28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Sayansi ya Tiba ya Afya (MUHAS) Mloganzila. Wakati wa kuhitimishwa kwa Bajeti ya Waziri Mkuu<br />

katika mkutano huu wa Bunge, Serikali ilieleza kwamba tathmini ya fidia inaendelea na kwamba<br />

wapo wananchi ambao tayari wamelipwa fidia na wengine bado hawajalipwa mpaka sasa.<br />

Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali kuzingatia kwamba fidia iliyolipwa kwa wananchi wachache ni<br />

ya mali na mazao; hata hivyo wananchi hawajalipwa fidia ya ardhi. Ofisi ya Waziri Mkuu ilitoa<br />

maelekezo kwa Wizara zinazohusika kuhakikisha fidia stahiki inalipwa. Mwaka 2010 Wizara ya Ardhi<br />

na Maendeleo ya Makazi ilifanya mkutano na wananchi na kuwaahidi kulipa fidia ya ardhi kwa<br />

mujibu wa sheria, Kambi ya Upinzani inataka Serikali ieleze malipo hayo yatatoka kwenye fungu lipi<br />

na yatalipwa lini (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, malalamiko dhidi ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA),<br />

mwaka 2004, Serikali kupitia wakala wa majen<strong>go</strong> mkoani Dodoma, waliwauzia wananchi<br />

nyumba zilizokuwa zinamilikiwa na lililokuwa Shirika la Reli Tanzania (TRC). Malalamiko makubwa<br />

kutoka kwa wananchi hawa wa Tambukareli ni kunyimwa hati za nyumba zao na CDA ilhali<br />

wameshalipia nyumba hizo kwa ukamilifu. Sababu zinazotolewa na CDA, zisizo na mashiko ni<br />

kwamba eti Serikali ilitoa uamuzi wa kuuza nyumba bila kuwahusisha CDA, hivyo hawatambui<br />

uuzwaji wa nyumba hizo! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali kutoa maelekezo kwa CDA kutoa<br />

hati husika, ni suala la kiburi na jeuri kwa taasisi ya Serikali kuhoji maamuzi ya Serikali au leo<br />

tuelezwe kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano inafanya kazi chini ya CDA Kama kulikuwa<br />

na uzembe ndani ya Serikali, kwa nini wananchi hawa maskini waliodunduliza vihela vyao wapate<br />

makazi waumizwe Kambi ya Upinzani inataka kauli thabiti ya Serikali kuhusiana na hili! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu Sheria Na. 5 ya Ardhi ya Vijiji na mustakabali wa Taifa, Sheria ya<br />

Ardhi ya Kijiji inatoa mamlaka kwa Halmashauri ya kijiji kusimamia ardhi yote ya kijiji. Halikadhalika<br />

Halmashauri ya kijiji imepewa mamlaka ya kugawa ardhi baada ya kuruhusiwa na Mkutano Mkuu<br />

wa Kijiji. Uzoefu umeonyesha kwamba kutokana na kutokuwa na ufahamu mpana wa sheria, watu<br />

wenye fedha wamekuwa wakitumia fursa hii ya kisheria vibaya kwa kuwarubuni vion<strong>go</strong>zi wa vijiji<br />

na hatimaye kugawa maeneo ya kijiji kwa wageni wenye fedha wachache, huku ikiwaacha<br />

wanakijiji bila ardhi yoyote. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, hali inakuwa mbaya zaidi pale ambapo watu ambao sio Watanzania<br />

wanatumia upenyo huu wa kisheria na kumilikishwa maeneo makubwa ya kijiji kinyemela! Kambi<br />

ya Upinzani imepata malalamiko kutoka kwa wanakijiji wa kijiji cha Orngadida, Kata ya Qash,<br />

Babati (taarifa ambayo Waziri wa Ardhi, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mkuu wa Wilaya na<br />

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wanayo). Wanakijiji hao wanawatuhumu vion<strong>go</strong>zi wa<br />

Serikali ya Kijiji wakishirikiana na Diwani kuuza ardhi kwa wageni pasipo kuwashirikisha, wanakijiji<br />

wamemwandikia Mkuu wa Wilaya ya Babati barua mbili ambazo nazo hazijajibiwa!<br />

Mheshimiwa Spika, hakuna ubishi kwamba kuna wageni wengi waliopata maeneo ya vijiji<br />

kinyemela kwa kutumia upenyo huo wakati Sheria ya Ardhi Na. 4 , kifungu cha 20 kinakataza<br />

wageni kumiliki ardhi nchini isipokuwa kwa malen<strong>go</strong> ya uwekezaji tu na ambao umiliki wake lazima<br />

upitie Kituo cha Uwekezaji Tanzania na si vinginevyo.<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali iliambie Bunge lako Tukufu, ni lini<br />

imefanya tathmini katika vijiji vyetu ili kuweza kubainisha ardhi zilizotolewa na Halmashauri za Kijiji<br />

na uhalali wake. Ni maoni ya Kambi ya Upinzani kwamba sheria hii isipoangaliwa kwa umakini<br />

itasababisha umwagaji damu mkubwa hasa pale wananchi watakapohisi kunyang’anywa ardhi<br />

yao kifisadi au vinginevyo na mbaya zaidi zoezi hili linafanywa hata mijini na Serikali za Mitaa<br />

ambazo hazina mamlaka ya kugawa ardhi. Mchezo ambao wanafanya kwa kushirikiana na<br />

watendaji wa manispaa na baadhi ya Maafisa wa Wizara! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu uvamizi wa maeneo ya wazi mkoa wa Dar es Salaam, kutokana<br />

na malalamiko ya wananchi mbalimbali kuhusu uvamizi wa maeneo ya wazi ya umma katika<br />

mkoa wa Dar es Salaam, Serikali iliunda Kamati ya kufanya uchunguzi kuhusu uvamizi katika<br />

maeneo husika. Kamati ilikamilisha kazi yake tarehe 13 Julai, 2010.<br />

51

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!