28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuongeza eneo nje ya Ukanda wa Kiuchumi Baharini katika<br />

mwaka wa 2010/2011 Wizara yangu iliendelea na mchakato wa kukamilisha andiko<br />

litakalowasilishwa Umoja wa Mataifa ili nchi yetu iweze kuongezewa eneo la ziada nje ya Ukanda<br />

wa Kiuchumi Baharini (Extended Continental Shelf). Andiko hilo lilikuwa liwasilishwe kabla ya tarehe<br />

13 Mei, 2011 lakini kutokana na tatizo la uharamia katika Bahari ya Hindi ukusanyaji wa takwimu za<br />

kijiolojia baharini kwa ajili ya andiko haukuweza kukamilika kwa wakati. Umoja wa Mataifa ulikubali<br />

kuongeza muda wa kuwasilisha andiko hadi tarehe 13 Novemba, 2011. Kwa mwaka 2011/2012<br />

Wizara itakamilisha andiko na kujiandaa kulitetea mbele ya Tume ya Mipaka ya Baharini<br />

(Commission on the Limits of the Continental Shelf). Nachukua fursa hii kushukuru vyombo vya ulinzi<br />

na usalama kwa ushirikiano waliotupa na hivyo kuwezesha kukamilika kwa kazi bila athari yoyote<br />

huko baharini. Ninatarajia kuon<strong>go</strong>za utetezi huo muhimu na nyeti kwenye Umoja wa Mataifa.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu upimaji wa viwanja na mashamba, katika mwaka 2010/2011<br />

Wizara yangu iliratibu na kuidhinisha upimaji wa viwanja 26,788 na mashamba 606, ikilinganishwa<br />

na len<strong>go</strong> la viwanja 50,000 na mashamba 100 Kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu inatarajia<br />

kuidhinisha upimaji wa viwanja 35,000 na mashamba 800. Ili kurahisisha urejeaji wa kumbukumbu<br />

za viwanja vilivyopimwa, Wizara imeandaa ramani moja unganishi (Cadastral Index Map) ya eneo<br />

la Mkoa wa Dar es Salaam. Ramani ndo<strong>go</strong> (survey plans) 2,321 zenye viwanja 15,188<br />

zimeunganishwa katika ramani hiyo kubwa na kuingizwa kwenye mfumo wa kielektroniki. Kwa<br />

mwaka 2011/2012 ramani unganishi zitaandaliwa kwa ajili ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya<br />

Moro<strong>go</strong>ro. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Kupima Viwanja (Plot Development Revolving Fund)<br />

unaendelea kuzisaidia Halmashauri mbalimbali nchini kupima viwanja kwa kuzipatia mikopo kwa<br />

ajili hiyo. Kuanzia Julai, 2000 hadi Juni, 2011 Wizara ilitoa mikopo ya jumla ya shilingi 1,101,353,518<br />

kwa Halmashauri 42. Jumla ya shilingi 651,758,143 zimerejeshwa na shilingi 642,130,579 bado<br />

hazijarejeshwa kati ya fedha zilizorejeshwa, shilingi 267,151,348 zilirejeshwa mwaka 2010/2011<br />

kutoka kwenye Halmashauri 12.<br />

Mheshimiwa Spika, tangu mwaka 2005, kupitia Mradi wa Kupima Viwanja 20,000 katika Jiji<br />

la Dar es Salaam, Wizara yangu ilizikopesha Halmashauri saba jumla ya shilingi bilioni 2.62.<br />

Halmashauri hizo ni za Manispaa ya Moro<strong>go</strong>ro (shilingi milioni 200); Jiji la Mwanza (shilingi milioni<br />

400); Mji wa Kibaha (shilingi milioni 220); Wilaya ya Bagamoyo (shilingi milioni 400); Manispaa ya<br />

Kinondoni (shilingi milioni 600); Manispaa ya Temeke (shilingi milioni 400) na Manispaa ya Ilala<br />

(shilingi milioni 400). Fedha hizo zilitolewa kwa ajili ya kuandaa michoro ya mipan<strong>go</strong> miji, kulipa<br />

fidia, kupima na kumilikisha viwanja. Hadi Juni, 2011 fedha hizo zilikuwa hazijarejeshwa.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya<br />

Fedha itaweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa Halmashauri zilizokopeshwa zinarejesha mikopo hiyo<br />

kwa wakati. Tunaendelea kushauriana na Wizara ya Fedha ili kuona uwezekano wa Halmashauri<br />

zinazodaiwa kurejesha mikopo hiyo moja kwa moja kutoka kwenye ruzuku zao zitakazotolewa na<br />

Wizara hiyo. Natoa wito kwa Halmashauri kutambua kwamba kushindwa kwao kurejesha mikopo<br />

hiyo kunaathiri utendaji kazi wa Wizara yangu na kuzinyima haki Halmashauri nyingine ambazo<br />

zingekopeshwa kama mikopo ingerejeshwa kwa wakati.<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu mipan<strong>go</strong> ya miji na vijiji, katika kuhakikisha kuwa makazi ya<br />

wananchi yanakuwa yenye ustawi na endelevu, Wizara yangu imeendelea kusimamia upangaji<br />

na uendelezaji wa miji na vijiji nchini kwa kuzingatia Sera ya Maendeleo ya Makazi ya mwaka<br />

2000, Sheria ya Mipan<strong>go</strong> Miji ya mwaka 2007, Sheria ya Mipan<strong>go</strong> ya Matumizi ya Ardhi ya mwaka<br />

2007 na Sheria ya Usajili wa Wataalam wa Mipan<strong>go</strong> Miji na Vijiji ya mwaka 2007. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu uandaaji na utekelezaji wa mipan<strong>go</strong> ya uendelezaji miji, katika<br />

kupanga miji, Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji huandaa<br />

mipan<strong>go</strong> ya jumla (General Planning Schemes) ya aina mbili kwa ajili ya kusimamia ukuaji na<br />

uendelezaji miji. Mipan<strong>go</strong> hiyo ni ya muda mrefu (Master Plans) ambayo hutoa mwon<strong>go</strong>zo wa<br />

uendelezaji kwa miaka ishirini na ya muda mfupi (Interim Land Use Plans) ambayo ni ya miaka<br />

kumi. Wizara vilevile huandaa mipan<strong>go</strong> ya uendelezaji upya wa maeneo mbalimbali ya miji<br />

27

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!