Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
tabia ya kuandika vijinoti kutoka juu kuagiza na kuwaelekeza vion<strong>go</strong>zi wa Serikali za Vijiji kwamba<br />
wawagawie ama wawapimie maeneo hayo na hatimaye kuwamilikisha ardhi. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba maadamu nime<strong>go</strong>ngewa hiyo kengele ya<br />
kwanza, niseme haya niliyokuwa nayo yanatosha, niunge mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)<br />
MHE. ABBAS Z. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.<br />
Mheshimiwa Spika, wakati nikichangia hotuba ya Waziri Mkuu, nilizungumzia maeneo<br />
mawili, Nishati na Madini na Wizara ya Ardhi. Jioni nilipata simu kutoka kwa mama mzazi anaitwa<br />
Bi. Siti Kilun<strong>go</strong> Mwihiyawe.<br />
SPIKA: Yaani mama yako wewe<br />
MHE. ABBAS Z. MTEMVU: Eeh! Mama mzazi, akaniambia mwanangu mbona umechangia<br />
kwa sauti kubwa sana, mimi sikujielewa, akaniambia angekuwa hai baba yako, asingependa,<br />
angependa uchangie kwa sauti ya taratibu lakini watu waelewe, kwa hiyo sauti yangu leo<br />
itabadilika. (Kicheko)<br />
Mheshimiwa Spika, niwashukuru sana wapigakura wangu wa TMK kwa imani kubwa na<br />
mapenzi makubwa kwangu. Wamekuwa wakipata tabu siku hizi, sasa nisiposema kido<strong>go</strong><br />
wanaweza wasielewe. Wamesikia mambo mengi ya DDC, niwahakikishie huko sipo, mwaka 2009<br />
mwenye dhamana, Mama Celina Kombani aliunda Tume ambayo ina taarifa zote za DDC. Kwa<br />
hiyo, wasiwe na wasiwasi sipo, hizo ni kelele za mlan<strong>go</strong> ambazo hazimzuii mwenye nyumba kulala.<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, niende moja kwa moja Kurasini. Nilichangia wakati wa Waziri Mkuu,<br />
Mheshimiwa Waziri anakumbuka, ndugu zangu wa Kurasini wana matatizo kwelikweli na Waziri<br />
amezungumza kwamba ule mpan<strong>go</strong> wa Kurasini ulianza toka mwaka 2006. Waheshimiwa<br />
Wa<strong>bunge</strong> hebu tuangalie wananchi hawa wanavyopata tabu toka mwaka 2006 leo mwaka 2011<br />
watu hawajalipwa fidia, wanazuiwa nyumba zao kutengeneza hata choo!<br />
Mheshimiwa Spika, nilipata taarifa jana zimenisikitisha kweli, Bwana Afya anapita Kurasini,<br />
wale ambao vyoo vyao vibovu anawatoza faini ya shilingi 40,000 mpaka shilingi 50,000, nimesikitika<br />
kwelikweli. Nilitamani yule Bwana Afya nimfukuze kazi, nikasema taratibu na sheria haziniruhusu,<br />
nisije nikafukuza kazi watu barabarani kumbe taratibu haziniruhusu, nikamuomba Mwenyezi<br />
Mungu. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, inasikitisha kweli lakini kilichonisikitisha zaidi ni hotuba ya Mheshimiwa<br />
Waziri katika ukurasa wa 25 naomba ninukuu, inasema:-<br />
“Nichukue fursa hii kuwashukuru wananchi wa eneo la mradi, ana maana Kurasini, kwa<br />
uvumilivu na ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi …”<br />
Mheshimiwa Spika, mimi nashindwa kuelewa hawa watu wanasubiri pesa zao ili waweze<br />
kuondoka lakini Mheshimiwa Waziri anasema anawashukuru kwa uvumilivu. Mimi kwa sababu<br />
nilichangia hotuba ya Waziri Mkuu, nilitarajia leo Mheshimiwa Waziri angesimama hapa angesema<br />
Bunge likiisha anakwenda kuwalipa hawa watu lakini uvumilivu gani usiokuwa na mwisho Wale<br />
watu wanateseka, hebu tujifikirie tungekuwa sisi, ni bora kama ule mradi hatuuwezi tuwaambie<br />
wananchi wajenge nyumba zao, waendelee kuishi kuliko kuendelea kuwatesa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, mimi napata wasiwasi sana tunapozungumzia mradi wa Kigamboni<br />
na tukionyeshwa picha nzuri. Kama wananchi wa Kurasini, mradi wa kuendeleza bandari toka<br />
mwaka 2006 mpaka leo wananchi wale hawajalipwa, wanapata taabu kwelikweli na cha<br />
kusikitisha zaidi, mimi Temeke nimeshinda kwa kura nyingi 58, lakini Kurasini sikushinda na sababu ni<br />
hiyohiyo ya ule mradi.<br />
60