28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

1997. Na ili ardhi husika iweze kupatikana lazima kwanza itambuliwe, itangazwe kwenye Gazeti la<br />

Serikali na iwe allocated kwa Kituo cha Uwekezaji ambacho ndicho kitakuwa na jukumu la<br />

kumpatia mwekezaji.<br />

Mheshimiwa Spika, haya yote hayajafanyika na kinachotaka kufanyika kwa kutumia<br />

vibaraka wa kitanzani , ni kuhakikisha kwamba wabia (vibaraka) wa Kitanzania wanakuwa na<br />

hisa nyingi katika umiliki wa ardhi ili kuepuka kikwazo cha kupitia katika Kituo cha Uwekezaji.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu mamlaka ya kuingia ubia (joint venture) na mwekezaji ambaye<br />

si Mtanzania kama ambavyo inaonekana ni kamchezo ambako kanataka kuchezwa na<br />

Serengeti Advisers Limited, mabadiliko ya Sheria ya Ardhi yaliyofanyika mwaka 2004, Sheria Na.<br />

2/2004 The Land (Amendment ) Act 2004 Kifungu cha 19(1), (2)(c) kinasema ili kufanikisha<br />

masharti ya uendelezaji wa ardhi, raia wa Tanzania anayemiliki ardhi anaweza kuingia joint<br />

venture na mwekezaji ambaye si raia wa Tanzania kwa madhumuni ya uwekezaji chini ya Sheria<br />

ya Uwekezaji, Sura ya 38. Kwa mujibu wa Kifungu hicho ubia unafanywa na mzawa na mgeni. Kwa<br />

mujibu wa Sheria ya Uraia (The Tanzanian Citizenship Act, Cap 357). Shirika la Umma au Kampuni<br />

au Halmashauri haiwezi kuwa na sifa za kuwa raia. Hivyo kwa mujibu wa kifungu 19(2)(c) si<br />

Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda wala Kampuni ya Serengeti Advisers yenye uwezo wa kutoa<br />

ardhi yake kwa mtu ambaye si raia ili kuwekeza kwa pamoja. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelezo ya vifungu nilivyovitaja hapo juu (isipokuwa<br />

kama kuna mabadiliko ya sheria ambayo hadi sasa haifahamiki), Halmashauri ya Wilaya ya<br />

Mpanda na Kampuni ya Serengeti Advisers haina uwezo wa kuwekeza kwa pamoja (joint<br />

venture) na wawekezaji ambao si Watanzania mpaka hapo sheria zitakapofanyiwa<br />

marekebisho. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ituambie, ilitumia utaratibu gani wa kisheria<br />

kuingia mkataba huo wa kifedhuli na usio na maslahi hata kido<strong>go</strong> kwa Halmashauri ya Wilaya ya<br />

Mpanda na Taifa kwa ujumla Nani aliwatuma (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, suala la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji, kilimo na<br />

ufugaji ni ya sekta zinazoon<strong>go</strong>za kwa kutoa mchan<strong>go</strong> mkubwa sana katika Pato la Taifa,<br />

halikadhalika ndizo zinazoon<strong>go</strong>za kwa kutoa ajira kwani zaidi ya 80% ya Watanzania wamejiajiri<br />

katika sekta hii hasa vijijini. Hivyo basi kuboresha hizi sekta mbili maana yake ni kwamba tutakuwa<br />

tumeboresha 80% ya maisha ya Watanzania kwa kuwa na uhakika wa kipato, usalama wa<br />

chakula na kuongezeka kwa Pato la Taifa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni jambo la kawaida kwa nchi yetu kutokea kwa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro<br />

baina ya wakulima na wafugaji, chanzo cha mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo ni kutokana na kutokuwa na mipan<strong>go</strong><br />

thabiti ya Serikali ili kubainisha/kutenganisha maeneo maalum kwa ajili ya wakulima, halikadhalika<br />

wafugaji. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Sheria yetu ya Ardhi, Na. 4 na Na. 5 ya mwaka 1999 imeainisha<br />

utaratibu ambao miliki ya ardhi ya mtu mmoja mmoja ama kikundi inavyotambulika kisheria mijini<br />

na vijijini kisheria ama kimila. Hata hivyo utaratibu wa utwaaji na umiliki ardhi hasa vijijini kwa<br />

matumizi ya wafugaji, wachungaji na wawindaji haujaainishwa ipasavyo! Mikakati ya kutenga<br />

ardhi hasa ya wafugaji imekuwa finyu mno kiasi kwamba wakulima na wawekezaji wameendelea<br />

kuhodhi/kuvamia ardhi ya wafugaji kwa msaada wa mawakala wa Serikali. Na wakati mwingine<br />

wafugaji wamekuwa wakivamia maeneo ya wakulima kutokana na kukosa maeneo muafaka<br />

kwa ajili ya malisho. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, tafiti pia zimeonyesha kwamba ardhi ya wafugaji imekuwa ikichukuliwa<br />

kwa ajili ya matumizi ya wawekezaji, kugeuzwa kuwa Hifadhi za Taifa au Game Reserves!<br />

Matokeo yake wafugaji wanageuka watu wa kutangatanga! Wakati Serikali imekuwa ikiwataka<br />

wafugaji waondokane na njia za kizamani za kufuga, bado haijaonyesha njia mbadala za ufugaji<br />

wa kisasa!<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali itueleze ina mikakati gani katika<br />

kuhakikisha kwamba maeneo rasmi ya wafugaji yanabainishwa ili kuepusha umwagaji damu na<br />

49

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!