14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kuanzia wakati huo, bwana arusi hutambuliwa kuwa mtu<br />

mzima anayestahili kuendesha maisha mapya ya taasisi ya ndoa<br />

yake, na anatarajiwa kuacha kabisa kuwa tegemezi kwa wazazi<br />

kama alivyokuwa kijana asiye na ndoa.<br />

Kwa baadhi ya makabila au mataifa mengine, nadharia ya<br />

urithishaji, huanza kutekelezwa na wazazi katika hatua ya kuozesha<br />

au kufungisha ndoa za watoto wao. Lakini kwa makabila mengine<br />

hatua ya urithishaji hufanyika wakati baba wa familia amefariki<br />

dunia. Baada ya kuhitimisha msiba wake, ndipo wanafamilia<br />

wakisaidiana na ukoo hutekeleza nadharia ya kurithisha mali za<br />

marehemu kwa mjane na watoto wote pasipo kujali wana ndoa au<br />

hawana ndoa.<br />

Sababu Za Msingi Wa Urithishaji<br />

Ukomo Wa Umri Wa Kuishi<br />

Biblia imetabiri ukomo wa umri wa kuishi ni miaka 70 mpaka<br />

80. Dalili za kizazi kinachomaliza muda wake kimekadiriwa watu<br />

kuanzia miaka 50 na kuendelea. Ukomo wa umri wa kutumikia<br />

serikali na taasisi za umma ni miaka 60.<br />

Kwa hiyo, watu wote wenye umri wa kuanzia miaka 50 na<br />

kuendelea, popote walipo, kwa mambo yoyote wanayofanya,<br />

mojawapo ya mipango muhimu kwetu ni kujiandaa kuachia<br />

majukumu tuliyo nayo na kuyarithisha kwa kizazi kinachoinukia<br />

hivi sasa.<br />

Umri wa kizazi kinachotakiwa kurithishwa ni kuanzia miaka<br />

18 mpaka 49. Kipindi cha kurithisha kinahitaji maandalizi yasiyozidi<br />

miaka 10 kwa watu waliofikisha miaka 50.<br />

Kwa hiyo tunalazimika kurithisha kwa sababu ya ukomo<br />

wa umri wa kuishi ambao hatuna udhibiti nao. Kwa bahati<br />

mbaya baadhi yetu tunaogopa kurithisha mapema kwa hofu<br />

83

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!