28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

makazi holela kwa kushirikiana na baadhi ya Halmashauri. Programu hiyo ni ya utekelezaji wa<br />

miradi mbalimbali ya kuboresha na kuzuia makazi holela mijini. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />

itakamilisha maandalizi ya programu hiyo na itazisaidia Halmashauri kujiandaa kuitekeleza kwa<br />

kutoa mafunzo katika miji ya Sumbawanga, Singida, Mbeya, Tanga, Tabora, Musoma na Iringa.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri<br />

ya Jiji la Mwanza itaendelea kurasimisha makazi kwa kutambua maeneo na kuyapima. Kwa<br />

kushirikiana na Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam itahakiki mipan<strong>go</strong> ya urasimishaji katika<br />

Kata ya Mbezi ili wananchi waweze kupimiwa maeneo yao kwa kuchangia gharama na kupata<br />

hatimiliki. Aidha, Wizara itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais kupitia mradi wa MKURABITA na<br />

wadau wengine kurasimisha na kuzuia makazi holela nchini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu uendelezaji miji mipya na vituo vya huduma, Wizara yangu kwa<br />

kushirikiana na Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam iliendelea na jitihada za kupunguza<br />

msongamano wa shughuli, watu na magari katikati ya Jiji kwa kuanzisha vituo vya huduma katika<br />

maeneo ya pembezoni. Katika mwaka 2010/2011 Wizara iliandaa taratibu za kushirikisha sekta<br />

binafsi katika uendelezaji wa Kituo cha Huduma cha Luguruni katika Manispaa ya Kinondoni. Kwa<br />

mwaka 2011/2012 Wizara itakamilisha mkataba utakaoiwezesha kampuni binafsi kuwekeza katika<br />

ujenzi wa miundombinu ya kituo hicho na kushirikiana na Wizara na Halmashauri ya Manispaa ya<br />

Kinondoni katika uendelezaji wa kituo. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa<br />

ya Temeke itaanzisha Kituo cha Huduma katika eneo la Kon<strong>go</strong>we. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya<br />

Temeke iliendelea na maandalizi ya mpan<strong>go</strong> kabambe wa kujenga Mji Mpya wa Kigamboni, Jijini<br />

Dar es Salaam. Eneo hilo linahusisha Kata za Kigamboni, Tungi, Vijibweni, Mjimwema na Kibada,<br />

pamoja na Mitaa ya Kizani na Mbwamaji katika Kata ya Somangila. Katika mwaka 2010/2011,<br />

Wizara yangu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ilianza<br />

mchakato wa kuunda mamlaka maalum itakayosimamia uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri<br />

ya Manispaa ya Temeke, itakamilisha maandalizi ya mpan<strong>go</strong> kabambe baada ya kuujadili katika<br />

mikutano ya hadhara itakayofanyika kwenye eneo la mpan<strong>go</strong> huo. Wizara pia itakamilisha<br />

uundaji wa mamlaka itakayosimamia uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni (Kigamboni New<br />

City Development Authority). Mamlaka hiyo itaandaa mipan<strong>go</strong> ya kina ya ujenzi wa<br />

miundombinu, itafanya uthamini wa mali na kutayarisha maeneo mbadala na makazi kwa ajili ya<br />

wananchi watakaolazimika kuhama maeneo yao ya sasa na kwenda mapya lakini ndani ya eneo<br />

hilohilo la Kigamboni. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha itaendelea na juhudi za<br />

kutafuta fedha kwa ajili ya kulipa fidia stahiki kwa wananchi. Aidha, mamlaka hiyo mpya itatumia<br />

mbinu za kisasa kupata fedha za kutosha kulipia fidia, kwa mfano kwa kutanganza Municipal<br />

bond ili wananchi wenye uwezo wachangie gharama hizo kwa kujipatia hisa katika eneo hilo<br />

litakalokuwa la kisasa. Nachukua fursa hii kwanza kuwashukuru wananchi wa Kigamboni na<br />

vion<strong>go</strong>zi wao wakion<strong>go</strong>zwa na M<strong>bunge</strong> wao Mheshimiwa Dkt. Faustine Engebert Ndugulile, kwa<br />

ushirikiano wao mkubwa. (Makofi)<br />

Pili, nawaomba waendelee kuwa wavumilivu wakati jitihada zikiendelea kufanyika ili<br />

kukamilisha zoezi hili la kwanza na la kipekee katika nchi yetu. Aidha, napenda kuwakumbusha<br />

wananchi kuwa ni ukiukaji wa Sheria ya Mipan<strong>go</strong>miji kujenga katika eneo la Mpan<strong>go</strong> Kabambe<br />

wa Mji Mpya Kigamboni bila kuwa na kibali halali cha ujenzi, kwani maendelezo yatakayofanyika<br />

kinyume cha sheria hayatatambulika wala kutolewa fidia. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu usimamizi wa mipan<strong>go</strong> ya matumizi ya ardhi vijijini, Wizara<br />

yangu ina jukumu la kusimamia maandalizi ya mipan<strong>go</strong> ya matumizi ya ardhi na kutoa mion<strong>go</strong>zo<br />

ya kuandaa mipan<strong>go</strong> ya kina ya maeneo ya makazi katika vijiji. Mkakati wa kutekeleza jukumu hilo<br />

unahusisha kuziwezesha Halmashauri za Wilaya na Vijiji kupanga, kutekeleza na kufuatilia mipan<strong>go</strong><br />

yao. Katika mwaka 2010/2011 Wizara ilitafsiri mwon<strong>go</strong>zo wa kuandaa mipan<strong>go</strong> ya kina ya makazi<br />

29

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!