Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Malen<strong>go</strong> ya Milenia. Hivyo, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu liidhinishe Makadirio<br />
ya Mapato na Matumizi kama ifuatavyo:-<br />
(i) Mapato - Mapato ya Serikali shilingi 20,645,006,000;<br />
(ii) Matumizi ya Kawaida - Matumizi ya Mishahara shilingi 7,351,409,000; Matumizi Mengineyo<br />
(OC) shilingi 18,353,352,000; Jumla shilingi 25,884,761,000;<br />
(iii) Matumizi ya Miradi ya Maendeleo - Matumizi ya Maendeleo Fedha za Ndani shilingi<br />
6,000,000,000; Fedha za Nje shilingi 16,010,437,000; Jumla shilingi 22,010,437,000.<br />
Mheshimiwa Spika, jumla ya Matumizi ya Mishahara, Matumizi Mengineyo na Matumizi ya<br />
Maendeleo ni shilingi 47,895,198,000. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, napenda kukushukuru tena wewe na Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> wote<br />
kwa kunisikiliza. Hotuba hii inapatikana pia kwenye tovuti ya Wizara yenye anuani ya<br />
www.ardhi.<strong>go</strong>.<strong>tz</strong>. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)<br />
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, naafiki. (Makofi)<br />
(Hoja ilitolewa iamuliwe)<br />
SPIKA: Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, kabla sijamuita Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia Wizara hii,<br />
wakati natangaza wageni nilipitiwa kwa bahati mbaya wageni wa Mheshimiwa Waziri Kivuli wa<br />
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Halima Mdee nimewaruka kwa bahati<br />
mbaya. (Makofi)<br />
Hawa ni wageni wake kutoka jimboni kwake Jimbo la Kawe yupo Ester Samanya, tena<br />
wamekaa kwenye Speakers Gallery I am sorry. Yupo Deusdedit Mtiro, Magesa Kazinyingi, Powell<br />
Mfinanga, Martha Charles, Milka Bulaza na Brighton Babile. (Makofi)<br />
Halafu juzi tulikuwa na msanii mwingine wa shughuli za daladala leo tuna msanii mwingine<br />
wa nyimbo za Injili anaitwa Bibi Beatrice Muhone. Huyu ni mwimbaji wa Nyimbo wa Injili yupo hapa<br />
Dodoma kwa ajili ya kuzindua kanda yake. Kwa hiyo, kama ni hapa Dodoma basi mkisikia huko<br />
basi mwende tu. (Makofi)<br />
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA – K.N.Y. MWENYEKITI WA KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA<br />
MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kanuni ya 99(7) ya Kanuni za Bunge, Toleo la 2007,<br />
naomba kuwasilisha Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kuhusu<br />
utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa<br />
fedha 2010/2011 na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hii kwa<br />
mwaka wa fedha 2011/2012. (Makofi)<br />
Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uzima, afya njema na<br />
kuniwezesha kuwasilisha maoni haya mbele ya Bunge lako Tukufu. Kabla sijawasilisha maoni ya<br />
Kamati naomba nichukue fursa hii kukushukuru wewe binafsi kwa kunipa fursa hii ili niweze<br />
kuwasilisha maoni ya Kamati. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, nitakuwa mkosefu wa fadhila kama sitawashukuru wapiga kura wangu<br />
wote wa Mkoa wa Mbeya na hasa Jumuiya ya Umoja wa CCM (UWT) wa Mkoa wa Mbeya kwa<br />
kunichagua kwa kishindo kuwa M<strong>bunge</strong> wao kwa kipindi cha miaka mitano na kwa ushirikiano<br />
mkubwa wanaonipatia katika kutekeleza majukumu yangu kama M<strong>bunge</strong>. Ninawahakikishia nipo<br />
pamoja nao na pindi shughuli za Bunge zitakapomalizika nitarudi kuungana nao ili tuendelee<br />
kushirikiana kwa pamoja katika kuendelea kuuletea Mkoa wetu wa Mbeya maendeleo.<br />
Nawaahidi kamwe sitawaangusha. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee kabisa nitoe shukrani zangu za dhati kwa familia<br />
yangu yote na hasa watoto wangu wapendwa Joseph na David. Ninawashukuru kwa uvumilivu<br />
37