Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kawaida huzalisha wadudu wanaoshambulia pamba na hivyo kufanya gharama ya kulima<br />
pamba na mapato yanayopatikana kwa wakulima wa pamba kuwa chini zaidi.<br />
Mheshimiwa Spika, kwa sababu hiyo, ni marufuku kwa kweli kuchanganya pamba na<br />
mahindi, na kwamba vion<strong>go</strong>zi wa kisiasa wanaowaambia wakulima wa kule wachanganye,<br />
hawawasaidii sana katika kuzingatia misingi ya kilimo bora. Kwa hiyo, ni vizuri walime pamba mbali<br />
na mahindi mbali.<br />
sana.<br />
SPIKA: Inatosha! Kweli nimekumbuka kwamba huyu alikuwa Waziri wa Kilimo. Nashukuru<br />
Na. 420<br />
Kuendeleza Ufugaji Nyuki<br />
MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI aliuliza:-<br />
Ufugaji Nyuki Kahama na Bukombe ni shughuli ya kiuchumi yenye tija kwa watu wengi<br />
kwenye maeneo hayo.<br />
(a)<br />
kisasa zaidi<br />
Je, Serikali ina mpan<strong>go</strong> gani wa kuendeleza na kuboresha ufugaji nyuki ili uwe wa<br />
(b) Serikali ina mpan<strong>go</strong> gani wa kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo ili wawe<br />
na mizinga mingi zaidi na viwanda vido<strong>go</strong> vido<strong>go</strong> vya kusafisha asali na kuifungasha kwenye<br />
chupa/makopo maalum ili kuiuza nje ya nchi<br />
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-<br />
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Kulikoyela K. Kahigi, M<strong>bunge</strong><br />
wa Bukombe, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-<br />
(a) Serikali inayo mipan<strong>go</strong> ya kuendeleza shughuli za ufugaji nyuki, ikiwa ni pamoja na<br />
kuanzisha miradi ya kuendeleza ufugaji nyuki katika Wilaya 30, ambapo Wilaya za Kahama na<br />
Bukombe ni kati ya Wilaya hizo. Len<strong>go</strong> la kuanzisha miradi hiyo ni kuhakikisha kuwa shughuli za<br />
ufugaji nyuki zinakuwa za kisasa zaidi ili kukuza uzalishaji wa mazao ya nyuki.<br />
Katika kuendeleza Miradi hiyo, Wizara imekuwa ikitenga fedha kiasi cha Shilingi milioni 150<br />
kila mwaka kuanzia mwaka 2007/2008 hadi hivi sasa. Fedha hizo hutumika kutoa elimu ya ufugaji<br />
nyuki na kuwawezesha wafugaji nyuki kuanzisha vikundi vido<strong>go</strong> vido<strong>go</strong> vya ufugaji nyuki<br />
sambamba na kuwapatia mizinga ya kisasa na mavazi ya kinga. Aidha, Serikali kwa kushirikiana<br />
na sekta binafsi imekuwa ikitoa mafunzo ya ubora, usalama na mfumo wa ufuatiliaji asali kama<br />
kigezo cha kupata soko la ndani na nje.<br />
Pia, Serikali kupitia Wizara yangu, imekuwa ikiandaa maonyesho ya asali kila mwaka kwa<br />
len<strong>go</strong> la kuwakutanisha wafugaji nyuki, wataalam wa nyuki na watengenezaji wa vifaa bora vya<br />
ufugaji wa nyuki. Katika maonyesho ya asali ya mwaka 2009 yaliyofanyika Dar es Salaam, jumla ya<br />
wafugaji nyuki watano kutoka Wilaya za Bukombe na Kahama walishiriki.<br />
(b) Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa kuwawezesha wananchi wa<br />
maeneo ya Bukombe, Kahama na maeneo mengine nchini, Serikali imewezesha vikundi<br />
mbalimbali vya wananchi wa kuvipatia mizinga ya mfano ili waweze kutengeneza mizinga yao<br />
wenyewe kwa kuwatumia mafundi seremala walioko kwenye vijiji vyao.<br />
Katika kipindi cha mwaka 2009/2010, Serikali ilitoa mavazi ya kinga 15 yenye thamani ya<br />
Sh. 975,000/= pamoja na mizinga 48 yenye thamani ya Sh. 1,440,000/= kwa vikundi vitano vya<br />
wafugaji nyuki Wilayani Kahama. Vikundi vilivyonufaika ni vya ufugaji nyuki Matumaini (kijiji cha<br />
8