Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
gharama nafuu. Len<strong>go</strong> la Wakala ni kuinua na kuboresha viwan<strong>go</strong> vya nyumba kwa kutumia vifaa<br />
vilivyotafitiwa na vipatikanavyo hapa hapa nchini jambo ambalo litaongeza ubora wa maisha ya<br />
wananchi mijini na vijijini ili kutimiza malen<strong>go</strong> ya MKUKUTA. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inataka ipewe taarifa ni kwa namna na kiasi gani<br />
wakala huu umefanikiwa kutimiza malen<strong>go</strong> ya kuanzishwa kwake kwani ujenzi wa nyumba za<br />
matope, fito na nyasi bado upo pale pale jambo ambalo linasababisha maisha bora kwa kila<br />
Mtanzania kuwa ni kitendawili kwa miaka mingi ijayo! (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kuhusu muhtasari wa matumizi ya fedha za kawaida na maendeleo<br />
kwa mwaka wa fedha 2010/2011, katika mwaka wa fedha 2010/2011 Wizara iliidhinishiwa jumla ya<br />
shilingi 53,848,061,000; kati ya fedha hizo shilingi 6,423,295,000 zilitengwa kwa ajili ya mishahara,<br />
shilingi 25,159,688,000 kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 22,265,078,000 kwa ajili ya miradi<br />
ya maendeleo. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, hadi Mei, 2011 Wizara ilipokea jumla ya shilingi 27,787,178,679 (bilioni<br />
27.7) sawa na asilimia 51.5 ya tengeo la Bajeti kwa mwaka. Kati ya fedha hizo shilingi<br />
25,658,017,495 sawa na asilimia 92.5 ya fedha zilizopokelewa shilingi 13,226,897,075 zilitumika kwa<br />
ajili ya matumizi mengineyo, shilingi 8,499,539,334 zilitumika kulipa mishahara na shilingi<br />
3,931,581,086 zilitumika kutekeleza miradi ya maendeleo. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali<br />
itueleze ni kwa sababu gani kati fedha za maendeleo zilizotengwa shilingi 22,265,078,000/=<br />
zilizoweza kutumika ni shilingi bilioni 3.9 tu Ni miradi mingapi iliyokuwa itekelezwe katika mwaka<br />
wa fedha 2010/2011 imeshindwa kutekelezwa kutokana na kukosekana huko kwa fedha<br />
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani tulikuja na hoja ya kuitaka Serikali iangalie upya<br />
mfumo wake wa ulipaji posho na marupurupu len<strong>go</strong> likiwa na kuisaidia Serikali kuokoa matumizi<br />
yasiyo ya lazima na hatimaye fedha ambazo tunazitumia kulipana posho tuzielekeze kwenye<br />
matumizi yenye tija kwa wananchi. Tunashukuru kwamba hatimaye tulichokuwa tukikipigia kelele<br />
na kubezwa kimeanza kutekelezwa na Serikali hii hii. Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati akiliomba<br />
Bunge kuahirisha hoja ya Wizara ya Nishati na Madini ili waende kujipanga upya alitamka<br />
yafuatayo naomba kunukuu: “Mheshimiwa Spika, ushauri mlioutoa ni wa msingi sana. Moja<br />
mmesema Serikali nunueni mtambo na tusitafute visingizio vya fedha. Kwamba tafuteni kila<br />
mbinu huko, tafuteni, kateni posho zenu, kateni vitu gani, nendeni mkatazame magari<br />
mnayotumia haya, punguza huko. Tazameni OC yenu kikamilifu, mtaona kule ndani yako matumizi<br />
mengine ambayo mkiamua kwa dhati mnaweza kabisa mkayaondoa huko, yakaenda<br />
yakanunua mitambo ya uhakika, yakawasaidia hata kuongeza uwezo wa mafuta kwa ajili ya<br />
mitambo inayotumia mafuta.” Mwisho wa kunukuu. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kumbe inawezekana! Tukiamua kupunguza anasa na starehe na<br />
kuwekeza kwa wananchi wetu, inawezekana! Hakika inawezekana! Katika Wizara hii zaidi ya<br />
shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya posho (wakati ni bilioni 3.9 tu zilitumika kwa shughuli za<br />
maendeleo). Cha kusikitisha zaidi hadi karne hii, kuna posho zinatengwa kwa ajili ya kuwalipia<br />
baadhi ya maafisa bili za maji na umeme kwa maofisa wanaostahili. Mfumo huu umesambaa<br />
mpaka kwenye Halmashauri zetu. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa Serikali kuangalia upya mfumo huu wa kimwinyi na<br />
kuacha huduma hizi binafsi zigharamiwe kwa vion<strong>go</strong>zi wa waandamizi (wakuu) tu wa mihimili<br />
mitatu ya dola! Tatizo kubwa linalotukumba kama nchi, ni kuendesha mambo kwa mazoea.<br />
Lazima tubadilike! (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa niaba ya Kambi ya Upinzani, naomba<br />
kuwasilisha. (Makofi)<br />
SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, naomba kuwashukuru tena Wasemaji wa awali<br />
katika hoja yetu hii kuanzia Waziri, Mwenyekiti na Msemaji wa Kambi ya Upinzani. (Makofi)<br />
Sasa kwa muda nilionao huu maana ni mpaka saa 7.15 mchana naweza kupata watu<br />
wanne tu. Atakayeanza ni Mheshimiwa John Cheyo, atafuatiwa na Mheshimiwa Mary Chatanda,<br />
atafuatiwa na Mheshimiwa Abbas Mtemvu na Mheshimiwa Dunstan Kitandula. (Makofi)<br />
55