28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2010/2011 Wizara iliidhinishiwa jumla ya Sh.<br />

53,362,742,663/=. Kati ya fedha hizo Sh. 7,573,264,663/=, sawa na asilimia 14 ya fedha<br />

zilizoidhinishwa, zilitengwa kwa ajili ya mishahara, Sh. 25,159,688,000/=, sawa na asilimia 47,<br />

zilitengwa kwa ajili ya matumizi mengineyo na Sh. 20,629,790,000/=, sawa na asilimia 39, zilitengwa<br />

kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Hadi Juni, 2011 jumla ya fedha zilizopatikana ni Sh.<br />

31,769,391,298/=, sawa na asilimia 60 ya fedha zilizoidhinishwa. Kati ya fedha hizo zilizopatikana,<br />

Sh.7,573,264,663/= zilitumika kwa ajili ya mishahara, Sh. 18,322,743,635/=, kwa ajili ya matumizi<br />

mengineyo, na Sh. 5,873,383,000/= kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Fedha za Maendeleo<br />

zilizopatikana zilikuwa sawa na asilimia 28 tu ya bajeti ya miradi ya maendeleo. Hadi Juni, 2011<br />

kiasi kilichotumika ni Sh. 31,423,143,942/= sawa na asilimia 99 ya fedha zilizopatikana.<br />

Mheshimiwa Spika, ardhi ni mhimili na raslimali muhimu katika kukuza uchumi wa nchi. Kwa<br />

kuzingatia umuhimu wake, Wizara yangu inaendelea kutoa huduma za utawala na usimamizi wa<br />

ardhi kwa len<strong>go</strong> la kuimarisha usalama au uhakika wa milki. Huduma zinazotolewa ni pamoja na<br />

utoaji wa hatimiliki za ardhi, utatuzi wa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi, utwaaji ardhi kwa manufaa ya umma<br />

na ubatilishaji milki za wanaokiuka masharti ya milki zao. Vilevile, Wizara inatoa elimu na mion<strong>go</strong>zo<br />

juu ya sera na Sheria za Ardhi, na inahamasisha uanzishwaji wa Masjala za Ardhi za Wilaya na Vijiji<br />

kwa len<strong>go</strong> la kufanikisha utoaji wa Vyeti vya Ardhi ya Kijiji na Hati za Hakimiliki ya Kimila.<br />

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kuandaa hatimilki za ardhi huanzia kwenye ngazi ya<br />

Halmashauri na huishia katika Ofisi za Ardhi za Kanda. Katika mwaka 2010/2011 Wizara ilitayarisha<br />

na kutoa hatimilki 19,648. Len<strong>go</strong> lilikuwa ni kutoa hatimilki 20,000. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />

yangu inatarajia kutayarisha na kutoa hatimiliki 21,000. Aidha, Wizara itaendelea kuimarisha na<br />

kuboresha matumizi ya teknolojia ya kompyuta ili kuharakisha uandaaji wa hatimiliki na kuimarisha<br />

utunzaji wa kumbukumbu.<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliahidi kufungua Ofisi ya Ardhi<br />

ya Kanda ya Magharibi Mjini Tabora itakayohudumia Mikoa ya Tabora, Shinyanga na Ki<strong>go</strong>ma.<br />

Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa jen<strong>go</strong> kwa ajili ya ofisi hiyo limepatikana. Ofisi hiyo<br />

itatoa huduma za Sekta ya Ardhi ikiwa ni pamoja na huduma za mipan<strong>go</strong> miji na vijiji, upimaji,<br />

umilikishaji, usajili, uthamini na ushauri kuhusu utatuzi wa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi na nyumba. Kwa<br />

mwaka 2011/2012 ukarabati utafanyika ili Ofisi hiyo ianze kutoa huduma kwa wananchi.<br />

Mheshimiwa Spika, mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliahidi kugatua mamlaka ya<br />

kuidhinisha upimaji wa ardhi katika Kanda sita za Sekta ya Ardhi ambazo ni Kanda ya Mashariki<br />

(Dar es Salaam), Kusini (Mtwara), Kusini Magharibi (Mbeya), Kati (Dodoma), Ziwa (Mwanza), na<br />

Kaskazini (Moshi). Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa maandalizi ya kugatua mamlaka<br />

hayo yamekamilika. Ofisi na vitendea kazi vimepatikana.<br />

Kwa mwaka 2011/2012 Wizara itawahamishia kwenye Kanda hizo watumishi<br />

watakaosimamia upimaji, ukaguzi na uidhinishaji wa ramani. Natoa wito kwa wananchi kuzitumia<br />

Ofisi za Kanda za Ardhi na Halmashauri nchini kupata huduma za ardhi, badala ya kufuata<br />

huduma hizo moja kwa moja kwenye Makao Makuu ya Wizara, kwani husababisha gharama na<br />

ucheleweshaji usio wa lazima katika kupata huduma hizo kwa mwananchi. Hata hivyo, ieleweke<br />

kwamba Wizara iko tayari kupokea rufaa pale ambapo mwananchi hakuridhika na maamuzi ya<br />

ofisi ya Kanda.<br />

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Wizara yangu ya mwaka jana, nililiarifu Bunge lako<br />

Tukufu kwamba Wizara itahakiki milki 4,018 katika maeneo ya Tegeta, Mbezi, Jangwani Beach,<br />

Ununio na Boko, Jijini Dar es Salaam. Hadi Juni, 2011, jumla ya milki 3,535 (asilimia 88) zilihakikiwa.<br />

Kazi ya kuhakiki milki 483 zilizobaki itakamilika katika mwaka 2011/2012. Aidha, jumla ya mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro<br />

58 ilijitokeza kutokana na uhakiki huo. Kati ya mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo, 46 (asilimia 79) ilitatuliwa kiutawala na<br />

mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro 12 haikuweza kutatuliwa. Hivyo, wahusika walishauriwa kwenda Mahakamani. Natoa<br />

wito kwa wananchi walioko kwenye maeneo tajwa ambao hawajawasilisha nyaraka zao kwa ajili<br />

ya uhakiki waziwasilishe Wizarani. Vilevile natoa wito kwa wananchi kufuata taratibu sahihi za<br />

kisheria katika kupata ardhi ili kujiepusha na mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro na hasara itokanayo na vitendo vya<br />

kujipatia ardhi kinyume cha sheria.<br />

21

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!