28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(ii) Naomba nifanye masahihisho, Mwendamtitu siyo kijiji, ni intake ambayo<br />

inategemewa kujengwa. Kwa vile shamba la NAFCO Mbarali lilipokuwa linabinafsishwa, Serikali<br />

iliahidi kwamba itawajengea intake ambayo ndiyo inaitwa Mwendamtitu ambayo itasaidia Kata<br />

za Rujewa, Ubaruku, Usongwe, Malilo na Mapo<strong>go</strong>lo kwa Vijiji vya Msesule na Itamba. Sasa hivi<br />

toka Serikali imetoa ahadi hiyo, bado utekelezaji wake haujaonekana na hivyo kusababisha<br />

m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro mkubwa kati ya wawekezaji na wananchi, na sasa hivi bajeti iliyotengwa ni Shilingi<br />

milioni 500 ambayo nina uhakika haiwezi kujenga intake ile. Je, Serikali ina jitahada gani nyingine<br />

za ziada kuona fedha hizo zinaongezeka na hiyo intake inajengwa ili wale wananchi<br />

wasiendelee kupata shida na kuwa na m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro na mwezekaji<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />

CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika majibu ya msingi, tayari<br />

Serikali imetenga Shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuboresha maeneo aliyoyataja Mheshimiwa<br />

M<strong>bunge</strong>. Namwomba Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> aende kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri wa<br />

Kilimo, Chakula na Ushirika, ukurasa wa 120, jedwali Na. 5 ataona hizo Shilingi milioni 500 ziko pale.<br />

Lakini pamoja na hayo, Serikali inahakikisha kwamba, inayaboresha hayo maeneo hatua kwa<br />

hatua kulingana na fedha zinavyopatikana.<br />

MHE. MICHAEL L. LAIZER: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali<br />

moja la nyongeza. Kwa kuwa, kuna mashamba ya NAFCO ambayo yalikuwa mashamba ya<br />

mifu<strong>go</strong>, na sasa hakuna mifu<strong>go</strong> na Serikali inataka kuyabinafsisha: Je, isingekuwa busara kwa<br />

Serikali kutenga maeneo ya kuwapa wafugaji wanaozunguka maeneo hayo ili nao wafugie<br />

mifu<strong>go</strong><br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />

CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, Serikali inapobinafsisha inakuwa na mpan<strong>go</strong> mkakati<br />

wa kuhakikisha kwamba wananchi wanaozunguka maeneo yalipo mashamba na wao<br />

wanafikiriwa katika kuhakikisha kwamba wanaendelea na shughuli zao kama kawaida. Kwa hiyo,<br />

maeneo hayo yatakavyobinafsishwa nimhakikishie Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba, suala hilo<br />

alilolisema litaangaliwa na kuhakikisha kwamba wananchi hawapati bugudha kama ambavyo<br />

amependekeza.<br />

MHE. CLARA D. MWATUKA aliuliza:-<br />

Na. 419<br />

Makato ya Zao la Korosho<br />

Ni kawaida kwa mnunuzi yeyote wa mazao ya nafaka kutafuta soko na kusafirisha mazao<br />

hayo: Je, ni kwanini muuzaji wa zao la korosho hulazimishwa kugharamia vifaa kama magunia,<br />

usafi wa ghala, usafirishaji pamoja na makato mbalimbali bila maridhiano<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />

CHAKULA NA USHIRIKA) alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika napenda kujibu<br />

swali la Mheshimiwa Clara Diana Mwatuka, M<strong>bunge</strong> wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-<br />

Mheshimiwa Spika, zao lolote linapopelekwa sokoni huwa na gharama zake ambazo<br />

haziwezi kukwepeka. Baadhi ya gharama hizo ni pamoja vibebeo, utunzaji ghalani, usafirishaji,<br />

usimamizi na uendeshaji. Katika kuuza korosho pia kuna gharama na makato mengine ya kisheria<br />

sawa na mazao mengine yanayozalishwa nchini.<br />

Mheshimiwa Spika, wakulima wa korosho huuza korosho zao kupitia mawakala wao<br />

ambao ni Vyama vya Ushirika au Vyama vya Wakulima. Mawakala hao hukusanya korosho na<br />

kuzipeleka sokoni kwa maridhiano yao. Wakulima hulipwa malipo ya bei dira (indicative price) na<br />

pia hulipwa malipo yatokanayo na bei ya soko au mnadani baada ya kutolewa gharama<br />

zilizotajwa hapo juu.<br />

6

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!