28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Moja ni COPEC ambayo hivi karibuni imepewa leseni ya kuanza kuagiza mafuta, lakini<br />

ilianzishwa miaka zaidi ya 11 iliyopita. Lakini hapo hapo tulianzisha Kampuni nyingine COPEC ishiriki<br />

katika usambazaji wa mafuta. Lakini tulianzisha pia Kampuni nyingine ishiriki katika usimamizi wa<br />

mfumo wa usambazaji wa gesi, Kampuni inaitwa GASCO na nyingine inaitwa KILAMCO isaidie<br />

kwenye gesi na uzalishaji wa mbolea. Kampuni hizo zote tatu zilizoanzishwa lakini hazikupewa fursa<br />

ya kufanya kazi. Je, baada ya kizaazaa ambacho tumepata hivi karibuni cha kudhalilisha Taifa hili<br />

kwa Makampuni yaliyokuwa na hisa…<br />

SPIKA: Tunaomba usituhubirie. Mheshimiwa Mntangi hiyo ni hotuba sasa. Naomba uulize<br />

maswali.<br />

MHE. HERBERT J. MNTANGI: Mheshimiwa Spika, tunasema nini sasa kuhusu kuirejesha<br />

Kampuni ya gesi ya GASCO ili iweze kusimamia usambazaji huo wa gesi<br />

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na tatizo lenyewe, lakini tunajibu kifupi.<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema tatizo kubwa<br />

ni matumizi ya gesi yenyewe. Magari yenyewe ni 36 kituo kinaweza kukidhi magari 200 na hii<br />

ilikuwa ni pilot study kwa maana ya kwamba kwa magari zaidi ya 10,000 yaliyopo Dar es Salaam,<br />

magari yenyewe 200 ni kweli hata ukiwa pale pale Dar es Salaam gari yako iko Mbagala,<br />

inaonyesha kwamba tanki imepungua mafuta uende mpaka Ubun<strong>go</strong> ndio urudi tena mjini, ni<br />

tatizo.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nadhani kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kazi kubwa<br />

ni kuongeza kwanza ufahamu, lakini pia upatikanaji wa CNG yenyewe. Sasa tumekusudia<br />

kwamba mkakati wa kwanza ni kwamba ile CNG na LPG haipatikani kutokana na gesi yetu<br />

wenyewe. Kwa hiyo, mkakati wa kwanza ni kutoa LPG instruction kwa ile gesi ya kwetu wenyewe,<br />

hii inayozalishwa hapa, halafu tuboreshe matumizi ya gesi kwa mfano ziko nchi India, China na<br />

kadhalika ambako kwenye Halmashauri za Miji magari ya mabasi na kadhalika hayaruhusiwi<br />

kutumia petroli kwa sababu ya environmental resources. Kwa hiyo, nasi tufike sehemu ambayo<br />

mabasi, daladala, teksi na yale magari ambayo yanakwenda kwa mwendo wa kati kwa safari<br />

fupi fupi mijini itumie gesi asilia na hapa tutapata matumizi ku-justify vituo viongezeke na kadhalika.<br />

Mheshimiwa Spika, la pili la COPEC nimekubaliana naye. Kwa hiyo, ndiyo maana Serikali<br />

imeirejesha COPEC ili isimamie zoezi la mafuta. Hili la GASCO nadhani ni kweli tunahitaji Kampuni<br />

ya kusambaza gesi, lakini litaendana na upatikanaji na kukua kwa matumizi ya hiyo gesi yenyewe<br />

katika jamii ya Watanzania.<br />

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nimwulize<br />

Mheshimiwa Waziri, kwa sababu sasa tumeambiwa kwamba kuna bei elekezi ya mafuta. Naomba<br />

utufahamishe Bunge hili bei ya petroli, mafuta ya taa na dizeli ni shilingi ngapi<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, nimemwelewa Mheshimiwa<br />

Ndassa, alikuwa anauliza kwamba bei ya mafuta. Sijaelewa vizuri swali lake.<br />

SPIKA: Mheshimiwa Ndassa, swali lako uliza tena kwa taratibu.<br />

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Waziri naomba nikuulize swali, kwa sababu sasa<br />

tunaambiwa kuna bei elekezi ya mafuta, bei mpya, dizeli ni shilingi ngapi Mafuta ya taa shilingi<br />

ngapi Na petroli ni shilingi ngapi ili Watanzania wote wajue<br />

SPIKA: Bei elekezi ya products hizo.<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, nafahamu kwamba kuna bei<br />

elekezi imetoka jana ambayo imezingatia viwan<strong>go</strong> vilivyonunuliwa mafuta kwa maana ya<br />

purchasing price iliyokuja kwa haya mafuta yaliyopo nchini sasa hivi.<br />

Mheshimiwa Spika, sijajua bado na siwezi kumhakikishia kwa sasa hivi kwamba bei exactly<br />

11

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!