28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nakuomba sana Mheshimiwa Waziri, haya ni<br />

makubaliano ambayo tumeshakubaliana tayari, vikao vimekaa na ushahidi upo. Sasa kuna nini<br />

kinachotukwamisha sisi kuhamisha Kata mbili zile kuja mjini Tunataka jibu hilo.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee, sisi tuna mji leo ndani ya nchi yetu Mikoa miwili tu ndio<br />

inayofanana ni Mtwara-Mikindani na Ki<strong>go</strong>ma-Ujiji, tuna Mji pale unaitwa Mikindani ni Mji wa<br />

kihistoria. Tangu sijazaliwa watu wako pale, marehemu baba yangu alikuwa anafanya kazi pale<br />

bandarini Mikindani, wazee wameacha majumba yao mpaka wamekuwa wameacha na urithi<br />

wa majumba kwa watoto wao. Leo tuna tatizo ndani ya Mji wa Mikindani, tunaambiwa ule mji<br />

hawawezi kupima na kutoa hati. Wale watu wamejenga wazazi wetu wameacha majumba pale<br />

kwa miaka mingi, wametuachia urithi sisi watoto, leo tunaambiwa kwamba hamwezi kutupimia,<br />

mkatupa hati eti kwa sababu Mikindani iko below sea water. Hivi Bagamoyo, Kilwa, Lindi na<br />

maeneo mengine ya Zanzibar hayafanani kabisa na Mikindani Kwa nini wenzetu wanapimiwa na<br />

wanapata hati, sisi tusipate<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumwambia Mheshimiwa Waziri kwamba ule Mji ni Mji<br />

wa kihistoria kuna wawekezaji wengi wanataka kuja kuwekeza, wanataka kujenga Mahoteli<br />

makubwa na kadhalika, lakini wanashindwa kwa sababu tunaambiwa kwamba hatuwezi kupima.<br />

Mheshimiwa Waziri tunaomba utufikirie utumie ujuzi wako na maarifa yako ili watu wa Mikindani<br />

sasa wapimiwe, wapate hati miliki ili na wao waweze kujidai pia. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Halmashauri ya Miji na Manispaa hakuna hati ya<br />

mashamba. Lakini sisi bado tuna vijiji ndani ya Manispaa yetu ya Mtwara Mikindani. Tuna kijiji<br />

ambacho kiko mbali na Mji kinaitwa Lwelu, Naliendele, Mbawalachini, Mkunjanguo, huko kote<br />

vijijini watu bado wana mashamba wanalima. Master plan yetu ya Mji kuweza kuwafikia kule<br />

inaweza ikachukua zaidi ya miaka 10 au 15. Lakini wale watu leo wanakosa kupimiwa wakapata<br />

hati hata za kimila. Mheshimiwa Waziri tunafanya nini miaka 10 mtu kukaa unasubiri mpaka master<br />

plan ya mji ifike kule, wale watu wanateseka. Leo mtu ana shamba lake zuri ambalo anapata<br />

mazao yake mazuri anakuja kukwama kwenye pembejeo anaambiwa kwamba lete dhamana ya<br />

shamba lenye hati hana dhamana, kwa hiyo, anashindwa kuendelea na anashindwa<br />

kujiendesha. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri, alifikirie pia suala hili kwamba hivi vijiji<br />

ambavyo viko katika Miji na vipo katika Manispaa ambayo master plan yetu kufikia kule itachukua<br />

muda mrefu sana. Sasa tunamwomba sana atuangalie, halafu atujibu kwamba tunafanya ili wale<br />

watu nao wajisikie na waweze kupata hati hata kama ni za kimila.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo katika Ilani yetu ya Uchaguzi, ukurasa wa 60, tunasema<br />

kwamba tutapeleka huduma za Ofisi za Ardhi katika Mikoa na hususan imeelekeza kabisa<br />

kwamba tutapeleka huduma ya ardhi Kanda ya Mtwara kwa maana kwamba tuwe na ofisi ya<br />

Kamishina wa Mtwara. Ofisi ya Kamishina wa Mtwara imeanzishwa tangu mwaka jana, lakini ofisi<br />

hii haifanyi kazi. Watalaam wapo, wasiokuwa na kazi kwa kipindi chote cha mwaka mzima. Tatizo<br />

linasababishwa na kwamba Kamishna hayupo pale, Mheshimiwa Waziri hajateua Kamishna bado.<br />

Tuna ofisi ya kanda ipo, watalaam wapo lakini tatizo Kamishna hayupo. Sasa leo ukuaji wa<br />

Manispaa yetu ya Mtwara inakua sana na ile huduma ilikuwa ni kwa sababu ya Kanda ya Kusini,<br />

Mikoa yote ya Kusini iweze kupata huduma haraka pale. Leo ukitaka hati mtu yeyote wa Mtwara<br />

inachukua zaidi ya mwaka mmoja na nusu au miwili ndio unaweza kupata hati wakati tuna Ofisi<br />

ya Kanda iko pale lakini tatizo ni Kamishina.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Mheshimiwa Waziri ajibu na tunaomba amteue<br />

Kamishna haraka iwezekanavyo ili aweze kuja kutoa huduma ile pale ili tuweze kupata huduma za<br />

hati kwa muda mfupi. Ni kero sana Mheshimiwa Waziri kwa sababu pale hati zinasafirishwa mpaka<br />

Manispaa wakusanye zile hati, ziwe sijui 50 au ngapi, wachange nauli ndio wamtume mtu aje Dar<br />

es Salaam, wakati Ofisi ya Kanda iko pale lakini Kamishna tu hayupo. Kwa hiyo, tunamwomba<br />

sana Mheshimiwa Waziri.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina ombi maalum kwa Mheshimiwa Waziri, sisi pale kuna eneo<br />

ambalo tunazikana tunaita Makaburimswafa, lile eneo sasa limejaa, imefikia hatua sasa<br />

tunachimbua kaburi tunazika juu ya kaburi, ndio hatua tuliyofikia kwa sababu eneo limejaa.<br />

84

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!