28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa kazi za Shirika la Nyumba la<br />

Taifa kuanzia Julai, 2010 hadi Mei, 2011 wanatarajia kupata shilingi bilioni 6.3 kutokana na mauzo<br />

ya nyumba hizo yaani faida ya shilingi bilioni 1.9 kwa tafsiri nyingine nyumba moja itauzwa na<br />

Shirika la Nyumba kwa shilingi milioni 129.2, wakati gharama halisi za ujenzi ni shilingi milioni 83. Kwa<br />

kila nyumba iliyounzwa shirika limepata faida ya shilingi milioni 46.<br />

Mheshimiwa Spika, mustakabali wa nyumba za Shirika la Nyumba, hivi karibuni kumekuwa<br />

na sintofahamu nyingi kuhusiana na nyumba za shirika. Wapangaji (hususan katika maeneo ya<br />

katikati ya miji) wamekuwa wakilitaka shirika liwauzie nyumba. Kambi ya upinzani inaitaka serikali<br />

itoe kauli, nini msimamo wake kuhusiana na suala hili, lakini sisi tunaona kuwa hakuna haja yoyote<br />

ya shirika hili kuuza nyumba hizo na badala yake iweke mkazo katika kujenga nyumba ambazo<br />

zitapangishwa kwa bei nafuu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mikopo yaani Government Loans, Guarantees and Grants<br />

Act 1974 and amendments 2003 inalifanya Shirika la Nyumba la Taifa kulazimika kupata kibali<br />

kutoka Wizara ya Fedha hata pale ambapo halihitaji kupata dhamana ya Serikali na pia hata kwa<br />

mikopo ya ndani ya nchi; wote tunafahamu rasilimali ambazo shirika hili linazo. Pamoja na<br />

kufahamu yote, bado tumeamua kuliweka shirika hili katika urasimu mkubwa wa Kiserikali wa<br />

kupata vibali kutoka Wizara ya Fedha bila ya sababu za lazima. Je, Serikali imedhamiria ya<br />

kutekeleza ahadi zake katika ujenzi wa nyumba na kuliwezesha shirika kujiendesha kibiashara<br />

kama sheria yake inavyolitaka Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali itoe ufafanuzi ni lini inatarajia<br />

kuanzisha mchakato wa kurekebisha sheria hiyo<br />

Mheshimiwa Spika, mpan<strong>go</strong> wa uendelezaji eneo la Kigamboni, tangu mwaka 2007,<br />

Wizara ilianza hatua za awali za kuendeleza Mji Mpya wa Kigamboni. Mradi huu unahusisha<br />

hekta 6500 linaloshirikisha kata tano za Kigamboni, Tungi, Mjimwema, Vijibweni, Kibada na mitaa<br />

miwili ya Mbwamaji na Kizani kwenye Kata ya Somangila. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, miaka minne imepita, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ibainishe ni lini<br />

hasa mradi huu utaanza na michakato ya fidia kwa wananchi imefikia wapi na ni utaratibu upi<br />

unaotumika kulipa fidia husika. Halikadhalika Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali kuhakikisha<br />

kwamba kunakuwepo kwa utaratibu ulio wa uwazi pasi na upendeleo kuhakikisha kwamba<br />

wananchi waishio ndani ya eneo la mpan<strong>go</strong> yaani wakazi wa kata zote tano wanabaki kwenye<br />

eneo hilo kama ambavyo madhumuni ya mpan<strong>go</strong> unavyoainisha. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani ina taarifa juu ya mchakato unaofanyika baina ya<br />

Serikali na Shirika la Nyumba la Taifa unaohusiana na uendelezaji wa eneo la Tanganyika Packers<br />

Kawe kama ilivyobainishwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wakati akijibu swali namba<br />

246, ambapo pamoja na mambo mengine alikiri kwamba katika eneo la Kawe kuna heka 180<br />

ambalo ni eneo la makazi na ambalo halikuuzwa na Serikali kwa mwekezaji. Kambi ya Upinzani<br />

inaitaka Serikali ifahamu kwamba eneo husika bado lina wakazi ambao walikuwa ni wafanyakazi<br />

wa Kiwanda cha Tanganyika Packers na hatua zozote za kuliendeleza eneo husika lazima<br />

uhakikishe unawahusisha kikamilifu wananchi hao ambao wameishi eneo hilo maisha yao yote.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mamlaka ya/wakala wa kuratibu bei za pan<strong>go</strong> la nyumba, kutokana<br />

na ongezeko kubwa la watu mijini, mahitaji ya nyumba za kupanga yamekuwa ni makubwa sana.<br />

Imekuwa ni jambo la kawaida kwa wenye nyumba kujipangia bei za kodi ya nyumba kwa kadri<br />

wanavyoona inafaa wao, kwa kuwa hakuna chombo cha kuwadhibiti. Matokeo yake kodi ya<br />

nyumba imegeuka mzi<strong>go</strong> mkubwa sana kwa wananchi wa kawaida. Kambi ya Upinzani inaitaka<br />

Serikali iweke utaratibu utakaotambulika kisheria utakaoweka mwon<strong>go</strong>zo na kuweza kudhibiti<br />

gharama za kodi za nyumba kwa ujumla wake. Kwa maana nyingine ni kuanzisha mamlaka ya<br />

udhibiti itakayoitwa Real Estate Regulatory Authority. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi<br />

(NHBRA), jukumu la Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (National<br />

Housing and Building Research Agency - NHBRA) ni kufanya tafiti, kuelimisha, kukuza, kushauri,<br />

kuhamasisha na kusambaza matokeo ya utafiti na utaalam wa ujenzi wa nyumba bora na za<br />

54

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!