28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

siku nyingine ukasema sasa tuusogeze mpaka, haiwezekani Sheria yake ni ngumu! Sasa wakati ni<br />

huu kwa Wizara husika kuona kuwa inalinda maeneo ya wananchi ili kusudi baadaye wasije kuwa<br />

watumwa ndani ya nchi yao.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nikija Kata ya Igava. Kata hiyo vijiji vyote vya pale<br />

vilionekana vinakuwa ni hifadhi lakini namshukuru sana Waziri Mkuu baada ya kutangaza, wale<br />

wananchi wamehangaika, wamechanga fedha nyingi, kesi wamepeleka Mahakamani kujinasua<br />

lakini nafikiri imefikia pazuri sasa karibu lile jambo litaisha. Nashukuru sana Serikali kwa hilo. Kata ya<br />

Rujewa maeneo ya Nyelegeti, Kata ya Songwe Imalilo maeneo ya Mahon<strong>go</strong>le, Mwanalala,<br />

Maningu, Mnazi nayo yalitaka kuchukuliwa hivihivi, wale wananchi wamehamishwa mara ya<br />

kwanza, wakahamishwa mara ya pili na sasa wangehamishwa ingekuwa mara ya tatu. Nchi hii<br />

ndugu zangu tunataka kufanya nini, hawa wananchi wetu tusipoangalia kuna siku watakuja kuwa<br />

watumwa.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo ukienda Kata ya Luhanga. Kata ya Luhanga<br />

nitaomba Waziri anayehusika mara baada ya Bunge akija pamoja na eneo hilo nitampeleka.<br />

Kata ya Luhanga wamevamia wajanja, wamefika pale wameongea na Watendaji wa Kata na<br />

Watendaji wa Vijiji wamechukua eneo kwa kuwadanganya kuwa tutawajengea Ofisi, tutafanya<br />

nini na wananchi kuja kushtuka hekta zaidi ya 8,000 wamepewa wale wakubwa kutoka huko<br />

sehemu mbalimbali sitaki kuwataja. Wananchi wamenituma na wameniomba nije niseme<br />

hawataki ardhi yao ichukuliwe. Nimejitahidi sana kufuata ngazi mbalimbali kwamba watatue<br />

kabla mimi sijalileta huku wale wananchi bado wananipigia kelele kwamba Mheshimiwa M<strong>bunge</strong><br />

kama hili eneo hutalisemea Bungeni usirudi huku, sasa mnataka niende wapi Kwa hiyo, ndugu<br />

zangu naomba wale wananchi wakasikilizwe wa Kata ya Luhanga wamechukuliwa ardhi yao na<br />

wajanja kwa kuwadanganya kwa kupitisha mihtasari kinyume na utaratibu. Naomba nalo<br />

lishughulikiwe.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo la shamba la mwekezaji la Kapunga. Mwekezaji yule<br />

alipewa hekta 5,500 ndio kisheria na zabuni yake ndivyo ilivyokuwa inatamka lakini baadaye<br />

wanapokabidhiwa lile shamba akakabidhiwa hekta 7,370. Sasa wale wananchi wakajikuta eneo<br />

la makazi yao ambalo ni hekta 1,070 amepewa mwekezaji. Eneo la small holder hekta 8,000<br />

amepewa mwekezaji. Sasa wanasema hivi kumbe tumekuwa tunauzwa tuko hapahapa. Hili liko<br />

peupe tu hata hesabu mtu asiyeenda shule linaeleweka, kama alipewa hekta 5,500 ilikuwaje<br />

apate hekta 7,370 Nalo hili wananchi wale wamenituma kwamba kabla sijarudi wanataka<br />

kupata majibu sasa na majibu mimi sina naomba nielezwe leo ni hatua gani zinachukuliwa<br />

kuhakikisha lile eneo la wananchi linatenganishwa na mwekezaji ili kuondoa kero na mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi ina kazi kubwa. Eneo la mwekezaji pale baada<br />

ya lile shamba kuchukuliwa, Mheshimiwa Baba wa Taifa alikuwa na roho nzuri, kila walipowekeza<br />

Shamba la Taifa aliandaa miundombinu mbalimbali wananchi wasaidiwe, sasa hivi miundombinu<br />

hiyo haipo. Sasa wameniomba wananchi wa Chimara na Kapunga yenyewe, Mwashikamile,<br />

Yala, Kwambaa wanataka eneo la Mpunga ambalo lina zaidi ya hekta 4,000 waboreshewe ili<br />

waweze kulima baada ya kuchukuliwa shamba ambalo walikuwa wanalitegemea.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mwaishikamile vilevile wanaomba waboreshewe,<br />

wananchi wa Yala wanaomba waboreshewe miundombinu yao. Nasema haya kwa uchungu<br />

sana kwa sababu tusipoangalia nchi hii mwishoni tutapigana. Tutasema wananchi sio watii wa<br />

sheria kumbe sisi wenyewe tunawakosea. Kwa hiyo, naomba kwa dhati kabisa na Mheshimiwa<br />

Waziri samahani nakutaja nitakuomba ufike twende wote nikupeleke ukaone hali<br />

ninayoizungumza.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyasema hayo …<br />

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)<br />

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Najua hiyo ni kengele ya kwanza.<br />

MWENYEKITI: Ni kengele ya pili Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>.<br />

68

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!