Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
1997. Na ili ardhi husika iweze kupatikana lazima kwanza itambuliwe, itangazwe kwenye Gazeti la<br />
Serikali na iwe allocated kwa Kituo cha Uwekezaji ambacho ndicho kitakuwa na jukumu la<br />
kumpatia mwekezaji.<br />
Mheshimiwa Spika, haya yote hayajafanyika na kinachotaka kufanyika kwa kutumia<br />
vibaraka wa kitanzani , ni kuhakikisha kwamba wabia (vibaraka) wa Kitanzania wanakuwa na<br />
hisa nyingi katika umiliki wa ardhi ili kuepuka kikwazo cha kupitia katika Kituo cha Uwekezaji.<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kuhusu mamlaka ya kuingia ubia (joint venture) na mwekezaji ambaye<br />
si Mtanzania kama ambavyo inaonekana ni kamchezo ambako kanataka kuchezwa na<br />
Serengeti Advisers Limited, mabadiliko ya Sheria ya Ardhi yaliyofanyika mwaka 2004, Sheria Na.<br />
2/2004 The Land (Amendment ) Act 2004 Kifungu cha 19(1), (2)(c) kinasema ili kufanikisha<br />
masharti ya uendelezaji wa ardhi, raia wa Tanzania anayemiliki ardhi anaweza kuingia joint<br />
venture na mwekezaji ambaye si raia wa Tanzania kwa madhumuni ya uwekezaji chini ya Sheria<br />
ya Uwekezaji, Sura ya 38. Kwa mujibu wa Kifungu hicho ubia unafanywa na mzawa na mgeni. Kwa<br />
mujibu wa Sheria ya Uraia (The Tanzanian Citizenship Act, Cap 357). Shirika la Umma au Kampuni<br />
au Halmashauri haiwezi kuwa na sifa za kuwa raia. Hivyo kwa mujibu wa kifungu 19(2)(c) si<br />
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda wala Kampuni ya Serengeti Advisers yenye uwezo wa kutoa<br />
ardhi yake kwa mtu ambaye si raia ili kuwekeza kwa pamoja. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelezo ya vifungu nilivyovitaja hapo juu (isipokuwa<br />
kama kuna mabadiliko ya sheria ambayo hadi sasa haifahamiki), Halmashauri ya Wilaya ya<br />
Mpanda na Kampuni ya Serengeti Advisers haina uwezo wa kuwekeza kwa pamoja (joint<br />
venture) na wawekezaji ambao si Watanzania mpaka hapo sheria zitakapofanyiwa<br />
marekebisho. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ituambie, ilitumia utaratibu gani wa kisheria<br />
kuingia mkataba huo wa kifedhuli na usio na maslahi hata kido<strong>go</strong> kwa Halmashauri ya Wilaya ya<br />
Mpanda na Taifa kwa ujumla Nani aliwatuma (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, suala la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji, kilimo na<br />
ufugaji ni ya sekta zinazoon<strong>go</strong>za kwa kutoa mchan<strong>go</strong> mkubwa sana katika Pato la Taifa,<br />
halikadhalika ndizo zinazoon<strong>go</strong>za kwa kutoa ajira kwani zaidi ya 80% ya Watanzania wamejiajiri<br />
katika sekta hii hasa vijijini. Hivyo basi kuboresha hizi sekta mbili maana yake ni kwamba tutakuwa<br />
tumeboresha 80% ya maisha ya Watanzania kwa kuwa na uhakika wa kipato, usalama wa<br />
chakula na kuongezeka kwa Pato la Taifa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, imekuwa ni jambo la kawaida kwa nchi yetu kutokea kwa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro<br />
baina ya wakulima na wafugaji, chanzo cha mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo ni kutokana na kutokuwa na mipan<strong>go</strong><br />
thabiti ya Serikali ili kubainisha/kutenganisha maeneo maalum kwa ajili ya wakulima, halikadhalika<br />
wafugaji. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, Sheria yetu ya Ardhi, Na. 4 na Na. 5 ya mwaka 1999 imeainisha<br />
utaratibu ambao miliki ya ardhi ya mtu mmoja mmoja ama kikundi inavyotambulika kisheria mijini<br />
na vijijini kisheria ama kimila. Hata hivyo utaratibu wa utwaaji na umiliki ardhi hasa vijijini kwa<br />
matumizi ya wafugaji, wachungaji na wawindaji haujaainishwa ipasavyo! Mikakati ya kutenga<br />
ardhi hasa ya wafugaji imekuwa finyu mno kiasi kwamba wakulima na wawekezaji wameendelea<br />
kuhodhi/kuvamia ardhi ya wafugaji kwa msaada wa mawakala wa Serikali. Na wakati mwingine<br />
wafugaji wamekuwa wakivamia maeneo ya wakulima kutokana na kukosa maeneo muafaka<br />
kwa ajili ya malisho. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, tafiti pia zimeonyesha kwamba ardhi ya wafugaji imekuwa ikichukuliwa<br />
kwa ajili ya matumizi ya wawekezaji, kugeuzwa kuwa Hifadhi za Taifa au Game Reserves!<br />
Matokeo yake wafugaji wanageuka watu wa kutangatanga! Wakati Serikali imekuwa ikiwataka<br />
wafugaji waondokane na njia za kizamani za kufuga, bado haijaonyesha njia mbadala za ufugaji<br />
wa kisasa!<br />
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali itueleze ina mikakati gani katika<br />
kuhakikisha kwamba maeneo rasmi ya wafugaji yanabainishwa ili kuepusha umwagaji damu na<br />
49