28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kigamboni, hivi tunavyosema tuna-develop mahali halafu<br />

ukienda kumfukuza yule mwenyewe hapati hata kitu hivi inakuwa safi kweli Mbona nchi za<br />

wenzetu wengine mtu anapokuja kuwekeza na wewe ndio wanapopata, lakini sisi mtu akija<br />

kuwekeza wewe ndio unakuwa maskini, sasa hali hii itakwenda mpaka lini<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijamaliza, hivi viwanja vinavyopimwa ambavyo vinauzwa<br />

shilingi milioni sita au nane, kiwanja ambayo ni mita 20 kwa 30, hivi mwanamke wa kawaida<br />

anaweza kulipia Hivi kuna kijana anaweza kulipia Kuna mfanyakazi anaweza kulipia Hivi hili<br />

tunalionaje na unapewa siku saba kwamba uwe umelipia, mwaka mmoja umejenga,<br />

inawezekana kweli Hivyo viwanja ni vya matajiri Sasa umekwenda kuchukua ardhi ya yule mtu<br />

maskini ndio umeigawa hiyo halafu na yeye unamgawia kiwanja halafu unamwambia alipie lakini<br />

fidia umempa kiduchu akienda kulipia kile kiwanja amekwisha, anajenga na nini, mtaji wote<br />

umechukua wewe. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ni mengi sana na inahitaji kufumuliwa kabisa. Mimi<br />

namjua Mheshimiwa Katibu Mkuu amekuwa katika Wizara zingine na alikuwa anasifika, tuliposikia<br />

anakwenda Ardhi tukajua anakwenda kumaliza matatizo lakini wanamzunguka, wajanja wengi.<br />

Wizara inahitaji kufumuliwa, wajanja wanajulikana vizuri sana. Ukienda kuona mahekalu yao<br />

huwezi kuamini kwamba huyu eti anapata mshahara wa shilingi 300,000/=. Unapata mshahara<br />

wa shilingi 300,000/= unajenga nyumba ya shilingi milioni 600 zingine umezipata wapi wala huna<br />

mkopo! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki kengele inililie, naomba nisiunge mkono hoja mpaka suala<br />

la Mloganzila lieleweke. Ahsante sana. (Makofi)<br />

MWENYEKITI: Nakushukuru sana Mheshimiwa Zarina, kwa kweli mchan<strong>go</strong> wako ni mahiri<br />

kabisa na leo umetupa msemo mpya pa kunawa pa kuoga. Kwa hiyo, tunakushukuru kwa<br />

mchan<strong>go</strong> wako. (Kicheko)<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, tunaendelea, naona Mheshimiwa Rebecca Mn<strong>go</strong>do hayupo<br />

basi naomba nimwite Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalifa.<br />

MHE. KHALIFA SULEIMAN KHALIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa fursa<br />

ya kusema kido<strong>go</strong> katika Wizara hii ambayo ni Wizara muhimu sana katika nchi yetu. Labda nianze<br />

kusema, nashangaa kido<strong>go</strong> ninapoona kuna Wizara moja ya Serikali inapewa fedha pending<br />

bilioni 350 lakini Wizara nyeti kama hii unaipa shilingi bilioni 47, nashindwa kuelewa au tuambiwe<br />

hapa kuwa hizi fedha zimetolewa zimsaidie Mheshimiwa Waziri wa Ardhi akapime ardhi katika<br />

Jimbo lake lakini kama ni kwa ajili ya nchi nzima, hiki ni kichekesho kikubwa, haiwezekani. Niliamua<br />

nianze na hilo na hapa ndipo itakapokuja lawama hapo baadaye, umeacha fedha ya kununua<br />

ugali na kauzu unarudi nyumbani unasema pilau, juice na mambo mengine, utakuwa ni baba wa<br />

ajabu sana. Sasa Serikali kama itafikia pahali ikasema Wizara ya Ardhi haikufanya kazi yake,<br />

nafikiri itahitaji kulaumiwa yenyewe.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye Wizara. Ameshasema mtangulizi wangu hapa<br />

Wizara ya Ardhi kuna mambo mengi ya kusikitisha na nianze na mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro inayojitokeza. Kuna<br />

maeneo watu wanavunjiwa nyumba zao na hapa Dodoma yapo maeneo hayo. Kuna maeneo<br />

yanaitwa Mji Mpya, miaka mitatu iliyopita watu wamevunjiwa nyumba 150 na mpaka leo<br />

hawajalipwa. Kinachosikitisha watu hawa wakati wanapiga matofali wanatafuta vitu mbalimbali<br />

wanaonekana lakini Serikali imenyamaza kimya, mpaka mtu anajenga nyumba ndio unakwenda<br />

kumvunjia Mtanzania mnyonge. Sasa huu kweli ni ubinadamu, huu ni uungwana au hiki ni kitu<br />

gani Serikali ambayo unategemea ikulinde na ikusaidie katika matatizo yako, inakutafutia namna<br />

ya kuku-fix ili ikufilisi, ili ikumalize, ili ikurudishe nyuma. Mimi nafikiri huo si mwenendo mzuri na si<br />

ustarabu mzuri.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mwingine wa hapahapa Dodoma pale Mzakwe,<br />

wamevunjiwa watu nyumba zao kwa kisingizio kuwa pana mashine ya maji, mimi nakubali,<br />

unahamisha watu lakini kwa nini unawahamisha wengine, wengine unawaacha Wafanyakazi<br />

wapo, kama ni vyoo, kwenye nyumba zao kuna vyoo, kama wanaweza kuharibu maji na wale<br />

71

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!