28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, kabla sijamwita Mheshimiwa Hasnain Murji<br />

nimeletewa tangazo na Ofisi ya Bunge, naomba niwasomee kama ifuatavyo: Nyumba za Kuishi<br />

Kwenye Mradi Medeli. Naomba uwatangazie Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> kuwa Waziri wa Ardhi na<br />

Maendeleo ya Makazi anawajulisha Wa<strong>bunge</strong> wote kuwa Wizara yake kupitia Shirika la Nyumba<br />

la Taifa (National Housing Cooperation) wapo hapa Bungeni kwa ajili ya kuuza nyumba za kuishi<br />

kwenye mradi wa Medeli uliozinduliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu tarehe 13 A<strong>go</strong>sti, 2011. Kituo<br />

cha Mauzo kipo kwenye viwanda vya maonyesho ya Bunge kuelekea jen<strong>go</strong> la habari, Wa<strong>bunge</strong><br />

wote mnakaribishwa kupata maelezo zaidi na kuchukua fomu na kuziwasilisha kwa Kaimu Katibu<br />

wa Bunge, Ndugu John Joel.<br />

MHE. HASNAIN M. MURJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami nichukue nafasi hii<br />

kwanza kukushukuru wewe Mwenyekiti kwa kunipa nafasi jioni hii ili niweze kutoa mchan<strong>go</strong> wangu.<br />

Lakini naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwenye rehema nyingi ambaye<br />

ameweza kunifikisha siku ya leo na kuweza kusimama hapa na kuweza kuja kutoa mchan<strong>go</strong><br />

wangu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri kwa Hotuba<br />

yake, nimeisoma, nimeridhika nayo, namshukuru na nampongeza. Lakini pamoja na kumpongeza<br />

nina imani kubwa kwa kipindi kifupi alichokaa Wizarani tumeanza kuona dalili na tumeanza kuona<br />

mabadiliko. Tunaomba Mheshimiwa Waziri, akaze buti. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na kumpongeza naomba nichukue nafasi hii<br />

kutokuunga mkono hoja. Siungi mkono hoja kwa sababu kuna vitu nimetumwa na wapiga kura<br />

wangu, nitakapopata majibu basi nitaunga mkono hoja hii. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Mji wa Mtwara Mikindani, ulipata hadhi ya kuwa Mji<br />

Mwaka 1963. Ndipo ikaanzishwa Halmashauri ya Mji wa Mtwara Mikindani. Hata hivyo, Historia ya<br />

Mji huu ilianzia mwaka 1948 wakati Serikali ya Kikoloni ya Mwingereza ilipoamua kuihamisha<br />

Bandari kutoka Mikindani na kuileta Mtwara kwa vile ilikuwa bandari kubwa (Deep Labour) hapo<br />

ndipo Mji ukaanza kuendelezwa. Hiyo ni mwaka 1963. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2004, tukaja kupata heshima ya Manispaa ya Mtwara-<br />

Mikindani. Lakini heshima hii tuliyopata ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani kulikuwa na vigezo,<br />

kulikuwa na masharti ambayo lazima yafanyike ili tuweze kupata hadhi ya Manispaa. Sharti<br />

mojawapo ni kwamba, tulikuwa hatukidhi hadhi za watu na vitu vingine. Kuweza kukidhi haja ya<br />

kuweza kupata Manispaa basi tulipanga tuweze kupata Kata mbili kutoka Halmashauri ya Mtwara<br />

Vijijini ambayo ni Kata ya Ziwani na Kata ya Namayanga.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama mbele yako hapa leo, ninao muhstari wa vikao<br />

ambayo Waheshimiwa Madiwani wa Mabaraza walikaa, walikubaliana kwamba, hizi Kata mbili<br />

sasa zije ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, wakakubaliana Vikao vya RCC, vimekaa<br />

vikakubaliana, tukaleta huku juu wakakubali na wakasema sasa Kata hizi zitatoka Mtwara Vijijini na<br />

kuja Manispaa ya Mtwara Mikindani. Nasikitika kusema tangu mwaka 2004 mpaka leo Kata hizi<br />

hazijafika bado Mtwara bado ziko huko ziliko. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuwa ana-windup basi<br />

aidha, aifute hadhi ya Manispaa ya Mtwara Mikindani hatuna hadhi kama Kata hizi mbili haziingii<br />

pale, la sivyo basi atamke sasa rasmi kwamba Kata ya Namayanga na Kata ya Ziwani ziko ndani<br />

ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani. Tunashindwa kufanya mambo mengi, Mheshimiwa Rais, juzi<br />

alikuwa yuko Mtwara ameongea na wawekezaji wakubwa, leo nchi hii na hata nchi mbalimbali<br />

inaiangalia Mtwara leo kwa jinsi rasilimali za gesi na Mungu akitujalia hata mafuta tutapata. Sasa<br />

hivi kila mtu anaiangalia Mtwara na sisi kuweza kupanga mji, ule mji ulishabana haya maeneo<br />

mengine tuliyoyaomba yaje basi ni ili tupange Mji, Mheshimiwa Waziri ili hawa wawekezaji wakija<br />

wasipate tabu.<br />

83

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!