Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
• Zinaa huharibu akili na uwezo wa kufikiri mambo ya maana<br />
• Zinaa husababisha umaskini kwa matumizi ya anasa zisizo na<br />
udhibiti<br />
• Zinaa husababisha uhasama/chuki/uadui mpaka mauaji<br />
• Zinaa husababisha migogoro na kusambaratisha familia<br />
• Zinaa hueneza maambukizo ya maradhi ya zinaa na VVU<br />
Tabia Sugu Ya Chuki Na Hasira<br />
Tabia ya chuki na hasira imetokea kuwa miongoni mwa<br />
tabia sugu ambazo zinaathiri <strong>vipaji</strong> vya asili kwa sababu waathirika<br />
wengi ni vijana, tena ambao ndio nguvu kazi ya taifa. Kimaumbile<br />
kila binadamu ana “hisia hasi” za chuki na hasira. Lakini hisia<br />
hizi zinatakiwa kudhibitiwa ili kudumisha mahusiano mema ya<br />
kifamilia na kijamii. Pale ambapo mtu anashindwa kudhibiti chuki<br />
na hasira matokeo yake atajikuta amesababisha madhara yenye<br />
kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili, kwa yeye mwenyewe na kwa<br />
jamii inayomzunguka pia.<br />
Tafsiri Ya Misamiati Ya Chuki Na Hasira.<br />
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu, neno “chuki”<br />
limetafsiriwa kuwa ni: “ tabia ya kutopenda watu au hali ya kuwa<br />
na roho mbaya, au kinyongo.” Neno hasira limetafsiriwa kuwa ni:<br />
“ ghadhabu au hamaki au fundo.”<br />
Hapa nitoe angalizo ya kwamba, hii “tabia sugu ya chuki<br />
na hasira”, inatofautiana na ile “tabia sugu ya kulalamika na<br />
kuhukumu” ambayo tayari tumejifunza habari zake. Mtu mmoja<br />
anaweza kuwa na tabia sugu zote mbili, lakini sio lazima aliye na<br />
tabia moja kati ya hizi awe na tabia ya pili.<br />
Kuna watu wameathiriwa na “tabia sugu ya chuki na hasira”<br />
lakini hawana hulka ya “tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu”<br />
wengine hadharani. Waathirika wa “chuki na hasira” wanaweza<br />
kuchukua hatua kali za kulipa visasi pasipo kupiga kelele hata<br />
kidogo.<br />
72