28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

(b) Je, Serikali haioni kuwa Jumuiya kuwanyima pasi hizo kunawadhalilisha<br />

Watanzania hao wanaofanya kazi huko na pia kutengeneza matabaka mion<strong>go</strong>ni mwa nchi<br />

Wanachama<br />

(c)<br />

Je, ni lini Serikali itaondoa kero hiyo kwa raia wake hao<br />

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joyce John Mukya, M<strong>bunge</strong> wa<br />

Viti Maalum lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-<br />

(a) Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Mkataba wa Uenyeji (Headquarters Agreement)<br />

uliotiwa saini mwaka 1996 Mjini Arusha umetamka katika kifungu cha 3(a) kuwa Watanzania<br />

watakaofanya kazi katika ngazi za Watendaji Wakuu na Wataalamu (Executives na Professional<br />

Staff) watastahili kupata pamoja na haki nyingine, Pasi ya Kidiplomasia kwa mujibu wa Kifungu<br />

15(b) cha Sheria Na. 5 ya mwaka 1986 ya haki na Kinga za Wanadiplomasia nchini Tanzania.<br />

Kifungu 15(b) kinaelekeza haki hizo kutolewa kwa kufuata orodha maalum (Part III of the Fourth<br />

Schedule) iliyopo sehemu ya tatu ya jedwali la nne katika Sheria hiyo.<br />

Hata hivyo, wakati wa utekelezaji, kulijitokeza tatizo kwa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki<br />

haikuwemo kwenye orodha ya Mashirika ya Kimataifa yaliyoainishwa katika Sheria na ambayo<br />

Watanzania wanaofanya kazi katika mashirika hayo kupata haki hizo za Kidiplomasia. Hali hii<br />

ilisababishwa na ukweli kuwa, Sheria Na. 5 ya mwaka 1986, ilipitishwa kabla ya kuundwa upya kwa<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki na kusainiwa kwa Mkataba wa Uenyeji kati ya Serikali yetu na Jumuiya<br />

hiyo. Hivyo, Jumuiya hiyo kutokuwepo kwenye orodha iliyoainishwa katika Sheria hiyo ya mwaka<br />

1986.<br />

(b) Mheshimiwa Spika, Jumuiya ya Afrika Mashariki haitoi pasi za kusafiria kwa<br />

wafanyakazi wake wa ngazi yoyote. Pasi za kusafiria za wafanyakazi wa Jumuiya hiyo hutolewa na<br />

nchi wanazotoka kuendana na matakwa ya kisheria ya nchi hizo.<br />

(c) Mheshimiwa Spika, kilio cha Watanzania wanaofanya kazi kwenye Jumuiya ya<br />

Afrika Mashariki katika ngazi za Watendaji Wakuu na Watalaamu (Executive na Professional)<br />

kimetufikia na tumekifanyia kazi ikiwemo kupokea ushauri wa kitaalamu na kisheria. Wakati<br />

wowote kuanzia sasa, Wizara kwa kuzingatia masharti ya Sheria Na. 5 ya mwaka 1986, itaingiza<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye orodha ya Asasi zinazofaidika na kinga na upendeleo wa<br />

kidiplomasia ili Watanzani hao waweze kupata haki hiyo.<br />

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri. Kuna<br />

baadhi ya Watanzania ambao wanamiliki pass hizo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wao<br />

wamezipataje wakati wengine hawana pass hizo<br />

Pili, katika jibu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kuwa si hakika kupata pass<br />

hizo. Naomba nisaidiwe majibu.<br />

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA: Mheshimiwa Spika,<br />

Sheria yetu ya uhamiaji tayari inatoa watu ambao wanastahili kupata pass za kidiplomasia, mfano<br />

ni wafanyakazi katika Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, yaani Foreign Service Officers, lakini pia,<br />

mfano wa Bunge na Maafisa wengine wa ngazi za juu. Mfano ni kama Naibu Katibu Mkuu wa East<br />

Africa - Ndugu Bukuku ambaye amekwenda akiwa tayari anastahili kupata Viza hiyo ya<br />

kidiplomasia.<br />

Bila shaka atakuwepo katika EAC na atakuwa tayari anayo Viza ya kidiplomasia na<br />

inawezekana pia wengine ambao wameingia katika EAC wakiwa tayari wanazo pass hizo za<br />

Kidiplomasia wataendelea kuwa na pass hizo. Tatizo linakuja kwa wale ambao wameingia wakiwa<br />

bado hawastahili na wanategemea mkataba ambao umeingiwa baina yetu sisi na Jumuiya ya<br />

Afrika Mashariki, ndiyo hilo ambalo tunalifanyia kazi. Ahsante.<br />

2

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!