28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

tabia ya kuandika vijinoti kutoka juu kuagiza na kuwaelekeza vion<strong>go</strong>zi wa Serikali za Vijiji kwamba<br />

wawagawie ama wawapimie maeneo hayo na hatimaye kuwamilikisha ardhi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba maadamu nime<strong>go</strong>ngewa hiyo kengele ya<br />

kwanza, niseme haya niliyokuwa nayo yanatosha, niunge mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)<br />

MHE. ABBAS Z. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.<br />

Mheshimiwa Spika, wakati nikichangia hotuba ya Waziri Mkuu, nilizungumzia maeneo<br />

mawili, Nishati na Madini na Wizara ya Ardhi. Jioni nilipata simu kutoka kwa mama mzazi anaitwa<br />

Bi. Siti Kilun<strong>go</strong> Mwihiyawe.<br />

SPIKA: Yaani mama yako wewe<br />

MHE. ABBAS Z. MTEMVU: Eeh! Mama mzazi, akaniambia mwanangu mbona umechangia<br />

kwa sauti kubwa sana, mimi sikujielewa, akaniambia angekuwa hai baba yako, asingependa,<br />

angependa uchangie kwa sauti ya taratibu lakini watu waelewe, kwa hiyo sauti yangu leo<br />

itabadilika. (Kicheko)<br />

Mheshimiwa Spika, niwashukuru sana wapigakura wangu wa TMK kwa imani kubwa na<br />

mapenzi makubwa kwangu. Wamekuwa wakipata tabu siku hizi, sasa nisiposema kido<strong>go</strong><br />

wanaweza wasielewe. Wamesikia mambo mengi ya DDC, niwahakikishie huko sipo, mwaka 2009<br />

mwenye dhamana, Mama Celina Kombani aliunda Tume ambayo ina taarifa zote za DDC. Kwa<br />

hiyo, wasiwe na wasiwasi sipo, hizo ni kelele za mlan<strong>go</strong> ambazo hazimzuii mwenye nyumba kulala.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, niende moja kwa moja Kurasini. Nilichangia wakati wa Waziri Mkuu,<br />

Mheshimiwa Waziri anakumbuka, ndugu zangu wa Kurasini wana matatizo kwelikweli na Waziri<br />

amezungumza kwamba ule mpan<strong>go</strong> wa Kurasini ulianza toka mwaka 2006. Waheshimiwa<br />

Wa<strong>bunge</strong> hebu tuangalie wananchi hawa wanavyopata tabu toka mwaka 2006 leo mwaka 2011<br />

watu hawajalipwa fidia, wanazuiwa nyumba zao kutengeneza hata choo!<br />

Mheshimiwa Spika, nilipata taarifa jana zimenisikitisha kweli, Bwana Afya anapita Kurasini,<br />

wale ambao vyoo vyao vibovu anawatoza faini ya shilingi 40,000 mpaka shilingi 50,000, nimesikitika<br />

kwelikweli. Nilitamani yule Bwana Afya nimfukuze kazi, nikasema taratibu na sheria haziniruhusu,<br />

nisije nikafukuza kazi watu barabarani kumbe taratibu haziniruhusu, nikamuomba Mwenyezi<br />

Mungu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, inasikitisha kweli lakini kilichonisikitisha zaidi ni hotuba ya Mheshimiwa<br />

Waziri katika ukurasa wa 25 naomba ninukuu, inasema:-<br />

“Nichukue fursa hii kuwashukuru wananchi wa eneo la mradi, ana maana Kurasini, kwa<br />

uvumilivu na ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi …”<br />

Mheshimiwa Spika, mimi nashindwa kuelewa hawa watu wanasubiri pesa zao ili waweze<br />

kuondoka lakini Mheshimiwa Waziri anasema anawashukuru kwa uvumilivu. Mimi kwa sababu<br />

nilichangia hotuba ya Waziri Mkuu, nilitarajia leo Mheshimiwa Waziri angesimama hapa angesema<br />

Bunge likiisha anakwenda kuwalipa hawa watu lakini uvumilivu gani usiokuwa na mwisho Wale<br />

watu wanateseka, hebu tujifikirie tungekuwa sisi, ni bora kama ule mradi hatuuwezi tuwaambie<br />

wananchi wajenge nyumba zao, waendelee kuishi kuliko kuendelea kuwatesa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mimi napata wasiwasi sana tunapozungumzia mradi wa Kigamboni<br />

na tukionyeshwa picha nzuri. Kama wananchi wa Kurasini, mradi wa kuendeleza bandari toka<br />

mwaka 2006 mpaka leo wananchi wale hawajalipwa, wanapata taabu kwelikweli na cha<br />

kusikitisha zaidi, mimi Temeke nimeshinda kwa kura nyingi 58, lakini Kurasini sikushinda na sababu ni<br />

hiyohiyo ya ule mradi.<br />

60

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!