Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
maeneo husika na kutoa amri husika, zinashindwa kutekelezeka na ndiyo maana tunapata hii<br />
mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya watu. Utasikia eneo fulani wame<strong>go</strong>ma, sijui imekuwaje, lakini suala hili lingewekwa<br />
wazi nafikiri lingeweza kuwasaidia wananchi wakaishi vizuri na kila mmoja akatimiza wajibu wake<br />
na kutii sheria.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuomba Wizara husika iangalie suala hili kwa<br />
sababu sekta ya ardhi ni mtambuka, ijaribu kushirikiana na Wizara nyingine zilizopo, wafanye kazi<br />
kwa pamoja, wawaondolee wananchi wetu hawa matatizo haya ya kila siku. Iwapo haya<br />
niliyoyasema yatafanyiwa kazi, ninaamini haya yanayotokea huko kote ambayo tunayasikia hapa<br />
Bungeni, hayatakaa yajitokeze kwa sababu kila mmoja atajua eneo lake likoje, atajua thamani ya<br />
shamba lake ikoje na hata akienda kuuza atajua auze kwa shilingi ngapi.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)<br />
MWENYEKITI: Nakushukuru sana Mheshimiwa Antony Mbassa, na kwa kweli sauti yako<br />
ulivyokuwa unatoa message ya kuchangia, ni kama mtumishi wa Mungu kabisa. Nakushukuru<br />
sana.<br />
MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Mbarali,<br />
naomba nichukue nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vilevile nichukue nafasi hii kuishukuru sana Serikali kwa<br />
kuwa sikivu kwa kilio cha wananchi wa Mbarali, hasa kupitia Waziri Mkuu alipotangaza kwamba<br />
wale wananchi hawatasumbuliwa tena na uhamisho ambao kwa kweli ilikuwa ni kero kubwa kwa<br />
wananchi wa Mbarali na mimi mwenyewe. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba nichukue nafasi hii kuishukuru Kamati ya Bunge<br />
ya Maliasili, Ardhi na Mazingira, kwa kuona umuhimu wa kutatua mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hii ya ardhi katika nchi<br />
hii wakiwa wameanzia kwangu Mbarali. Walikuwa ni mchan<strong>go</strong> mkubwa sana wa kuona kwamba<br />
wananchi wanabaki na ardhi yao na si vinginevyo.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vilevile nimshukuru sana Waziri wa Maliasili na Utalii,<br />
Mheshimiwa Ezekiel Maige kwa kuungana na Kamati pamoja na Serikali, kuona kwamba wale<br />
wananchi wa Mbarali ardhi yao isingefaa kuchukuliwa.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa nimekosea sana kama sitashukuru uon<strong>go</strong>zi wa TANAPA<br />
kwa kukubali kwamba ni kweli TANAPA haiko kwa ajili ya kuwa na mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro na wananchi, inataka<br />
mahusiano ya karibu na wananchi na hivyo iko tayari kufanya mahusiano ya karibu na wananchi<br />
wa Mbarali na siyo ku<strong>go</strong>mbana kwa kung’ang’ania mipaka. Hivyo na wenyewe naomba<br />
niwashukuru sana.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema nawashukuru hao kwa sababu inawezekana wananchi<br />
wa Mbarali wakashangaa imekuwaje leo nawashukuru! Kwa kweli katika kikao cha pamoja<br />
tulichofanya tarehe 28 na 29 na hao wote niliowataja, tulifikia hatua hiyo nzuri ya maridhiano.<br />
Tatizo kubwa lilikuwa ni ramani iliyoridhiwa na RCC ambayo haikuwa imeandaliwa awali na<br />
TANAPA, kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ile ramani ya<br />
mwanzo haikuwa na m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro kwa wananchi wa Mbarali, sasa ilipoongezwa hii ya RCC ambayo<br />
ililetwa kinyume na taratibu, ilileta m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro mkubwa, wananchi wa Mbarali wakakosa imani na<br />
Serikali yao lakini baada ya kukaa tumekubaliana kwamba, ramani ya mwanzo ndiyo<br />
itakayofuatwa na siyo ile iliyoongezwa na RCC. Naishukuru sana Serikali kwa kuwa sikivu.<br />
Wananchi wa Mbarali wana imani kubwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi lakini vilevile na<br />
uon<strong>go</strong>zi wa ngazi ya Taifa kwa maana ya Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda sasa baada ya kuongea hayo, niongelee mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya<br />
ardhi Wilayani Mbarali na maeneo mengine yaliyopo katika nchi hii. Mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi katika nchi<br />
hii tusipoiangalia, itatupeleka pabaya! Ni kweli kwangu Mbarali kuna mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro lakini vilevile kama<br />
66