Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kujifunza kwa akili ili kupata ujuzi wa maisha ya kila siku.<br />
• Jumbe Za Vitisho Na Udhalilishaji (Cyberbullying)<br />
• Shirika moja lijulikanalo kama Enough is Enough, lilifanya utafiti<br />
na kugundua kwamba 95% vijana wanaotumia mitandao ya<br />
kijamii wameshuhudia mawasiliano ya vitisho na udhalilisha na<br />
33% yao ni waathirika wa mawasliano hayo<br />
• Watoto Huathirika Vibaya Zaidi Na Mitandao Ya Kijamii<br />
Wasipodhibitiwa<br />
• Hii ni kwa sababu kwenye mitandao hii zinarushwa picha<br />
mbaya za ugomvi na picha za uchi ambazo huwaathiri<br />
kisaikolojia watoto na vijana. Baadaye husababisha watoto na<br />
vijana kujihusisha na vitendo vya uhalifu na ngono haramu.<br />
• Kichocheo Cha Mkengeuko Wa Maadili Mema<br />
• Maambukizi ya mkengeuko wa maadili ya kimaani na<br />
kiutamaduni kwa sababu ya mwingiliano wa walioharibika<br />
kitabia, waliojaa tamaa ya kupata faida kubwa bila kujali<br />
maadili mema katika nchi husika.<br />
Changamoto Za Ndani<br />
Katika utangulizi wa sehemu hii tumepata tafsiri kuhusu<br />
changamoto za ndani kuwa ni mambo hasi ya ndani yanayomwathiri<br />
kila mtu binafsi kitabia. Katika uchambuzi wa changamoto za<br />
ndani tunakwenda kutumia msamiati mpya ambao unaitwa “tabia<br />
sugu”. Msamiati huu unalenga kuchambua tabia sugu zenye<br />
kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya mhusika.<br />
Tafsiri Ya Misamiati Ya Tabia Sugu<br />
Sasa tumefikia kipengele ambacho hasa ndio kikwazo<br />
sugu chenye kuathiri <strong>vipaji</strong> vya asili katika jamii. Labda nianze na<br />
uchambuzi wa misamiati. Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili<br />
Sanifu, neno “tabia” limetafsiriwa kuwa ni: “mazoea yatokanayo<br />
na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo”<br />
55