07.12.2012 Views

12TH JULY 2002 - ConstitutionNet

12TH JULY 2002 - ConstitutionNet

12TH JULY 2002 - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

watueleze maoni yao juu ya Katiba mpya ambaye itatusaida kujenga Kenya mpya. Tunajua kwamba Kenya inabahati sana<br />

kwa vile watu wa Kenya wametafuta sana Katiba huu mpya kwa miaka zaidi ya kumi. Na si kawaida kwa nchi nyingi ya Africa<br />

kutengeneza Katiba kama hakuna vita. Lakini hapa kwetu tumebahatika kwa maana Serikali pamoja na watu wote wakenya<br />

walikubali Katiba mpya iandikwe wakati huu ambao tuko na President ambaye yuko mamlakani wakati huu na hakuna mzozo<br />

wowote ilio mbaya zaidi katika nchi hii kwa hivyo tuna shukuru Mungu kwa hayo. Na tunatumaini ya kwamba nyinyi ambao<br />

mulifika hapa mutatusaidia na fakira njema ya kutengeneza Katiba mpya. Sisi kama ma-commissioners hatuko na uwezo<br />

wakuandika Katiba bila kupata ithini na maoni kutoka kwenu. Kwa hivyo tunawashukuru na ku wauliza tafadhali mtuletee<br />

mambo yatakayo tu saidia kuandika Katiba mpya. Asanteni sana.<br />

Com. Ayonga : Asante mama Asiyo, sasa itakuwa Bwana Abubakar Zein.<br />

Com. Abubakar : Habari ya asubuhi. Kama alivyo sema mwenyekiti wa kikao hiki, mimi naitwa Abubakar Zein na mimi<br />

ni mmoja kati ya ma-commissioner wa Tume ya kurekebisha Katiba na kwa ada na desturi zetu za kiafrica wazee wakisha<br />

sema mimi ni kukubali na kuafik na kuyapendekeza waliosema. Asanteni.<br />

Com. Ayonga : Asante Bwana Abubakar Zein. Sasa katika kikao cha leo. Ninataka kumuuliza Bwana Abubakar Zein<br />

achukuwe wadhifa wa mwenyekiti. Yeye ndiye atawaambia taratibu ya kuchukua maoni. Sasa mpaka wakati tutakapomaliza<br />

yeye ndiye atakuwa mwenyekiti. Bwana Zein njoo uketi hapa.<br />

Com. Abubakar : Asante sana Pastor Mzee Ayonga. Kama alivyo sema Mzee amenipa kazi ya kufanya na mimi<br />

nitajaribu kuifanya kwa uwezo yangu. Kwanza kabisa ningependa kuwapa maelezo kuhusu kazi ya leo tutaifanya namnagani,<br />

na kwa haraka kabisa nita waambia kwamba, wale ambao wamekuja hawajajiandikisha waende pale kwa lile dawati pale,<br />

kwenye meza ile ndogo alio kaa ule Binti, wajiandikishe pale. Wale watu wanaojiandikisha pale, wanajiandikisha kwamba<br />

wamefika na kuhudhuria kikao hiki. Na kuna watu aina mbili wanaojiandikisha pale. Wale ambao watatoa maoni leo, na wale<br />

ambao wata kaa kusikiliza tu. We are registering both observers as well as those who have submissions to make. Hilo ni la<br />

kwanza.<br />

La pili, tutakuwa tukitumia ile orodha ya majina tukipata kutoka pale, tutakuwa tukitumia hiyo ili kuwaita watu jinsi walivyo<br />

jiandikisha. Aliyejiandikisha number ya kwanza ataitwa apewe fursa ya kwanza. Halafu nikuaambie ya kwamba sisi kawaida<br />

huwa tunajipa haki kama Tume, ikifika wakati kutakuwa kuna sababu za kutosha kutoka katika orodha hii ya majina. Kando<br />

kidogo kama kwa mfano tupate bibi ambaye ni mjamzito tuta jaribu kumpa fursa ya kuzungumza au mtu Mzee sana, au mtu<br />

ambaye ni mlemavu, au mtu mgonjwa, au mtu yeyote ambaye anasababu ya kutosha kupewa fursa ya kuzungumza mbele, hata<br />

kiongozi wetu yeyote hapa akitokea tutampa fursa azungumze halafu tutarudi kwenye orodha. Au si sawa hivyo? Ikiwa<br />

siwasikii na pengine munaona si sawa. Ni sawa hivyo? Sawa.<br />

5

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!