28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Serikali kufikia muafaka wa kuhakikisha wananchi wale hawadhalilishwi. Nakataa kabisa kauli ya<br />

Mheshimiwa Waziri ya kusema maeneo hayo yamevamiwa. Hakuvamia mtu pale. Wanaovamia<br />

maeneo ni vyura sio watu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, wale watu wako pale, wamejenga, wana huduma ya maji,<br />

umeme, barabara na leo Serikali Kuu inajenga barabara mpya kutokana na watu walivyoboresha<br />

maeneo yale. Kwa hiyo, kama kuna mpan<strong>go</strong> Jangwani, kwanza uwajali watu wa pale,<br />

wajengewe maeneo mazuri pale pale, halafu ndiyo mtuletee maeneo ya watu kupumzika na<br />

mkija na ice cream zenu ndiyo mtakula, sisi tutakula ubuyu nyie kuleni ice cream. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu hawa hawana ndoto ya utajiri, watu hawa hawana ndoto<br />

za nyumba, watu hawa ndoto zao ni kusomesha watoto wao, watu hawa ni maskini, hawana<br />

mbele hawana nyuma, wako watu wamekaa pale zaidi ya 10,000 na hao ndiyo watu<br />

wamekichagua Chama cha Mapinduzi, ndiyo watu wanaompenda Rais, leo Waziri anakwenda,<br />

anaibua mpan<strong>go</strong> wa mwaka 1979 anatuletea hapa anasema ndiyo anataka tuufanye Hiyo sisi<br />

hatukubali. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, aje akae na sisi, atueleze sisi vion<strong>go</strong>zi, tuelewe mpan<strong>go</strong> huu<br />

kwanza kwa kujali wale wanyonge wa maeneo yote ya Jangwani na Mchikichini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tena hakuna mtu anayependa watu wale waishi vile,<br />

lakini hakuna njia nyingine. Wale watoto wao wote wanasoma mjini, hivi uwatoe pale uwapeleke<br />

Maji Matitu, watoto hawa watasoma lini (Kicheko/Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo hatukubali, mnatakiwa mlielewe hilo. Nilitegemea<br />

Mheshimiwa Waziri angekuja na bajeti yake ashughulikie hati feki, mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya viwanja, rushwa<br />

ndani ya Wizara yake, kitu ambacho anashindwa kukisema, matokeo yake mnakwenda<br />

kunyanyasa maskini wa Mungu, hawana mbele wala nyuma, hilo muache. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri hata maeneo yenu Mheshimiwa Waziri na Naibu huko<br />

kwenu kuna mabonde vilevile anzeni kule kuweka mahali pa kupumzika sio huku. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza hata bajeti yenyewe hamna, hamna hela za kuendesha<br />

Wizara yenu mtakwenda kuboresha nini Huu mtikisiko wa uchumi duniani kweli mtampata mtu<br />

Mnarusha watu roho, watu wanashindwa kuamka asubuhi sababu ya mambo yenu hayo<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya nakuja, katika suala la National Housing. Kwanza<br />

niwapongeze National Housing na Bodi, namjua Chairman Mitta na Director General, wanafanya<br />

kazi nzuri na mpan<strong>go</strong> wao wanaosema ni mzuri wa kuondoa nyumba ndo<strong>go</strong>ndo<strong>go</strong> mijini, kuweka<br />

nyumba kubwa, hiyo ndiyo njia ya kuwakomboa watu na hiyo ndiyo spirit ya kufanya, lakini lazima<br />

kwanza Serikali hii kwenye Bunge lililopita na M<strong>bunge</strong> wa Temeke kasema na mimi sasa nanukuu,<br />

watu wanasema Wa<strong>bunge</strong> wa CCM hawasomi, hawafuatilii hivi vitabu, si kweli sisi tunasoma zaidi<br />

ya hawa wengine. Sasa nitamsomea Mheshimiwa Waziri, hii ni bajeti ya Chiligati ya mwaka jana<br />

ukurasa wa 57 kitu ambacho Mheshimiwa Waziri hakusema wala Kamati ya nyumba haikusema.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema hivi katika ukurasa wa 57, bajeti ya 2010/2011 kwa<br />

ruhusa yako, naomba ninukuu:-<br />

“Mheshimiwa Spika, katika hotuba yangu ya bajeti iliyopita, iliyopita hii sasa ya mwaka<br />

jana, iliyopita ina maana ya 2009/2010, hii ilikuwa 2010/2011 niliarifu kuhusu azma ya National<br />

Housing kuuza baadhi ya nyumba zake ambazo gharama za kuziendesha ni kubwa kuliko<br />

mapato. Zoezi hili linahitaji maandalizi makubwa, maandalizi hayo yanahusu kuwatambua<br />

wapangaji wa nyumba hizo na uwezo wao wa kulipia ununuzi. Kutafuta benki ziwakopeshe fedha<br />

za ununuzi, hizo flats na pia kuelimisha wahusika taratibu za umilikishaji nyumba hizo chini ya sheria<br />

ya umilikishaji wa sehemu ya jen<strong>go</strong>. Maandalizi haya yakikamilika ndipo zoezi la uuzwaji wa<br />

nyumba hizi utaanza kutekelezwa. Napenda kurudia tena kwamba National Housing watauza<br />

sehemu tu ya nyumba zilizowapa hasara kuziendesha na sio nyumba zote.”<br />

88

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!