28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Wizara ya Ardhi haijatoa tamko kuwaambia wale watu. Hivi kweli kama Serikali inataka itashindwa<br />

kuwasindikiza hata na Polisi wale watu waliokuja, huyu consultant akaenda kuchukua udon<strong>go</strong>,<br />

watashindwa kuwasindikiza hawa watu wa Wizara ya Ardhi kwenda kufanya survey au ndio<br />

kwamba huo mradi hautakiwi ili kusudi viwanja vibaki tupate kugawana Mambo ya Air Tanzania<br />

na KLM ilikuwa hivihivi. KLM walianza kuja Tanzania lakini ikawa pa kunawa, pa kuoga, pa kunawa<br />

pa kuoga mwisho wamekwenda Kenya. (Makofi/Kicheko)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mkataba wa mradi huu unasema hivi, gharama yoyote<br />

itakayoongezeka kwa sababu ya kutokutekelezwa italipwa na Serikali ya Tanzania, hiyo moja. Pili,<br />

mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi ikitokea watahamisha mradi huu na kuupeleka kwingine. Leo tokea tarehe 28<br />

Juni wako hapa mpaka hivi ninavyozungumza hakuna kinachoeleweka, hivi hawaondoki hawa<br />

Sasa wakiondoka hawa sisi tumepata nini jamani Ni kweli Serikali inashindwa kwenda<br />

kuwasimamia wakachukua udon<strong>go</strong> tena baada ya kulipwa shilingi bilioni nane Mimi sielewi<br />

kabisa.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo siungi mkono hoja hii mpaka niambiwe ni jinsi gani wale<br />

watu watakwenda kuchukua udon<strong>go</strong>, ni jinsi gani Ardhi watakwenda kupima halafu waondoke<br />

waende wakatutengenezee mambo tuje kujenga. Kama hawa watu wengine wanadai shilingi<br />

bilioni mbili hivi kweli tuukose mradi wa shilingi bilioni 115 Rais aliokwenda kuutafuta huko Ughaibuni<br />

kwa ajili ya shilingi bilioni mbili Haieleweki! Hilo naliomba la kwanza, Mloganzila wanasubiri, Diwani<br />

ananiambia hata tamko tu la Wizara, anasema Wizara wanashindwa kuja kwetu kutuambia<br />

jamani tatizo ni hili, moja, mbili na tatu. Sisi MUHAS wamekwenda kule wameongea nao<br />

wakatuambia sisi hatuwajui ninyi.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dar es Salaam Mji mkubwa, kuna mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro mingi sana ya ardhi.<br />

Mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hii inaletwa na Wizara ya Ardhi na Wizara ya Ardhi namhurumia sana Mama Tibaijuka,<br />

kwa sababu mingine ameikuta, lakini pale pana Watendaji wabovu sana. Sio kwamba<br />

wanafanya labda kwa bahati mbaya hapana, makusudi kabisa. Kiwanja kinaweza kikatolewa<br />

kwa watu wawili au watatu na ukienda jina lako leo linaweza likawepo kesho ukienda halipo.<br />

Kubadilisha majina kwenye kompyuta shilingi million sita, inatokea hiyo. Akitaka nitamwambia na<br />

majina yao watu wanaofanya hivyo. Mimi niko tayari kumsaidia Mheshimiwa Waziri kwa sababu<br />

vinatia aibu na vinatia uchungu lakini siku hizi jamani si kuna hawa computer forensic, kwa nini<br />

usiwaite computer forensic, nenda ukachambue zile kompyuta majitu utakayokuta kule utazimia.<br />

Ni mambo ya ajabu, ni mambo ya aibu na wana-chain kabisa Wilaya ya Kinondoni ndio<br />

wakubwa wa hao. Hata Mheshimiwa Lukuvi Kamati yake ilipowasimamisha wengine sasa hivi<br />

wanatafuta njia za kurudi kwa milan<strong>go</strong> ya nyuma, tunajua kwa sababu ndio chain yao. Kwa hiyo,<br />

nakuomba Mheshimiwa Waziri ushughulikie suala hili.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna viwanja vingine ambavyo wananchi wamegawiwa,<br />

vimetoka Ardhi anakwenda kule kwenye kiwanja anafurushwa, aliyemkuta anasema mimi<br />

sijalipwa huwezi kuingia hapa na bahati mbaya sana wengine ni akinamama. Wakirudi Wizarani<br />

wanaambiwa wao hawana taarifa na Temeke wanasema hawana taarifa. Mheshimiwa Waziri<br />

naomba ulichukue hilo kwa sababu akinamama wamekuja kunililia hawajui mahali pa kwenda,<br />

Wizarani wamefukuzwa, Wilayani wamefukuzwa ofa zao wanazo mkononi.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iangalie, kuna viwanja vinaitwa vya miradi,<br />

viwanja hivi vya miradi ni viwanja gani na ndio hivyo vinavyotumika kula. Mimi nakuomba<br />

uangalie hivyo viwanja vya miradi na utavikuta viko katika lucrative arrears lakini uvamizi wa<br />

viwanja umekithitri na unaondoa amani Dar es Salaam. Hilo lazima mliangalie jamani, naona<br />

watu wapo tu hakuna mtu analiangalia, jamani na wavamizi wanakwenda kila siku. Kuna mtu<br />

ambaye kila siku anavamia na anakwenda kubomolea watu nyumba, wanafukuzwa hakuna<br />

kinachosemwa.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kengele yangu ya pili haijalia, naomba nizungumzie<br />

kuhusu hii Sheria ya Ardhi. Tunaomba Sheria ya Ardhi iangaliwe upya ina upungufu mwingi sana.<br />

Hilo silisemei sana maana kuna watu tayari wamelisemea.<br />

70

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!