28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

gharama nafuu. Len<strong>go</strong> la Wakala ni kuinua na kuboresha viwan<strong>go</strong> vya nyumba kwa kutumia vifaa<br />

vilivyotafitiwa na vipatikanavyo hapa hapa nchini jambo ambalo litaongeza ubora wa maisha ya<br />

wananchi mijini na vijijini ili kutimiza malen<strong>go</strong> ya MKUKUTA. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inataka ipewe taarifa ni kwa namna na kiasi gani<br />

wakala huu umefanikiwa kutimiza malen<strong>go</strong> ya kuanzishwa kwake kwani ujenzi wa nyumba za<br />

matope, fito na nyasi bado upo pale pale jambo ambalo linasababisha maisha bora kwa kila<br />

Mtanzania kuwa ni kitendawili kwa miaka mingi ijayo! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu muhtasari wa matumizi ya fedha za kawaida na maendeleo<br />

kwa mwaka wa fedha 2010/2011, katika mwaka wa fedha 2010/2011 Wizara iliidhinishiwa jumla ya<br />

shilingi 53,848,061,000; kati ya fedha hizo shilingi 6,423,295,000 zilitengwa kwa ajili ya mishahara,<br />

shilingi 25,159,688,000 kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 22,265,078,000 kwa ajili ya miradi<br />

ya maendeleo. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, hadi Mei, 2011 Wizara ilipokea jumla ya shilingi 27,787,178,679 (bilioni<br />

27.7) sawa na asilimia 51.5 ya tengeo la Bajeti kwa mwaka. Kati ya fedha hizo shilingi<br />

25,658,017,495 sawa na asilimia 92.5 ya fedha zilizopokelewa shilingi 13,226,897,075 zilitumika kwa<br />

ajili ya matumizi mengineyo, shilingi 8,499,539,334 zilitumika kulipa mishahara na shilingi<br />

3,931,581,086 zilitumika kutekeleza miradi ya maendeleo. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali<br />

itueleze ni kwa sababu gani kati fedha za maendeleo zilizotengwa shilingi 22,265,078,000/=<br />

zilizoweza kutumika ni shilingi bilioni 3.9 tu Ni miradi mingapi iliyokuwa itekelezwe katika mwaka<br />

wa fedha 2010/2011 imeshindwa kutekelezwa kutokana na kukosekana huko kwa fedha<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani tulikuja na hoja ya kuitaka Serikali iangalie upya<br />

mfumo wake wa ulipaji posho na marupurupu len<strong>go</strong> likiwa na kuisaidia Serikali kuokoa matumizi<br />

yasiyo ya lazima na hatimaye fedha ambazo tunazitumia kulipana posho tuzielekeze kwenye<br />

matumizi yenye tija kwa wananchi. Tunashukuru kwamba hatimaye tulichokuwa tukikipigia kelele<br />

na kubezwa kimeanza kutekelezwa na Serikali hii hii. Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati akiliomba<br />

Bunge kuahirisha hoja ya Wizara ya Nishati na Madini ili waende kujipanga upya alitamka<br />

yafuatayo naomba kunukuu: “Mheshimiwa Spika, ushauri mlioutoa ni wa msingi sana. Moja<br />

mmesema Serikali nunueni mtambo na tusitafute visingizio vya fedha. Kwamba tafuteni kila<br />

mbinu huko, tafuteni, kateni posho zenu, kateni vitu gani, nendeni mkatazame magari<br />

mnayotumia haya, punguza huko. Tazameni OC yenu kikamilifu, mtaona kule ndani yako matumizi<br />

mengine ambayo mkiamua kwa dhati mnaweza kabisa mkayaondoa huko, yakaenda<br />

yakanunua mitambo ya uhakika, yakawasaidia hata kuongeza uwezo wa mafuta kwa ajili ya<br />

mitambo inayotumia mafuta.” Mwisho wa kunukuu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kumbe inawezekana! Tukiamua kupunguza anasa na starehe na<br />

kuwekeza kwa wananchi wetu, inawezekana! Hakika inawezekana! Katika Wizara hii zaidi ya<br />

shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya posho (wakati ni bilioni 3.9 tu zilitumika kwa shughuli za<br />

maendeleo). Cha kusikitisha zaidi hadi karne hii, kuna posho zinatengwa kwa ajili ya kuwalipia<br />

baadhi ya maafisa bili za maji na umeme kwa maofisa wanaostahili. Mfumo huu umesambaa<br />

mpaka kwenye Halmashauri zetu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa Serikali kuangalia upya mfumo huu wa kimwinyi na<br />

kuacha huduma hizi binafsi zigharamiwe kwa vion<strong>go</strong>zi wa waandamizi (wakuu) tu wa mihimili<br />

mitatu ya dola! Tatizo kubwa linalotukumba kama nchi, ni kuendesha mambo kwa mazoea.<br />

Lazima tubadilike! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa niaba ya Kambi ya Upinzani, naomba<br />

kuwasilisha. (Makofi)<br />

SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, naomba kuwashukuru tena Wasemaji wa awali<br />

katika hoja yetu hii kuanzia Waziri, Mwenyekiti na Msemaji wa Kambi ya Upinzani. (Makofi)<br />

Sasa kwa muda nilionao huu maana ni mpaka saa 7.15 mchana naweza kupata watu<br />

wanne tu. Atakayeanza ni Mheshimiwa John Cheyo, atafuatiwa na Mheshimiwa Mary Chatanda,<br />

atafuatiwa na Mheshimiwa Abbas Mtemvu na Mheshimiwa Dunstan Kitandula. (Makofi)<br />

55

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!