Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, kabla sijamwita Mheshimiwa Hasnain Murji<br />
nimeletewa tangazo na Ofisi ya Bunge, naomba niwasomee kama ifuatavyo: Nyumba za Kuishi<br />
Kwenye Mradi Medeli. Naomba uwatangazie Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> kuwa Waziri wa Ardhi na<br />
Maendeleo ya Makazi anawajulisha Wa<strong>bunge</strong> wote kuwa Wizara yake kupitia Shirika la Nyumba<br />
la Taifa (National Housing Cooperation) wapo hapa Bungeni kwa ajili ya kuuza nyumba za kuishi<br />
kwenye mradi wa Medeli uliozinduliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu tarehe 13 A<strong>go</strong>sti, 2011. Kituo<br />
cha Mauzo kipo kwenye viwanda vya maonyesho ya Bunge kuelekea jen<strong>go</strong> la habari, Wa<strong>bunge</strong><br />
wote mnakaribishwa kupata maelezo zaidi na kuchukua fomu na kuziwasilisha kwa Kaimu Katibu<br />
wa Bunge, Ndugu John Joel.<br />
MHE. HASNAIN M. MURJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami nichukue nafasi hii<br />
kwanza kukushukuru wewe Mwenyekiti kwa kunipa nafasi jioni hii ili niweze kutoa mchan<strong>go</strong> wangu.<br />
Lakini naomba nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwenye rehema nyingi ambaye<br />
ameweza kunifikisha siku ya leo na kuweza kusimama hapa na kuweza kuja kutoa mchan<strong>go</strong><br />
wangu. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri kwa Hotuba<br />
yake, nimeisoma, nimeridhika nayo, namshukuru na nampongeza. Lakini pamoja na kumpongeza<br />
nina imani kubwa kwa kipindi kifupi alichokaa Wizarani tumeanza kuona dalili na tumeanza kuona<br />
mabadiliko. Tunaomba Mheshimiwa Waziri, akaze buti. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na kumpongeza naomba nichukue nafasi hii<br />
kutokuunga mkono hoja. Siungi mkono hoja kwa sababu kuna vitu nimetumwa na wapiga kura<br />
wangu, nitakapopata majibu basi nitaunga mkono hoja hii. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Mji wa Mtwara Mikindani, ulipata hadhi ya kuwa Mji<br />
Mwaka 1963. Ndipo ikaanzishwa Halmashauri ya Mji wa Mtwara Mikindani. Hata hivyo, Historia ya<br />
Mji huu ilianzia mwaka 1948 wakati Serikali ya Kikoloni ya Mwingereza ilipoamua kuihamisha<br />
Bandari kutoka Mikindani na kuileta Mtwara kwa vile ilikuwa bandari kubwa (Deep Labour) hapo<br />
ndipo Mji ukaanza kuendelezwa. Hiyo ni mwaka 1963. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2004, tukaja kupata heshima ya Manispaa ya Mtwara-<br />
Mikindani. Lakini heshima hii tuliyopata ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani kulikuwa na vigezo,<br />
kulikuwa na masharti ambayo lazima yafanyike ili tuweze kupata hadhi ya Manispaa. Sharti<br />
mojawapo ni kwamba, tulikuwa hatukidhi hadhi za watu na vitu vingine. Kuweza kukidhi haja ya<br />
kuweza kupata Manispaa basi tulipanga tuweze kupata Kata mbili kutoka Halmashauri ya Mtwara<br />
Vijijini ambayo ni Kata ya Ziwani na Kata ya Namayanga.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama mbele yako hapa leo, ninao muhstari wa vikao<br />
ambayo Waheshimiwa Madiwani wa Mabaraza walikaa, walikubaliana kwamba, hizi Kata mbili<br />
sasa zije ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, wakakubaliana Vikao vya RCC, vimekaa<br />
vikakubaliana, tukaleta huku juu wakakubali na wakasema sasa Kata hizi zitatoka Mtwara Vijijini na<br />
kuja Manispaa ya Mtwara Mikindani. Nasikitika kusema tangu mwaka 2004 mpaka leo Kata hizi<br />
hazijafika bado Mtwara bado ziko huko ziliko. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuwa ana-windup basi<br />
aidha, aifute hadhi ya Manispaa ya Mtwara Mikindani hatuna hadhi kama Kata hizi mbili haziingii<br />
pale, la sivyo basi atamke sasa rasmi kwamba Kata ya Namayanga na Kata ya Ziwani ziko ndani<br />
ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani. Tunashindwa kufanya mambo mengi, Mheshimiwa Rais, juzi<br />
alikuwa yuko Mtwara ameongea na wawekezaji wakubwa, leo nchi hii na hata nchi mbalimbali<br />
inaiangalia Mtwara leo kwa jinsi rasilimali za gesi na Mungu akitujalia hata mafuta tutapata. Sasa<br />
hivi kila mtu anaiangalia Mtwara na sisi kuweza kupanga mji, ule mji ulishabana haya maeneo<br />
mengine tuliyoyaomba yaje basi ni ili tupange Mji, Mheshimiwa Waziri ili hawa wawekezaji wakija<br />
wasipate tabu.<br />
83