishwa na wakoloni waliotawala mataifa ya kiafrika. Kwa<br />

ujanja walituandalia mifumo ya elimu kwa nia ya kutufanya vibarua<br />

katika mashamba na miradi yao, na sio kwa ajili ya kuwaandaa<br />

watoto wa kiafrika wagundue na kunoa <strong>vipaji</strong> vyao ili wakihitimu<br />

waweze kujitegemea kupitia <strong>vipaji</strong> vyao vya asili.<br />

Kwa bahati mbaya, mpaka hivi sasa bado mifumo ya “elimu<br />

tegemezi” inaendelea kutumika; na ndiyo chimbuko la “dhana ya<br />

kuajiriwa”. Badala ya mhitimu kuwa na mtazamo wa “kujitegemea”<br />

kwa yeye kubuni kazi zake za ustadi na kutoa huduma za kulipwa<br />

kulingana na thamani ya viwango vya ubora; yeye anataka “nafasi<br />

ya kuajiriwa”.<br />

Naomba ieleweke kwamba si makosa wala si dhambi<br />

kuajiriwa. Mantiki hapa ni kwamba nafasi za ajira katika serikali<br />

na taasisi za umma ambazo ni haki ya kila mhitimu ni chache<br />

kuliko idadi ya wahitimu. Na hata sekta binafsi ina vigezo vyake<br />

vya kuajiri ikiwa ni pamoja na malipo ya chini ili kutengeneza faida<br />

kubwa. Hii ndiyo changamoto ya kutegemea ajira peke yake.<br />

Kama nilivyokwisha kusema tangu awali, kila mtoto<br />

ambaye ni binadamu kamili, mwenye afya njema na akili timamu,<br />

anacho kipaji cha asili ndani yake cha kumwezesha kuishi maisha<br />

ya kujitegemea pindi atakapokuwa mtu mzima.<br />

Lakini basi, katika ngazi hii ya ubunifu, ndipo mtoto<br />

anapotumia uwezo wake wa kufikiri kuelekea aina ya kipaji chake<br />

alichoumbiwa tangu tumboni mwa mama yake.<br />

43

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!