Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe rai kwa Wa<strong>bunge</strong> wenzangu, naomba mniunge<br />
mkono, naomba tusipitishe hii bajeti ya Wizara mpaka pale Serikali itakapokuja na majibu ya<br />
msingi, najua ndani ya Bunge hili Tukufu kuna Wa<strong>bunge</strong> zaidi ya 50 ambao ni wakazi au<br />
wamewekeza katika Jimbo la Kigamboni, naomba waniunge mkono katika hili, tuwatetee<br />
wananchi wa Kigamboni, naomba bajeti hii isipite mpaka pale majibu ya msingi yatakapoweza<br />
kupatikana. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema tena, kauli ambayo nimeitoa kwamba<br />
baada ya tarehe 30 Juni, 2012, kama Serikali hamtakuja na mpan<strong>go</strong> thabiti ambao unaainisha na<br />
kujibu masuala ya msingi, naomba msije tena Kigamboni. Mimi nitakuwa wa kwanza kuwasimamia<br />
na kuwatetea wale wote ambao watakuwa wamevunja agizo la Serikali. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tu muwe makini, mkajipange, mje na<br />
mpan<strong>go</strong> thabiti ambao utaonesha lini na wapi mnaanza na mnaanza na nini, haki za<br />
Wanakigamboni zitakuaje Naomba niseme wananchi wa Kigamboni katika masuala ya fidia<br />
wanataka mambo matatu; kwa wale ambao hawatoweza, wapewe fidia yao na wahame na<br />
fidia iwe katika bei ya soko. Wale ambao watakuwa na uwezo wanataka kuingia ubia na<br />
wawekezaji na wengine ambao wana uwezo mkubwa zaidi wanataka kuyaendeleza yale<br />
maeneo yao wao wenyewe, watachukua fedha benki, watafanya hiyo kazi. Kwa hiyo, naomba<br />
utaratibu huo utumike, najua kabisa Mheshimiwa Waziri ana uzoefu mkubwa, wananchi wa<br />
Kigamboni wana imani ingawa majibu yake ya tarehe 31 Machi, 2011 hayakukidhi haja. Kwa hiyo,<br />
naomba arudi tena akiwa na majibu ya msingi katika suala hili.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo machache, siungi mkono hoja. (Makofi)<br />
MHE. MUSSA Z. AZZAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru sana kwa kunipa<br />
nafasi, lakini namshukuru Mwenyezi Mungu vile vile kwa kunipa fursa na pumzi kuwepo hapa<br />
pamoja na wewe na Watanzania wote na Vion<strong>go</strong>zi wetu wote. Nawashukuru wananchi wangu<br />
wa Jimbo la Ilala kwa kunisaidia na kushirikiana na mimi katika maendeleo ya Jimbo letu.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza na mimi naanza kwa kauli thabiti na swaumu yangu<br />
siungi mkono hoja. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, siungi mkono hoja, narudia maneno kwanza aliyoandika<br />
Mheshimiwa Waziri kwa maneno mazuri na matamu na kuya-highlight kwa maandishi makubwa<br />
anaposema kuwa Mheshimiwa Spika, Jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na uhaba mkubwa wa<br />
maeneo ya kupumzika, tunakubali kabisa Jiji la Dar es Salaam halina maeneo ya kupumzika. Lakini<br />
Jiji la Dar es Salaam sio halina maeneo ya kupumzika tu, halina hata maeneo ya kuegesha<br />
magari. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika eneo ambalo umeliona mnataka liwe eneo la<br />
kupumzika, ni eneo la Jangwani, nakubaliana na wala sikubali kabisa mazingira ya watu<br />
wanaoishi Jangwani kwa hali ile. Lakini hawana budi kuishi vile kutokana na umaskini ambao<br />
wanao. (Makofi)<br />
Kwa hiyo, kama kuna mpan<strong>go</strong> ambao unaletwa na Serikali Jangwani na Mchikichini na<br />
maeneo yote ya Majangwani yaliyoandikwa hapa, ni lazima yashirikishe wananchi wenyewe<br />
waliohusika. Ni lazima washirikishe watu waliowakuta katika maeneo yao, sasa kama mnataka<br />
kufukuza watu Mchikichini na maeneo ya Jangwani, ili muweke maeneo, mkitoa Oystebay mje<br />
kula ice cream pale, hatukubali. Tutabanana hapo hapo na ikibidi niko radhi mimi Mussa Azzan<br />
Zungu, M<strong>bunge</strong> Jimbo la Ilala kujiuzulu Bunge, kujiunga na wananchi na kwenda Mahakamani<br />
kuzuia mpan<strong>go</strong> huu kama hamtashirikisha wananchi waliokuwepo pale. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnasema kuna agizo la Rais, na sisi tunaheshimu, mbona kuna<br />
agizo la Rais kuuza nyumba mlishindwa wala hamtaki kuuza nyumba Kwa hiyo, huo upepo wa<br />
Jangwani na sisi tunataka tupumzike. Nilikuwa nategemea mseme mnakuja na mpan<strong>go</strong>.<br />
Mheshimiwa Waziri umenitia hofu, sasa hivi Jangwani watu hata kufuturu hawajui watafuturu wapi,<br />
roho zao zimewaruka na mimi nawathibitishia wananchi wote mabondeni, tulieni, tutakaa na<br />
87