Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
heka 240 bila kushirikisha Vion<strong>go</strong>zi, bila kufuata taratibu na sheria za nchi kwa pretext kwamba<br />
wanataka kujenga Bandari. Sasa kama kule Kurasini kunawashinda, kwa nini mnataka kuja<br />
Vijibweni na kuwahangaisha wananchi Huu mpan<strong>go</strong> ambao mnataka kuja nao, una fit namna<br />
gani katika Mji Kabambe wa Kigamboni Cha kusikitisha zaidi katika suala kubwa na la msingi<br />
namna hii, Wizara inadiriki kutuma Maafisa wa ngazi za chini kwenda kukaa na kuongea na<br />
wananchi pasipo kufuata taratibu. Naomba zoezi hili lisitishwe na taratibu za msingi ziweze<br />
kufuatwa. Hata kwa suala la msingi kama upanuzi wa Bandari, lazima taratibu za msingi zifuatwe.<br />
Mheshimiwa Waziri naomba sana zoezi hilo lisitishwe ili utaratibu wa msingi uweze kufanyika.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya tano kwa nini siungi mkono hoja, katika eneo la<br />
Kisota, kuna viwanja 20,000 vilivyopimwa na Serikali, lakini watendaji wa Wizara ya Ardhi,<br />
wamepima na kutoa kwa wananchi viwanja vichache kuliko maeneo ambayo yamepimwa. Sasa<br />
hivi pale Kisota kuna mapori mengi kweli kweli, hali ambayo imepelekea kuwa na hali kubwa sana<br />
ya uhalifu.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Waziri wa Wizara husika, wafanye audit ya maeneo<br />
yaliyopimwa na idadi ya viwanja vilivyotolewa kwa sababu wajanja wachache ndani ya Wizara<br />
ya Ardhi wanachokifanya sasa hivi, wanapita tena katika yale maeneo na kuanza kutoa kiwanja<br />
kimoja kimoja. Kwa hiyo, naomba hili suala lifuatiliwe, audit iweze kufanyika na yale maeneo<br />
ambayo tayari yamepimwa lakini viwanja havikutolewa basi hayo maeneo yaweze kutolewa kwa<br />
wananchi ambao wanahitaji.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya sita kwa nini siungi mkono hoja, ni suala la Mji mpya<br />
wa Kigamboni na nawashukuru sana Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> ambao wameniunga mkono katika<br />
suala hili. Suala hili ni kubwa na suala hili ni zito, lakini suala hili Serikali mnalichukulia kimzahamzaha.<br />
Wanakigamboni wanataabika tangu wameingia kifun<strong>go</strong>ni Oktoba mwaka 2008 na hawana<br />
matumaini ya kutoka kifun<strong>go</strong>ni. Hawajui tarehe ambayo mtawatoa kifun<strong>go</strong>ni, Serikali imekuwa<br />
kimya mno na majibu ambayo yamekuwa yakitolewa ikiwa pamoja na yale ambayo yametolewa<br />
katika hotuba hii, kwa kweli hayaashirii kwamba Serikali inawatakia neema Wanakigamboni.<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kigamboni, hawawezi kuuza ardhi yao, hawawezi<br />
kuuza nyumba zao, hawawezi kuziendeleza na hawakopesheki. Kwa takriban miaka mitatu sasa<br />
hivi, hakuna kitu chochote cha maana ambacho kinaendelea pale Kigamboni na maswali<br />
ambayo Wanakigamboni wanayo na wangependa kupata majibu ni maswali manne tu. Mradi<br />
huu utaanza lini Mradi huu utaanzia wapi Haki zao za msingi ni zipi na hatima yao ni ipi (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa miaka mitatu Serikali hii imekuwa inapiga chenga<br />
kutoa majibu ya maswali haya ya msingi. Nasikitika kusema kwamba sitaunga mkono hoja mpaka<br />
majibu ya haya maswali manne ya msingi yaweze kupatikana. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama M<strong>bunge</strong> wa Jimbo la Kigamboni, nitakubali mradi<br />
huu ikiwa tu mambo mawili yatafanyika; moja wananchi wa Kigamboni wanufaike na pili<br />
wananchi wa Kigamboni wasisumbuliwe. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kigamboni wamenituma, Serikali ilipotoa tamko<br />
ilisema kwamba ndani ya miaka miwili wangekuwa wameanza mpan<strong>go</strong> wao, sasa wameshapita<br />
hiyo miaka miwili. Wananchi wa Kigamboni wamenituma, itakapofika tarehe 30 Juni, 2012<br />
hawataki kusikia tena kuhusiana na masuala ya mradi huu. Naomba nirudie, wananchi wa<br />
Kigamboni wamenituma, kama Serikali haitakuja na mpan<strong>go</strong> thabiti, itakapofika tarehe 30 Juni,<br />
2012, hawataki tena kuusikia mradi huu, chukueni mradi huo pelekeni sehemu nyingine yoyote,<br />
lakini baada ya hapo wananchi wa Kigamboni hawataki na hawatatoa ushirikiano kwa Serikali<br />
katika suala hili. Ni vema Serikali inapokuja na miradi kama hii, muwe mmeshajipanga, sio mnatoa<br />
zuio wakati wenyewe hamjajiandaa. Kuna matatizo ya msingi na nilipokuwa naangalia katika<br />
hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 26 na 27, wanasema bado wako kwenye mchakato;<br />
wakati wananchi wa Kigamboni wanaumia, Serikali iko kwenye mchakato, wakati wananchi wa<br />
Kigamboni wanaendelea kuwa maskini, Serikali iko kwenye mchakato. (Makofi)<br />
86