14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

SURA YA NNE<br />

Utangulizi<br />

WAJIBU KWA KIZAZI CHA SASA<br />

KURITHISHA KIZAZI KIPYA<br />

Kitabu hiki hakitakuwa na msaada kwa msomaji kama<br />

hakutakuwepo na uchambuzi makini unaohusu wajibu kwa kizazi<br />

cha sasa, kizazi cha wazee, kutambua wajibu mkuu wa kurithisha<br />

majukumu ya kijamii, kiuchumi na kiuongozi kwa kizazi kipya.<br />

Kizazi kilichopo hivi sasa kimefikia mahali kilipo hivi sasa<br />

kwa sababu kizazi cha zamani, kilichotangulia kiliacha misingi<br />

ambayo kiliirithisha kwa kizazi kinachomaliza muda wake sasa.<br />

Kwa bahati mbaya, nadharia ya uritishaji imeanza<br />

kupoteza umuhimu wake kwa jamii kiasi kwamba kizazi kipya<br />

hakina matumaini wala mwelekeo wa kule kinakojiandaa<br />

kuelekea. Muktadha wa kitabu hiki ni kukihimiza kizazi cha sasa<br />

kinachomaliza muda wake kutimiza wajibu wake wa kurithisha<br />

kizazi kipya majukumu ya msingi kwa mustakabari wa taifa.<br />

Makundi muhimu yenye wajibu wa kusimamia mchakato<br />

wa urithishaji kwa kizazi kipya unaanzia na “wazazi” au “walezi”<br />

katika ngazi ya familia. Ngazi ya familia ndio kitovu cha malezi<br />

kuanzia mtoto anapozaliwa, kukua hadi anapofikia umri wa<br />

kujitegemea kama mtu mzima.<br />

Kundi la pili ambalo linahusika katika wajibu wa kurithisha<br />

kizazi kipya ni kanisa. Natumia msamiati kanisa kwa maana ya<br />

taasisi inayosimamia kueneza na kurithisha maadili ya kiimani<br />

kwa wafuasi wake. Wakati familia ni mlezi mkuu wa maisha ya<br />

81

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!