28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

heka 240 bila kushirikisha Vion<strong>go</strong>zi, bila kufuata taratibu na sheria za nchi kwa pretext kwamba<br />

wanataka kujenga Bandari. Sasa kama kule Kurasini kunawashinda, kwa nini mnataka kuja<br />

Vijibweni na kuwahangaisha wananchi Huu mpan<strong>go</strong> ambao mnataka kuja nao, una fit namna<br />

gani katika Mji Kabambe wa Kigamboni Cha kusikitisha zaidi katika suala kubwa na la msingi<br />

namna hii, Wizara inadiriki kutuma Maafisa wa ngazi za chini kwenda kukaa na kuongea na<br />

wananchi pasipo kufuata taratibu. Naomba zoezi hili lisitishwe na taratibu za msingi ziweze<br />

kufuatwa. Hata kwa suala la msingi kama upanuzi wa Bandari, lazima taratibu za msingi zifuatwe.<br />

Mheshimiwa Waziri naomba sana zoezi hilo lisitishwe ili utaratibu wa msingi uweze kufanyika.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya tano kwa nini siungi mkono hoja, katika eneo la<br />

Kisota, kuna viwanja 20,000 vilivyopimwa na Serikali, lakini watendaji wa Wizara ya Ardhi,<br />

wamepima na kutoa kwa wananchi viwanja vichache kuliko maeneo ambayo yamepimwa. Sasa<br />

hivi pale Kisota kuna mapori mengi kweli kweli, hali ambayo imepelekea kuwa na hali kubwa sana<br />

ya uhalifu.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Waziri wa Wizara husika, wafanye audit ya maeneo<br />

yaliyopimwa na idadi ya viwanja vilivyotolewa kwa sababu wajanja wachache ndani ya Wizara<br />

ya Ardhi wanachokifanya sasa hivi, wanapita tena katika yale maeneo na kuanza kutoa kiwanja<br />

kimoja kimoja. Kwa hiyo, naomba hili suala lifuatiliwe, audit iweze kufanyika na yale maeneo<br />

ambayo tayari yamepimwa lakini viwanja havikutolewa basi hayo maeneo yaweze kutolewa kwa<br />

wananchi ambao wanahitaji.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya sita kwa nini siungi mkono hoja, ni suala la Mji mpya<br />

wa Kigamboni na nawashukuru sana Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> ambao wameniunga mkono katika<br />

suala hili. Suala hili ni kubwa na suala hili ni zito, lakini suala hili Serikali mnalichukulia kimzahamzaha.<br />

Wanakigamboni wanataabika tangu wameingia kifun<strong>go</strong>ni Oktoba mwaka 2008 na hawana<br />

matumaini ya kutoka kifun<strong>go</strong>ni. Hawajui tarehe ambayo mtawatoa kifun<strong>go</strong>ni, Serikali imekuwa<br />

kimya mno na majibu ambayo yamekuwa yakitolewa ikiwa pamoja na yale ambayo yametolewa<br />

katika hotuba hii, kwa kweli hayaashirii kwamba Serikali inawatakia neema Wanakigamboni.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kigamboni, hawawezi kuuza ardhi yao, hawawezi<br />

kuuza nyumba zao, hawawezi kuziendeleza na hawakopesheki. Kwa takriban miaka mitatu sasa<br />

hivi, hakuna kitu chochote cha maana ambacho kinaendelea pale Kigamboni na maswali<br />

ambayo Wanakigamboni wanayo na wangependa kupata majibu ni maswali manne tu. Mradi<br />

huu utaanza lini Mradi huu utaanzia wapi Haki zao za msingi ni zipi na hatima yao ni ipi (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa miaka mitatu Serikali hii imekuwa inapiga chenga<br />

kutoa majibu ya maswali haya ya msingi. Nasikitika kusema kwamba sitaunga mkono hoja mpaka<br />

majibu ya haya maswali manne ya msingi yaweze kupatikana. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama M<strong>bunge</strong> wa Jimbo la Kigamboni, nitakubali mradi<br />

huu ikiwa tu mambo mawili yatafanyika; moja wananchi wa Kigamboni wanufaike na pili<br />

wananchi wa Kigamboni wasisumbuliwe. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kigamboni wamenituma, Serikali ilipotoa tamko<br />

ilisema kwamba ndani ya miaka miwili wangekuwa wameanza mpan<strong>go</strong> wao, sasa wameshapita<br />

hiyo miaka miwili. Wananchi wa Kigamboni wamenituma, itakapofika tarehe 30 Juni, 2012<br />

hawataki kusikia tena kuhusiana na masuala ya mradi huu. Naomba nirudie, wananchi wa<br />

Kigamboni wamenituma, kama Serikali haitakuja na mpan<strong>go</strong> thabiti, itakapofika tarehe 30 Juni,<br />

2012, hawataki tena kuusikia mradi huu, chukueni mradi huo pelekeni sehemu nyingine yoyote,<br />

lakini baada ya hapo wananchi wa Kigamboni hawataki na hawatatoa ushirikiano kwa Serikali<br />

katika suala hili. Ni vema Serikali inapokuja na miradi kama hii, muwe mmeshajipanga, sio mnatoa<br />

zuio wakati wenyewe hamjajiandaa. Kuna matatizo ya msingi na nilipokuwa naangalia katika<br />

hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 26 na 27, wanasema bado wako kwenye mchakato;<br />

wakati wananchi wa Kigamboni wanaumia, Serikali iko kwenye mchakato, wakati wananchi wa<br />

Kigamboni wanaendelea kuwa maskini, Serikali iko kwenye mchakato. (Makofi)<br />

86

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!