Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
siku nyingine ukasema sasa tuusogeze mpaka, haiwezekani Sheria yake ni ngumu! Sasa wakati ni<br />
huu kwa Wizara husika kuona kuwa inalinda maeneo ya wananchi ili kusudi baadaye wasije kuwa<br />
watumwa ndani ya nchi yao.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nikija Kata ya Igava. Kata hiyo vijiji vyote vya pale<br />
vilionekana vinakuwa ni hifadhi lakini namshukuru sana Waziri Mkuu baada ya kutangaza, wale<br />
wananchi wamehangaika, wamechanga fedha nyingi, kesi wamepeleka Mahakamani kujinasua<br />
lakini nafikiri imefikia pazuri sasa karibu lile jambo litaisha. Nashukuru sana Serikali kwa hilo. Kata ya<br />
Rujewa maeneo ya Nyelegeti, Kata ya Songwe Imalilo maeneo ya Mahon<strong>go</strong>le, Mwanalala,<br />
Maningu, Mnazi nayo yalitaka kuchukuliwa hivihivi, wale wananchi wamehamishwa mara ya<br />
kwanza, wakahamishwa mara ya pili na sasa wangehamishwa ingekuwa mara ya tatu. Nchi hii<br />
ndugu zangu tunataka kufanya nini, hawa wananchi wetu tusipoangalia kuna siku watakuja kuwa<br />
watumwa.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo ukienda Kata ya Luhanga. Kata ya Luhanga<br />
nitaomba Waziri anayehusika mara baada ya Bunge akija pamoja na eneo hilo nitampeleka.<br />
Kata ya Luhanga wamevamia wajanja, wamefika pale wameongea na Watendaji wa Kata na<br />
Watendaji wa Vijiji wamechukua eneo kwa kuwadanganya kuwa tutawajengea Ofisi, tutafanya<br />
nini na wananchi kuja kushtuka hekta zaidi ya 8,000 wamepewa wale wakubwa kutoka huko<br />
sehemu mbalimbali sitaki kuwataja. Wananchi wamenituma na wameniomba nije niseme<br />
hawataki ardhi yao ichukuliwe. Nimejitahidi sana kufuata ngazi mbalimbali kwamba watatue<br />
kabla mimi sijalileta huku wale wananchi bado wananipigia kelele kwamba Mheshimiwa M<strong>bunge</strong><br />
kama hili eneo hutalisemea Bungeni usirudi huku, sasa mnataka niende wapi Kwa hiyo, ndugu<br />
zangu naomba wale wananchi wakasikilizwe wa Kata ya Luhanga wamechukuliwa ardhi yao na<br />
wajanja kwa kuwadanganya kwa kupitisha mihtasari kinyume na utaratibu. Naomba nalo<br />
lishughulikiwe.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo la shamba la mwekezaji la Kapunga. Mwekezaji yule<br />
alipewa hekta 5,500 ndio kisheria na zabuni yake ndivyo ilivyokuwa inatamka lakini baadaye<br />
wanapokabidhiwa lile shamba akakabidhiwa hekta 7,370. Sasa wale wananchi wakajikuta eneo<br />
la makazi yao ambalo ni hekta 1,070 amepewa mwekezaji. Eneo la small holder hekta 8,000<br />
amepewa mwekezaji. Sasa wanasema hivi kumbe tumekuwa tunauzwa tuko hapahapa. Hili liko<br />
peupe tu hata hesabu mtu asiyeenda shule linaeleweka, kama alipewa hekta 5,500 ilikuwaje<br />
apate hekta 7,370 Nalo hili wananchi wale wamenituma kwamba kabla sijarudi wanataka<br />
kupata majibu sasa na majibu mimi sina naomba nielezwe leo ni hatua gani zinachukuliwa<br />
kuhakikisha lile eneo la wananchi linatenganishwa na mwekezaji ili kuondoa kero na mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi ina kazi kubwa. Eneo la mwekezaji pale baada<br />
ya lile shamba kuchukuliwa, Mheshimiwa Baba wa Taifa alikuwa na roho nzuri, kila walipowekeza<br />
Shamba la Taifa aliandaa miundombinu mbalimbali wananchi wasaidiwe, sasa hivi miundombinu<br />
hiyo haipo. Sasa wameniomba wananchi wa Chimara na Kapunga yenyewe, Mwashikamile,<br />
Yala, Kwambaa wanataka eneo la Mpunga ambalo lina zaidi ya hekta 4,000 waboreshewe ili<br />
waweze kulima baada ya kuchukuliwa shamba ambalo walikuwa wanalitegemea.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mwaishikamile vilevile wanaomba waboreshewe,<br />
wananchi wa Yala wanaomba waboreshewe miundombinu yao. Nasema haya kwa uchungu<br />
sana kwa sababu tusipoangalia nchi hii mwishoni tutapigana. Tutasema wananchi sio watii wa<br />
sheria kumbe sisi wenyewe tunawakosea. Kwa hiyo, naomba kwa dhati kabisa na Mheshimiwa<br />
Waziri samahani nakutaja nitakuomba ufike twende wote nikupeleke ukaone hali<br />
ninayoizungumza.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyasema hayo …<br />
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)<br />
MHE. MODESTUS D. KILUFI: Najua hiyo ni kengele ya kwanza.<br />
MWENYEKITI: Ni kengele ya pili Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>.<br />
68