Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
ajitambue na kujiandaa kwa ajili ya kutumikia kipaji chake wakati<br />
atakapohitimu masomo yake.<br />
Hapa ndipo mifumo yetu ya elimu katika nchi za kiafrika<br />
ilipodhoofishwa na wakoloni waliotawala mataifa ya kiafrika. Kwa<br />
ujanja walituandalia mifumo ya elimu kwa nia ya kutufanya vibarua<br />
katika mashamba na miradi yao, na sio kwa ajili ya kuwaandaa<br />
watoto wa kiafrika wagundue na kunoa <strong>vipaji</strong> vyao ili wakihitimu<br />
waweze kujitegemea kupitia <strong>vipaji</strong> vyao vya asili.<br />
Kwa bahati mbaya, mpaka hivi sasa bado mifumo ya “elimu<br />
tegemezi” inaendelea kutumika; na ndiyo chimbuko la “dhana ya<br />
kuajiriwa”. Badala ya mhitimu kuwa na mtazamo wa “kujitegemea”<br />
kwa yeye kubuni kazi zake za ustadi na kutoa huduma za kulipwa<br />
kulingana na thamani ya viwango vya ubora; yeye anataka “nafasi<br />
ya kuajiriwa”.<br />
Naomba ieleweke kwamba si makosa wala si dhambi<br />
kuajiriwa. Mantiki hapa ni kwamba nafasi za ajira katika serikali<br />
na taasisi za umma ambazo ni haki ya kila mhitimu ni chache<br />
kuliko idadi ya wahitimu. Na hata sekta binafsi ina vigezo vyake<br />
vya kuajiri ikiwa ni pamoja na malipo ya chini ili kutengeneza faida<br />
kubwa. Hii ndiyo changamoto ya kutegemea ajira peke yake.<br />
Kama nilivyokwisha kusema tangu awali, kila mtoto<br />
ambaye ni binadamu kamili, mwenye afya njema na akili timamu,<br />
anacho kipaji cha asili ndani yake cha kumwezesha kuishi maisha<br />
ya kujitegemea pindi atakapokuwa mtu mzima.<br />
Lakini basi, katika ngazi hii ya ubunifu, ndipo mtoto<br />
anapotumia uwezo wake wa kufikiri kuelekea aina ya kipaji chake<br />
alichoumbiwa tangu tumboni mwa mama yake.<br />
43