28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Leo amekuja Mheshimiwa Waziri humu ndani hata hii taarifa sidhani kama anayo,<br />

watendaji wake wamwambie, wanamwingiza mkenge mjini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, eeh! Kwa hiyo kama kuna maagizo ya Rais msichambue<br />

mkanyofoa maagizo ya Rais, mkaacha maagizo mengine, hili nalo ni agizo la Rais wasaidieni<br />

hawa watu waliokaa zaidi ya miaka 40 kwenye nyumba hizi. Kigeugeu kiko wapi Nyumba za Ilala,<br />

Amana, Buguruni, Tandika, Ubun<strong>go</strong>, hizi nyumba haziwasaidii chochote. Let the people live and<br />

the state will live.ndiyo eeh! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mchechu aendelee kujenga maghorofa mjini ili watu wakae<br />

katika nyumba safi na salama, hilo nawapongeza sana National Housing, lakini mjenge affordable<br />

houses, mjenge nyumba ambazo mtu wa kawaida ataweza na yeye kumudu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo umetutangazia hapa kuna nyumba, hizo nyumba zitakuwa<br />

milioni 100, hivi wale watu hatuzungumzii Dar es Salaam, Mtanzania gani wa sasa hivi ataweza<br />

kununua nyumba ya milioni 100 Jengeni nyumba ndo<strong>go</strong>, nyumba za kawaida ambazo watu wa<br />

kawaida na wao waone raha kuishi katika makazi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ya nyumba ambazo tunazo mjini, naomba radhi hata<br />

ile raha na tendo na heshima ya ndoa hakuna, hakuna. Mtu anakaa chumba kimoja na mkewe<br />

na watoto watatu, hajui cha kufanya, asubuhi akitaka shughuli zingine watoto wameshaamka<br />

kwenda shule. Jengeni nyumba ambazo zitawafanya watu wawe na heshima za ndoa zao<br />

kwenye nyumba zao nchini mwao kwa gharama ndo<strong>go</strong> na kwa mkopo wa miaka 20.<br />

(Kicheko/Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei za viwanja, kiwanja cha rahisi Ilala milioni nne na laki tano.<br />

Hivi squatters wataacha kuwepo Dar es Salaam kama viwanja bei zake ni hizi Lazima viwanja<br />

viwe bei ya chini na maeneo maalum ya kuwasaidia watu wa kipato cha chini, kununua viwanja<br />

hivyo kwa gharama ndo<strong>go</strong> na hakuna mtu yeyote mwenye uwezo mkubwa kisheria, anaruhusiwa<br />

kuingia kununua viwanja hivyo na yule ndiyo anaruhusiwa kuuza. Lakini leo vikija viwanja vya bei<br />

ndo<strong>go</strong> anataka huko huko, ana viwanja 20 huku, 20 huku, 30 huku. Hii ni roho mbaya, ubinafsi na<br />

ni dhambi kubwa sana tunayowafanyia watu wetu na watu wakome kujilimbikizia ardhi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeanzishwa mpan<strong>go</strong> mzuri wa benki ya ardhi, land bank, very<br />

nice. Huwezi ukawa na benki ya ardhi bila kuwa na Land Ceiling Act, lazima Mheshimiwa Waziri<br />

alete sheria ya kuzuia watu kujichukulia ardhi nyingi bila sababu. Land Ceiling Act, lazima<br />

Mheshimiwa Waziri ailete ili kuhakikisha kwa Watanzania, hii nchi ni yetu wote. Haiwezekani<br />

baadhi ya watu wakawa na maheka mamilioni, wengine hata heka mbili au heka moja hawana.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia suala lingine la nini Leo asubuhi kuna mtu<br />

alisimama akawa anazungumza anasema nyumba za National Housing uzeni kwa bei ya soko,<br />

mimi imenisikitisha sana. Sisi Dar es Salaam hatuna pamba, korosho wala mifu<strong>go</strong>. Sisi Dar es Salaam<br />

siasa ni nyumba. Sasa unaposimama mtu unatetea pamba unaacha kutetea nyumba kwa<br />

sababu mnazo pamba, sisi hatuna hela za pamba, tunataka wale wapangaji wauziwe nyumba<br />

kwa bei rahisi na nyumba mpya zinazojengwa, zijengwe kwa bei rahisi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia suala la Kigamboni. Serikali mpaka sasa hivi<br />

haijaonesha dalili zozote zaidi ya kubana, lini mtaachia (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine. Nalisema hili kwa watu wote wanaohusika na Wizara<br />

yote husika walielewe. Mpan<strong>go</strong> huu wa Kurasini wa kupanua Bandari, ebu Vion<strong>go</strong>zi wa Serikali<br />

rudini mkalitazame upya na mpime haya ninayoyasema.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mpan<strong>go</strong> wa nchi jirani, wameshaingia mkataba na nchi za<br />

Asia kuboresha Bandari yao na Bandari hii ikishaboreshwa unafanywa mpan<strong>go</strong> unaitwa<br />

Transhipment Port. Bandari hii itazuia meli kuja Dar es Salaam, itakuwa sasa meli zote zinakwenda<br />

89

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!