28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Vijijini, Kinondoni, Mafia, Mkinga, Simanjiro, Musoma, Serengeti, Njombe na Makete. Vilevile, elimu<br />

hiyo ilitolewa kupitia maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Saba Saba na Nane Nane.<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha utayarishaji wa mion<strong>go</strong>zo ya utekelezaji wa sheria<br />

za ardhi. Kwa mwaka 2011/2012 mion<strong>go</strong>zo hiyo itasambazwa katika Halmashauri zote ili Watendaji<br />

waitumie katika kuboresha utekelezaji wa majukumu yao. Natoa wito kwa Halmashauri zote nchini<br />

kutenga fedha kwa ajili ya usimamizi na utekelezaji wa sheria hizo.<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Wizara yangu ilijiwekea len<strong>go</strong> la kusajili hati za<br />

kumiliki ardhi na nyaraka nyingine za kisheria zipatazo 50,000. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu<br />

kuwa hadi Juni, 2011 jumla ya hatimiliki na nyaraka za kisheria 59,544 zilisajiliwa. Kati ya nyaraka<br />

zilizosajiliwa, 22,923 ni hatimiliki, na 28,572 ni nyaraka zilizosajiliwa chini ya Sheria ya Usajili wa Ardhi<br />

(Sura ya 334). Vilevile, nyaraka 7,449 zilisajiliwa chini ya Sheria ya Usajili wa Nyaraka (Sura ya 117)<br />

na nyaraka 600 zilisajiliwa chini ya Sheria ya Usajili wa Rehani ya Mali Zinazohamishika (Sura ya 210).<br />

Kwa mwaka 2011/2012, Wizara ina len<strong>go</strong> la kusajili hatimiliki na nyaraka za kisheria 60,000. Kati ya<br />

hizo, 25,000 zinatarajiwa kuwa hatimiliki na 35,000 nyaraka nyingine za kisheria.<br />

Mheshimiwa Spika, mwaka 2010/2011 Wizara yangu ilikusudia kuifanyia marekebisho<br />

Sheria ya Usajili wa Ardhi na Sheria ya Usajili wa Nyaraka za Kisheria ili ziendane na mabadiliko ya<br />

sera na sheria nyingine za sekta ya ardhi. Napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kuwa rasimu za<br />

marekebisho ya sheria hizo zimetayarishwa. Kwa mwaka 2011/2012. Wizara inatarajia kuwasilisha<br />

Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria hizo baada ya kupata ridhaa ya Serikali.<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara iliendelea kufanya uthamini wa mali kwa ajili ya utozaji wa kodi<br />

ya pan<strong>go</strong> la ardhi, ushuru wa Serikali kutokana na mauzo au uhamisho wa mali na mizania ya<br />

makampuni na asasi, na kwa ajili ya uwekaji mali rehani, mirathi na bima. Jumla ya uthamini 8,872<br />

uliidhinishwa mwaka 2010/2011. Wizara yangu vilevile iliidhinisha taarifa za uthamini wa mali za<br />

wananchi walioguswa na miradi ya upanuzi wa barabara, uwekezaji katika mi<strong>go</strong>di na misitu, na<br />

maeneo ya upimaji wa viwanja. Uthamini pia ulifanyika katika eneo huru la uwekezaji (EPZ) lililopo<br />

Bagamoyo, eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya cha Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba<br />

Muhimbili huko Kwembe Mloganzila, Dar es Salaam na maeneo ya Mradi wa Mabasi yaendayo<br />

Kasi Jijini Dar es Salaam.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu imelenga kuthamini na<br />

kuidhinisha taarifa za uthamini wa mali zipatazo 13,000 kwa madhumuni mbalimbali. Uthamini<br />

utafanyika kwa ajili ya fidia ili kupisha utekelezaji wa miradi ya kitaifa kama vile mradi wa Mji Mpya<br />

wa Kigamboni na upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam katika eneo la Vijibweni, Kigamboni.<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha rasimu ya Sheria ya Uthamini na Usajili wa<br />

Wathamini. Kwa mwaka 2011/2012 Muswada wa Sheria hiyo utawasilishwa Bungeni baada ya<br />

kuridhiwa na Serikali. Kutungwa kwa sheria hiyo, pamoja na mambo mengine, kutaongeza uwazi<br />

katika shughuli za uthamini na kuongeza uwajibikaji wa wataalam wa uthamini nchini ili<br />

watekeleze kazi zao kwa weledi zaidi na kwa kuzingatia mazingira ya sasa ya kisera, kiuchumi na<br />

kijamii.<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Wizara yangu ilianza zoezi la kukusanya<br />

takwimu zitakazoiwezesha kukadiria vizuri zaidi thamani ya ardhi na mazao nchini kuanzia Mmkoa<br />

wa Dar es Salaam. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara itahuisha viwan<strong>go</strong> vya fidia nchini na kuanzisha<br />

mfumo wa kisasa wa Hazina ya Takwimu za Uthamini (Valuation Data Bank) ambao utawezesha<br />

uthamini wa mali kufanyika kwa uhakika na uwazi. Vilevile, Wizara itatoa mafunzo kwa wathamini<br />

wa Mikoa na Halmashauri juu ya ukokotoaji wa viwan<strong>go</strong> vya thamani ya ardhi, mazao na<br />

majen<strong>go</strong>.<br />

Mheshimiwa Spika, tangu wazo la kuanzisha hazina ya ardhi libuniwe mwaka 2002, Wizara<br />

yangu kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Mikoa na Halmashauri imefanya zoezi la kutambua<br />

ardhi inayofaa kuingizwa katika hazina hiyo ili itumike kwa ajili ya uwekezaji. Ili kutimiza len<strong>go</strong> la<br />

kuwa na hazina ya ardhi, ardhi yake inatakiwa kuwa imepangwa, imepimwa na kusajiliwa, haina<br />

m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro kuhusu umiliki wala matumizi yake, iko karibu na huduma za msingi na miundombinu, au<br />

23

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!