28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

nafuatilia vizuri Rutoro Muleba kwa ndugu yangu Charles Mwijage na Misenyi kwa ndugu yangu<br />

Assumpter Mshama, ni hivyohivyo kuna mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo ya ardhi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, inafikia mahali nchi hii tunawapa wawekezaji maeneo ambayo<br />

baadaye wananchi wanageuka kuwa watumwa kwenye nchi yao! Hayo maeneo niliyotaja hayo<br />

ni maeneo yaliyoko mpakani, matokeo yake Ranchi zile zimebinafsishwa kwa watu ambao siyo<br />

Watanzania na sasa uwezo wa kufuga mifu<strong>go</strong> wao hawana, kinachofanyika ni kukodishia watu<br />

kutoka Uganda, watu kutoka nje ya nchi. Hili liliniuma sana niliposikia, kwa kweli sasa kama<br />

tumefikia hapo Watanzania tumefikia pabaya. Tuna wafugaji wetu nchi hii, hivi haya maeneo ya<br />

NARCO kwa nini tusiwape wafugaji wetu wanaohangaika Tunafika mahali tunaanza kukodisha<br />

maeneo ya NARCO yaliyopimwa! Kwa nini Serikali isipime maeneo mengi ya namna hiyo Kama<br />

kuna masharti basi wapewe wafugaji kuliko kubinafsisha kwa watu wengine. Tatizo hili ninalo<br />

Mbarali na nadhani na wenzangu mtakuwa na maeneo yenye matatizo kama niliyoyataja.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna NARCO Mbarali, ndugu zangu wananchi wa Kata ya Ruiwa<br />

na Mwatenga wamenituma Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na<br />

naomba Serikali isikie, pamoja na wananchi waliohamishwa Msangaji, watu hawa wamepelekwa<br />

mahali ambapo kuna ukame, hakuna malisho, hakuna nini, lile eneo la NARCO ambalo ni zuri kwa<br />

kufuga na kilimo ambalo sasa wanakodishwa wananchi, wale waliochukua, uwezo wa kufuga<br />

hawana, sasa wanawakodisha wananchi. Naomba Mheshimiwa Waziri baada ya kikao hiki, ili<br />

uone mimi ni mwon<strong>go</strong>, ukashuhudie kule jinsi ambavyo ardhi ile watu wanakodishiwa. Watu wale<br />

walitoa ardhi ile kwa nia nzuri kwa Serikali kuwa inataka kuleta ufugaji wa kisasa, sasa Serikali<br />

imeshindwa, kwa nini isiwape wale wananchi ikawapa na masharti yaleyale ambayo wamepewa<br />

wawekezaji (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa wito kwa Serikali Ranchi zote za Taifa wapewe wananchi<br />

wetu wafugaji. Kama kuna masharti wamepewa wawekezaji, tuwape wafugaji wetu badala ya<br />

kuacha leo hii wanahangaika na hawana pa kwenda. Hili naomba Mheshimiwa Waziri, tukimaliza<br />

hapa aje Mbarali.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka vilevile nikuambie mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi iliyoko Mbarali,<br />

eneo la I<strong>go</strong>melo pale Igawa njiani, namshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa uzalendo wake na<br />

moyo wake wa busara. Eneo lile Serikali imewekeza pale, watu wanalima kiangazi na muda wote<br />

panalimwa pale. Wachina walijenga pale, lakini katika hali ambayo ni ya kushangaza sana mtu<br />

mmoja akafika akasema hii yote ni Game Reserve. Waziri Mkuu alipokuja pale wananchi<br />

wakamwambia, “Angalia Mheshimiwa Waziri Mkuu, eneo lote tumeambiwa sasa ni Game<br />

Reserve”. Mheshimiwa Waziri Mkuu aliwaambia kwamba “Hata kama mimi ningekuwa<br />

mwendawazimu nisingekubali”. Eneo lile limebaki kwa kauli ya Waziri Mkuu. Naomba na<br />

kwenyewe Waziri afike akawatamkie ardhi yao ile, wanataka kuwa na uhakika kwamba<br />

inachukuliwa au wanabaki nayo. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemualika aje nimpeleke NARCO akakae na wananchi wa<br />

Ruiwa na Mwatenga na wananchi waliohamishwa kutoka Msangaji ambao sasa wanahangaika<br />

hawana mahali pa kuishi, tabu tupu! Aje aone ninayoyasema kama ni ya uwon<strong>go</strong> au ya ukweli.<br />

Mheshimiwa Waziri, siwezi kukulaumu sana, utendaji wako ninaufahamu kwa muda mfupi,<br />

Wizara hii wewe ni mpya lakini naomba tukuambie ili tukusaidie.<br />

MWENYEKITI: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>, unapojadili mjadala wako elekeza kwenye Kiti, kwa<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti siyo unampa Mheshimiwa Waziri moja kwa moja.<br />

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la ardhi katika Wilaya ya Mbarali,<br />

nimeshukuru kuwa tayari limeshaonesha njia ya kulipatia ufumbuzi lakini nikianzia Madibira<br />

Kiton<strong>go</strong>ji cha Mlonga, maeneo ya Kinyasuguni, maeneo ya Silyamboga ni maeneo ambayo ni<br />

muhimu sana kwa wakulima wado<strong>go</strong>wado<strong>go</strong>, nikiacha lile shamba la awamu ya pili ambalo<br />

linatakiwa kuridhiwa tena ili kusudi wananchi wapate sehemu ya kilimo. Eneo hili wale wakulima<br />

ambao wameshindwa kupata nafasi kwenye yale mashamba yaliyoboreshwa ndiko wanakolima,<br />

lakini vilevile tukumbuke watu wale wanaongezeka na TANAPA ikiishachukua eneo huwezi ukaja<br />

67

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!